Skip to main content

Posts

Showing posts from 2018

Serikali yawakaribisha wafanyabiashara kununua korosho

  SERIKALI  kupitia kwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Joseph Kakunda imewakaribisha wafanyabiashara kununua korosho na kuzibangua.   Mbali na   uamuzi huo , Waziri Kakunda amesema Serikali  bado inaendelea kuingia mikataba na wabanguaji ili kupunguza mzigo wa korosho. Kakunda ametoa kauli hiyo wakati taarifa ya timu ya pamoja ya wataalamu kuhusu hali ya utekelezaji wa operesheni korosho iliyotolewa Novemba 27 ikionyesha kuwa itachukua muda mrefu  kubangua korosho za msimu huu. Novemba 12, Rais John Magufuli alitangaza Serikali kununua korosho yote kutoka kwa wakulima msimu huu kwa bei ya Sh3,300 kwa kilo. Licha ya Waziri Kakunda kusema haina shida kwa ubanguaji kuchukua muda mrefu, amewataka wafanyabiashara wanaoweza kubangua wenyewe wakae meza moja na Serikali ili wauziwe korosho. “Kama mtu anatokea popote iwe ndani au nje akasema mimi nataka ninunue korosho nikabangue mwenyewe, labda ana bei nzuri aje tuzungumze. Ije mvua, lije

TFDA imefanikiwa kufikia na kuvuka malengo iliyojiwekea

MAMLAKA ya chakula na dawa (TFDA), imefanikiwa kufikia na kuvuka malengo iliyojiwekea katika udhibiti wa ubora, usalama na ufanisi wa chakula, dawa, vipodozi, vifaa tiba na vitendendanishi ili kulinda afya ya jamii. TFDA imeweka mifumo na taratibu za ndani za utoaji huduma bora kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya ISO 9001:2015 kwa huduma za kawaida na ISO 17025:2005 kwa huduma za maabara. Hayo yamesemwa jana jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Adam Mitangu wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa kazi za udhibiti wa ubora,usalama na ufanisi wa bidhaa chini ya serikali ya awamu ya tano. Alisema kuwa,mfumo wa usajili wa bidhaa umeendelea kuimarika mwaka hadi mwaka ambapo idadi ya bidhaa za chakula,dawa, vipodozi,vifaa tiba na vitendanishi imekua ikiongezeka mwaka hadi mwaka,katika kipindi cha 2015/2016 hadi17/18. ''TFDA imesajili jumla ya bidhaa 14,345 kutoka bidhaa 8,866 zilizokuwa zimesajiliwa mwaka 2015/16 ambapo ni saw

Simba sasa kukutana na wababe wengine

Klabu ya soka ya Simba imefanikiwa kutinga hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika kwa mara ya kwanza baada ya miaka 15 baada ya kuichapa Nkana FC ya Zambia. Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam, ulimalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 na kufuzu kwa uwiano wa mabao 4-3. Simba ndiyo timu pekee ya Afrika Mashariki iliyofanikiwa kutinga hatua hiyo, ambapo sasa inaungana na wababe wengine 15, ikivunja rekodi yake iliyoiweka mara ya mwisho mwaka 2003. Timu zilizofuzu hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika ni: Simba Sc (Tanzania), Asec Memosas (Ivory Coast), Al Ahly (Misri),  AS Vita (Congo DRC), JS Saoura (Algeria), Club Africain (Tunisia), Al Nasri (Libya), Mamelodi Sundowns (Afrika Kusini), FC Platinum (Zimbabwe), CS Constatine (Algeria), TP Mazembe (Congo DRC), Orlando pirates (Afrika Kusini), Lobi Stars FC (Nigeria), Wydad AC (Morocco), Ismaily SC (Misri), Horoya SC (Guinea). Droo ya hatua hiyo ya makundi inatarajia ku

Wekundu wa Msimbazi sasa kukutana na wababe wengine

Klabu ya soka ya Simba imefanikiwa kutinga hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika kwa mara ya kwanza baada ya miaka 15 baada ya kuichapa Nkana FC ya Zambia. Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam, ulimalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 na kufuzu kwa uwiano wa mabao 4-3. Simba ndiyo timu pekee ya Afrika Mashariki iliyofanikiwa kutinga hatua hiyo, ambapo sasa inaungana na wababe wengine 15, ikivunja rekodi yake iliyoiweka mara ya mwisho mwaka 2003. Timu zilizofuzu hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika ni: Simba Sc (Tanzania), Asec Memosas (Ivory Coast), Al Ahly (Misri),  AS Vita (Congo DRC), JS Saoura (Algeria), Club Africain (Tunisia), Al Nasri (Libya), Mamelodi Sundowns (Afrika Kusini), FC Platinum (Zimbabwe), CS Constatine (Algeria), TP Mazembe (Congo DRC), Orlando pirates (Afrika Kusini), Lobi Stars FC (Nigeria), Wydad AC (Morocco), Ismaily SC (Misri), Horoya SC (Guinea). Droo ya hatua hiyo ya makundi inatarajia kufanyi

Rais Dkt. John Pombe Magufuli :Serikali yake imejitahidi kununua ndege za kisasa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa Serikali yake imejitahidi kununua ndege za kisasa, lakini sio jambo la kushangaa endapo viongozi wengine wajao wataziuza kwani hata kipindicha nyuma Baba wa Taifa alinunua na hapa katikati ndege zikapotea.

Gazeti la Mtanzania leo

Wazazi wametakiwa kuacha kuegemea kuchangia sherehe za harusi badala yake wajikite kutoa msaada wa kiuchumi kwa watoto

Jamii imeshauriwa kuacha utamaduni wa kuyakimbia majukumu ya malezi ya kiuchumi badala yake  ijikite katika kutoa eliumu ya ujasiriamali kwa watoto itakayosaidia kuwakomboa kiuchumi  pamoja na kuliingizia taifa kipato. Wazazi wametakiwa kuacha kuegemea kuchangia sherehe za harusi badala yake wajikite  kutoa msaada wa kiuchumi kwa watoto wao wanaoshiriki harusi hizo kuwakwamua kiuchumi. Hayo yamesemwa  jijini Dar es Salaam na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Joseph  Kakunda katika Maonesho ya Ujasiriamali kwa vijana yaliyoandaliwa na Taasisi ya Nama  inayojishughulisha na masuala ya utoaji elimu ya ujasiriamali kwa vijana na kuwawezesha  kupitia mikopo nafuu. Amesema kuwa kuna utamaduni umejenga katika jamii ambapo wazazi hutumia fedha nyingi  kwenye sherehe za harusi za watoto na kwamba baada ya harusi wanandoa huishi magumu  kutokana kutowezeshwa kiuchumi. " Jamii isikimbie malezi ya kiuchumi kwa watoto tuwape elimu ya ujasiriamali tusii

WAZIRI wa Afya Ummy Mwalimu :Jukumu la Baraza la Famasi ni kuleta msukumo wa utoaji huduma bora ya afya kwa

IMEELEZWA kuwa utaalamu wa kutengeneza, uagizaji, usafirishaji, usambazaji, utoaji dawa sahihi  kwa wagonjwa, utunzaji  na utoaji mafunzo yahusuyo dawa ndiyo msingi mkubwa wa taaluma ya Famasi. WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu jana jijini Dar es Salaam amezindua Baraza la Famasi na kuwataka kusimamia sheria ili kudhibiti uuzwaji wa dawa katika maduka ya dawa yasiyo na vibali. Waziri Ummy Mwalimu amesema kuwa,  jukumu la Baraza la Famasi ni kuleta msukumo wa utoaji huduma bora ya afya kwa mtanzania.  Hili linawezekana kwa kuhakikisha kuwa wanataaluma wanazingatia maadili na nidhamu ya taaluma katika ununuaji, utunzaji na matumizi sahihi ya dawa na vifaa tiba vilivyo salama na ubora wa hali ya juu.  Alisema anapenda kuisisitiza kuwa Baraza hilo lione umuhimu wa kuweka msukumo wa pekee kwenye masuala ya kuboresha mafunzo na elimu ili  tuwe na wanataaluma  wenye uwezo wa utendaji wa kiwango cha hali ya juu katika nchi yetu katika maeneo

Waziri Mwakyembe: Kupoteza mechi za kwanza isiwe sababu ya kukata tamaa mapema

Serikali kupitia Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo imetoa ushauri kwa klabu za Simba na Mtibwa kujipanga vema kuelekea mechi za marejeano za mashindano ya kimataifa. Kupitia Waziri mwenye dhamani, Harisson George Mwakyembe, amesema kupoteza katika mechi za kwanza ambazo walicheza ugenini isiwe sababu ya kukata tamaa mapema. Mwakyembe amewamua kuwapa nguvu Simba na Mtibwa ili waweze kujipanga vizuri kuelekea mechi za marejeano akiamini lolote linaweza kutokea ndani ya dakika 90. "Nawasihi vijana wetu wapambane na wajipange kuelekea mechi za marudiano, sikutegemea kama wangeweza kupoteza kulingana na namna walivyofanya vizuri katika mechi za kwanza" alisema. Katika mchezo ambao Simba walicheza dhidi ya Nkana Red Devils ya Zambia walipoteza kwa jumla ya mabao 2-1 kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika na Mtibwa akipoteza kwa mabao 3-0 kwenye Kombe la Shirikisho Afrika. Simba itarejeana na Nkana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar e

GERMANY SUPPORTS WFP’S HUMANITARIAN ASSISTANCE FOR REFUGEES IN TANZANIA

DAR ES SALAAM – The United Nations World Food Programme (WFP) today welcomed a €3.25 million contributionfrom the Federal Republic of Germany to support its work in favour of refugees and asylum seekers in Tanzania in 2018-19. “WFP greatly appreciates this generous contribution from the Government and people of Germany,” said Michael Dunford, WFP Tanzania Country Representative. “Germany is a key supporter of WFP’s programme providing life-saving food assistance for refugees in Tanzania.” WFP distributes monthly rations consisting of cereal, pulses, vegetable oil and salt as well as fortified supplementary foods for vulnerable pregnant and lactating women, children under five, malnourished persons with HIV/AIDS and hospital in-patients. In addition, high energy biscuits are provided to refugees in transit. Tanzania hosts some 290,000 refugees, most of them women and children, in Nduta, Nyarugusu and Mtendeli refugee camps in Kigoma region in northwest Tanzania.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezindua Chaneli ya Taifa ya Utalii iitwayo Tanzania Safari Channel

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amezinduaChaneli ya Taifa ya Utalii iitwayo Tanzania Safari Channel na amewataka watu wote waliopewa dhamana ya kuiendesha wahakikishe wanazingatia viwango vya kimataifa katika vipindi watakavyokuwa wanaviandaa. “Vipindi vyenu ni lazima vivutie kama vile tunavyoviangalia katika chaneli za wanyama za kimataifa kama vile National Geographic, Discovery, Travel na zingine ili lengo lililokusudiwa wakati wa kuanzishwa kwake litime.” Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Desemba 15) wakati akizindua chaneli hiyo kwenye Ofisi za TBC, Mikocheni, jijini Dar es Salaam, ambapo ametoa wito kwa Wizara zote zinazohusika na uanzishwaji wa Chaneli hiyo kuhakikisha zinailea wakati ikijijenga kujiendesha kibiashara. Amesema Tanzania ni moja ya nchi duniani zilizotenga moja ya tatu ya eneo lote la nchi kwa ajili ya uhifadhi, ambapo kuna tamaduni za makabila mbalimbali, ngoma za kuvutia, vyakula vya asili, sinema za maisha yetu na lugha adhimu ya Kiswahili. “Hivyo, kw

CHAMA CHA WAAJIRI TANZANIA (ATE) YAANDAA TUZO ZA MWAJIRI BORA WA MWAKA 2018

Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Disemba 14 2018 kimeandaa Tuzo za Mwajiri Bora wa Mwaka  2018  zilizofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City.  Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2005,tuzo hizo zimejikita katika kutambua waajiri wenye  misingi bora  ya usimamizi wanguvu kazi na rasilimali watu kwa lengo la kuwawezesha kutimiza  wajibu wao kikamilifu na kupelekea kukuza uzalishaji wa kibiashara.  Tuzo hizo zilihudhuriwa na wadau mbali mbali wakiwemo Mh. Jenista Mhagama, Mh.  Anthony Mavunde,  Mhe. Stella Ikupa, Mkuu wa MkoaDSM, Mhe. Paul Makonda, Balozi  wa Norway nchini, Bi. Elisabeth Jacobsen, Balozi wa Denmark nchini, Bw. Einer H.  Jensen na Balozi wa China nchini Nd. Wang Fe, pamoja na taasisi mbali mbali  ikiwemo TUKTA na ILO. Tuzo hizo zinazofanyika kila mwaka zimasaidia kuhamasisha wanachama kuchukulia masuala ya ajira na usimamizi wa rasilimali watu kama misingi muhimu katika kumwezesha mwajiri kuwa na wafanyakazi wenye uwezo na ueledi ili kukidhi