Skip to main content

Wasemavyo wadau kuhusu Al Masry




SIMBA itakwea pipa kesho Jumatano kwenda Misri kumalizana na Al Masry katika mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika, lakini akili aliyofanya kocha wa timu hiyo, Pierre Lechantre imerahisisha kazi kwa vijana wake kuwa nyepesi kabisa.


Vinara hao wa Ligi Kuu Bara wanakwenda katika mchezo huo kusaka ushindi, baada ya kulazimishwa sare ya 2-2 kwenye mechi ya raundi ya kwanza.

Hata hivyo, kabla ya kuondoka jijini Dar es Salaam, Simba ilikataa kucheza mechi zake mbili za ligi dhidi ya Mtibwa Sugar na Njombe Mji tena za ugenini kwa kile ilichodaiwa ni agizo la Lechantre hivyo, kuzusha kelele nyingi mtaani.

Lakini, Kocha Abdallah Kibadeni ‘King’ amefichua alichokifanya Mfaransa huyo kuigomea timu yake kucheza mechi za ligi kabla ya kuvaana na Al Masry, ilikuwa ni akili ya maana kwelikweli. Pia, kwa akili hiyo Simba inaweza kupata ushindi ugenini kwani, kama wangecheza ingweza kuwaletea madhara zaidi.

“Wanacheza mechi ngumu na muhimu na wameipa uzito mkubwa ndio maana wameomba muda wa kutosha ili kujiandaa. Hiyo inaweza kuwa na faida kubwa kwao kwa kupata muda wa kutosha,” alisema Kibadeni na kuongeza;

“Kikosi cha Simba ni kipana, lakini wachezaji wao mahiri ambao wanafanya vizuri msimu huu, wengi ni majeruhi labda waliogopa hilo wanaweza kuwapoteza kama wangeumia kabla ya mechi hiyo.

“Kama watafanya maandalizi muhimu ya kimwili na kiakili itakuwa faida kuwa tayari kupambana na kupata matokeo ambayo wanatarajia, lakini wakishindwa kufanya hivyo wanaweza kushuka morali.”

Naye nyota wa zamani wa timu hiyo, Boniface Pawasa alisema; “Utaratibu huu ulikuwepo muda mrefu kwa timu inapokuwa na ratiba ngumu za kimataifa na Simba inaweza kuwa na faida ya kupata muda wa kutosha wa kujiandaa tofauti kama wangecheza mechi za ligi,

“Wanasafiri umbali mrefu kwenda Misri na muda waliokuwa nao unatosha kabisa kusafiri mapema na kuzoea mazingira na kama kutakuwa na fitna watakabiliana nazo,” alisema.

Hata hivyo, alisema Simba inaweza kupata hasara ya kuwapunguzia morali wachezaji wao kwani, wanapaswa kuwa fiti muda wote kwa maana ya kucheza uwanjani.

“Kama wangecheza mechi za ligi na kushinda ingewaongezea morali na hata wakienda Misri wangekuwa moto, ila kocha ametumia akili kufanya maamuzi hayo,” alisema.

Lakini, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ alikuwa na mtazamo tofauti kwa kusema; “Sidhani kama imefanya maamuzi sahihi, kwani itawaondolea ubora wachezaji kuelekea mchezo huo na wasishangae nyota wanaowategemea wakacheza vibaya dhidi ya Al Masry.

“Wanasema wanaogopa mastaa wao kuumia, hiyo ni mipango ya Mungu unaweza kuumia hata kama ukiwa nyumbani, hivyo Simba hawakuwa sahihi.”

Simba itakayokabiliana na Al Masrty kwenye mchezo huo, itaondoka nchini kesho Jumatano kabla ya Jumamosi kushuka Uwanja wa Port Said kuivaa Waarabu hao, ambao jana usiku walikuwa uwanjani kucheza mechi ya ligi ya nchi yao.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.