Skip to main content

Wasemavyo wadau kuhusu Al Masry




SIMBA itakwea pipa kesho Jumatano kwenda Misri kumalizana na Al Masry katika mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika, lakini akili aliyofanya kocha wa timu hiyo, Pierre Lechantre imerahisisha kazi kwa vijana wake kuwa nyepesi kabisa.


Vinara hao wa Ligi Kuu Bara wanakwenda katika mchezo huo kusaka ushindi, baada ya kulazimishwa sare ya 2-2 kwenye mechi ya raundi ya kwanza.

Hata hivyo, kabla ya kuondoka jijini Dar es Salaam, Simba ilikataa kucheza mechi zake mbili za ligi dhidi ya Mtibwa Sugar na Njombe Mji tena za ugenini kwa kile ilichodaiwa ni agizo la Lechantre hivyo, kuzusha kelele nyingi mtaani.

Lakini, Kocha Abdallah Kibadeni ‘King’ amefichua alichokifanya Mfaransa huyo kuigomea timu yake kucheza mechi za ligi kabla ya kuvaana na Al Masry, ilikuwa ni akili ya maana kwelikweli. Pia, kwa akili hiyo Simba inaweza kupata ushindi ugenini kwani, kama wangecheza ingweza kuwaletea madhara zaidi.

“Wanacheza mechi ngumu na muhimu na wameipa uzito mkubwa ndio maana wameomba muda wa kutosha ili kujiandaa. Hiyo inaweza kuwa na faida kubwa kwao kwa kupata muda wa kutosha,” alisema Kibadeni na kuongeza;

“Kikosi cha Simba ni kipana, lakini wachezaji wao mahiri ambao wanafanya vizuri msimu huu, wengi ni majeruhi labda waliogopa hilo wanaweza kuwapoteza kama wangeumia kabla ya mechi hiyo.

“Kama watafanya maandalizi muhimu ya kimwili na kiakili itakuwa faida kuwa tayari kupambana na kupata matokeo ambayo wanatarajia, lakini wakishindwa kufanya hivyo wanaweza kushuka morali.”

Naye nyota wa zamani wa timu hiyo, Boniface Pawasa alisema; “Utaratibu huu ulikuwepo muda mrefu kwa timu inapokuwa na ratiba ngumu za kimataifa na Simba inaweza kuwa na faida ya kupata muda wa kutosha wa kujiandaa tofauti kama wangecheza mechi za ligi,

“Wanasafiri umbali mrefu kwenda Misri na muda waliokuwa nao unatosha kabisa kusafiri mapema na kuzoea mazingira na kama kutakuwa na fitna watakabiliana nazo,” alisema.

Hata hivyo, alisema Simba inaweza kupata hasara ya kuwapunguzia morali wachezaji wao kwani, wanapaswa kuwa fiti muda wote kwa maana ya kucheza uwanjani.

“Kama wangecheza mechi za ligi na kushinda ingewaongezea morali na hata wakienda Misri wangekuwa moto, ila kocha ametumia akili kufanya maamuzi hayo,” alisema.

Lakini, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ alikuwa na mtazamo tofauti kwa kusema; “Sidhani kama imefanya maamuzi sahihi, kwani itawaondolea ubora wachezaji kuelekea mchezo huo na wasishangae nyota wanaowategemea wakacheza vibaya dhidi ya Al Masry.

“Wanasema wanaogopa mastaa wao kuumia, hiyo ni mipango ya Mungu unaweza kuumia hata kama ukiwa nyumbani, hivyo Simba hawakuwa sahihi.”

Simba itakayokabiliana na Al Masrty kwenye mchezo huo, itaondoka nchini kesho Jumatano kabla ya Jumamosi kushuka Uwanja wa Port Said kuivaa Waarabu hao, ambao jana usiku walikuwa uwanjani kucheza mechi ya ligi ya nchi yao.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Poland’s GROM special services mastermind found dead

Brigadier General Slawomir Petelicki, responsible for the formation of the GROM special services unit in the 1990s, was found dead at his apartment, Saturday, with bullet wounds to the head. Sławomir Petelicki, 1946-2012. Photo: Archive/PAP/Radek Pietruszka Police spokesman Maciej Karczynski informed that Petelicki’s body was found by his wife in the garage of his Warsaw apartment on Saturday. He was 65. Primary investigations point to suicide as the cause of death. It is expected that prosecutors will decide on an investigation into Petelicki’s death on Monday. After examining the scene of the incident, “the body of General [Petelicki] has been taken to a forensic laboratory, although a post-mortem will probably take place on Monday,” prosecutor Katarzyna Calow-Jaszewska from the Warsaw District Prosecution told the PAP news agency. “He was a tough man, a brilliant soldier and commander,” Colonel Krzysztof Przepiorka, head of the ...