Skip to main content

Jumuiya ya Wazazi Ilala yakerwa na watendaji wasiojua majukumu yao






Na Heri Shaaban

JUMUIYA ya Wazazi Wilaya ya  Ilala yakerwa na watendaji wasiojua majukumu yao..

Hayo yalisemwa Dar es salaam Jana, na Katibu wa Wazazi Wilaya ya Ilala Sophia Hamadi katika ziara ya kamati ya utekelezaji wilaya va Ilala walipokuwa jimboni SEGEREA kuangalia uhai wa jumuiya.

" Sirizishwi na nafasi zilizo wazi katika jumuiya hii ya wazazi has a kata ya SEGEREA " alisema Sophia


Alisema kila kazi INA misingi yake  ukichaguliwa lazima utekeleze majukumu sitaji kuona nafasi zinapwaya bila kuzibwa huyo  atakakuwa sio kiongozi ambaye yupo nyuma kimaendeleo .


Aidha Sophia alisema Mara. Baada ya ziara hiyo atashuka chini ngazi ya matawi kuangalia kama vikao vinafanyika.

Alisema  dhumuni lingine la ziara hiyo kujua idadi ya wazee waliopo kila kata, kujua idadi ya Shule na zahanati.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wazazi Wilaya ya Ilala Lucas Lutainurwa alizitaka kila jumuiya kuanzisha vikundi vya uzalishaji vitakavyowakomboa kiuchumi.

Lucas alisema jumuiya hiyo ikiwa na vikundi itasaidia  wanachama wake  kuendesha jumuiya hiyo bila kuwa ombaomba.

Wakati huo huo aliagiza 
Makundi yalio katika Jumuiya  hiyo Kuvunjwa   badala yake washirikiane katika kuongeza wanachama na kufatilia hada kwa wakati.

Alisema chaguzi zilishakwisha tushirikiane tuwe wamoja na kuakikisha idadi ya wanachama inaongezeka.

Comments