Skip to main content

Posts

Showing posts from November, 2015

‘King’ Kibadeni aula Kilimanjaro Stars

Abdallah Kibadeni akiwa na kocha wa Taifa Stars Charles Mkwasa (kulia) Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limemteua Abdallah Kibadeni kuwa kocha mkuu wa timu wa Taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Star’ akisaidiwa na Juma Mgunda kuelekea katika michuano ya CECAFA Chelenji itakayoanza kutimua vumbi Novemba 21 mjii Addis Ababa, Ethiopia. Kilimanjaro Stars inashiriki michuano hiyo mikongwe kabisa barani Afrika, ambapo jumla ya nchi 12 wanachama wamedhibitisha kushiriki michuano hiyo itakayomalizika Disemba 6 mwaka huu. Nchi zingine zinazoshiriki michuano hiyo ni tofati na Tanzania bara ni Burundi, Djibouti, Ethiopia, Eritrea, Kenya, Rwanda, Somalia, Sudani, Sudani Kusini, Uganda na Zanzibar. Kibadeni mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, na timu ya Taifa Tanzania, ni kocha mwenye leseni B, ambapo ameshafundisha vilabu vingi chini kwa mafanikio ikiwemo kuifiksha klabu ya S

Kufuatia Vuguvugu za kisiasa Afande Sele kuacha muziki kushika jembe

Aliyekuwa mgombea Ubunge wa jimbo la Morogoro mjini kwa tiketi ya chama cha ACT-Wazalendo, Suleman Msindi alimaarufu kama 'Afande Sele' amefunguka na kusema hawezi kufanya muziki tena, na badala yake atajikita katika shughuli za kilimo. Afande Sele amesema haya katika kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio na kudai sasa atafanya kilimo pamoja na ufugaji na maamuzi haya yamekuja kutokana na yeye kushindwa katika uchaguzi wa mwaka huu, na ameamua iwe hivyo kwa sababu tayari anaamini amepoteza mashabiki wake wengi ambao walikuwa Ukawa na CCM ambao walikuwa wanaamini katika maono na mashairi yake. “Kwa sasa nimeamua tu kufanya kilimo pamoja ufugaji sitafanya muziki tena sababu nilipoingia kwenye siasa mlango nilioingilia huu wa ACT-Wazalen

OZIL AWEKA REKODI MPYA EPL

Mpika mabao wa Arsenal Mesut Ozil ameweka rekodi mpya katika Ligi Kuu nchini England (EPL) baada ya kutoa pasi za magoli katika michezo sita mfululizo. Mjerumani huyo alitoa pasi ya goli kwa Kieran Gibbs katika mchezo wa jana dhidi ya Tottenham ulioisha kwa sare ya goli 1-1, mchezo uliopigwa kwe ye dimba la Emirates. Ozil ameisaidiz Arsenal kushinda michezo mitano na kutoka sare mchezo mmoja katika michezo sita ya mwisho aliyocheza na kupelekea Arsenal kushika nafasi ya pili nyuma ya Man City wakizidiwa kwa tofauti ya mabao. Ozil amekuwa mchezaji wa kwanza kutoa pasi 10 za magoli katika michezo 11 ya mwanzo ya Ligi Kuu nchini Enlgand.

Ben Pol na Mwana FA wakifanya video Africa Kusini Patoranking naye ndani

Rnb super staa Ben Pol ametimiza ahadiyake ya kwenda Africa Kusini kufanya video ya nyimbo mbili kama alivyo sema awali. Staa huyu pia amekutana na msanii wa dance hall kutoka Nigeria Patoranking na Ben Pol anasema “Alikutana na Patoranking juu kwa juu tu na hawakupata muda wa kuongea mengi ila walibadilishana mawasiliano ” Ben alikutana na Patoranking kwenye show yake ya My Woman mjini Johannesburg Africa Kusini. Ukiacha Ben Pol,Mwana Fa pia naye yupo Africa Kusini akifanya video ambayo hatujui ni wimbo gani na ni muongozaji gani.