Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2016

Dante awatiwa matumaini Yanga

MLINZI wa kati wa mabingwa wa Tanzania Yanga, Andrew Vicent 'Dante' amewatoa hofu wapenzi na wanachama wa timu hiyo baada ya kuumia katika dakika za mwanzo za mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Mo Bejaia hapo jana. Dante amesema leo  anaendelea vizuri baada ya kupata matibabu jana huku akiamini anaweza kuanza mazoezi jumatatu hii kujiandaa na mchezo dhidi ya Azam. "Nilipata maumivu makali nikaomba kutolewa, ila sasa sisikii maumivu kama jana, nitaanza mazoezi keshokutwa na Mungu akijalia nitakuwa tayari hata kwa mchezo wa Ngao ya Jamii na safari ya kuifuata Mazembe," alisema Dante. Beki huyo wa zamani wa Mtibwa  Sugar mwenye nguvu na anayetumia mbinu katika ukabaji amekuwa hapati nafasi mara kwa mara katika kikosi cha kwanza lakini mwenyewe anaamini ipo siku mwalimu atamwamini. "Niliumia sana roho kutoka jana, kiukweli nilipanga kuwaonyesha watu kile nilichonacho katika mechi kubwa kama ile. Lakini Mungu ndiye anajua, naamini siku

Wajua Umuhimu wa namba tisa

ZURICH, USWISI Anthony Martial (katikati) akifunga bao dhidi ya Liverpool, Clyne (kushoto) akisindika kwa macho KUNA washambuliaji wengi katika ulimwengu wa kandanda katika Ligi Kuu nchini Tanzania utakutana na namba tisa wengi kama John Bocco, Amis Tambwe, Donald Ngoma, Malimi Busungu na wengine wengi. Nje  ya Tanzania utawaona Michael Olunga (Kenya), Edin Dzeko (Bosni-Herzegovina), Luis Suarez (Uruguay), Clint Dempsey (Marekani), Mario Balotelli (Italia) na kadhalika. Mfano wetu utaanzia kwa nyota aliyekuwapo Liverpool ya England na sasa yupo katika klabu ya AC Milan huyo ni Mario Balotelli. Alipokuwa Liverpool wengi walikaririwa wakisema uwezo wa nyota huyo umekwisha hivyo kocha wake wakati huo Brendan Rodgers ikaonekana  alifanya usajili usio kuwa na macho akimwacha Luis Suarez atimkie Barcelona ya Hispania. Swali ni kweli Balotelli alikuwa akichezeshwa kama yeye alivyo au kocha Brendan alikuwa akimtengeneza kwa ajili ya nafasi  nyingine, jibu kale tuta

Kwa wachezaji ni bahati wachezaji kupata bahati ya kushiriki michuano ya olimpiki

BUENOS AIRES, ARGENTINA Roberto Ayala SIO wachezaji wote hupata bahati ya kushiriki michuano ya olimpiki katika maisha yao hususani katika mchezo wa kandanda. Hata hao waliobahatika huweza kutwaa medali mbili tu. Miongoni mwao ni Muargentina Roberto Fabian Ayala ambaye alifanikiwa kuitumikia timu ya taifa katika michuano iliyofanyika Atlanta, Canada mwaka 1996 na ile ya mwaka 2004 jijini Athens nchini Ugiriki. Alipewa jina la ‘El Ratón’ na mashabiki  yaani ‘The Mouse’ kifaa kimojawapo katika kompyuta. Nyota huyo anasimulia namna ambavyo ina maana kwa mchezaji wa kandanda wa kiwango cha Kimataifa anapoitumikia nchi yake katika michuano ya Olimpiki. Kwa miaka 15 Ayala alikuwa nyota na nembo ya La Albiceleste. “Unapokuwa mchezaji, ndoto zako na malengo ni kucheza Kombe la Dunia. Lakini michuano ya Olimpiki ni tofauti kabisa unapotaka kucheza cha kwanza kabisa ni pale unapostaajabishwa na wanamichezo wote kukaa katika kijiji kimoja.” Ayala ambaye amewahi kuhudumu R

TANZANIAN SPORTS PARK LEADING THE WAY THANKS TO SUNDERLAND AFC

Nearly a year on since its opening a state-of-the-art sports park in Tanzania is starting to show real promise as Sunderland AFC’s Head of International Football Development discovered. The JMK Youth Park, a multi-sport facility developed by Symbion Power and Sunderland AFC, officially opened to the Tanzanian public in October last year, and is now leading the way in developing young talent across Dar es Salaam. Graham Robinson from Sunderland AFC visited the park this week to sit down with the coaches at the park to discuss forward planning and to see first-hand the developments at the park. Graham said: “We held some great discussions and it was good to hear that player development was top of the sports park agenda and that all the coaches are keen to keep learning with many educating themselves with new trends from Europe.” As part of Graham’s visit he also delivered training sessions to the JMK Park’s U16 Centre of Excellence squad. The J

Msimu Mpya Wa Soka Unakujia Kupitia SuperSport

ZOTE 760 za misimu mipya ya Ligi Kuu Ya Soka Uingereza (Premier League) & Ligi Kuu Ya Soka Hispania (La Liga) zitapatikana kupitia DStv, SuperSport itawaletea watazamaji na wapenzi wa soka michezo kabambe ya soka kuliko ambavyo imewahi kuonekana kabla kutoka kwenye UEFA Super Cup, Ligi Ya Mabingwa ya UEFA, Kombe la FA, Kombe la Capital One, Super Cup ya Hispania, Fainali ya Copa Del Rey, German Cup na mingine mingi , Msimu unaanza Jumamosi tarehe 13 Agosti na kumalizika Mei 21, 2017. Lakini Sio Hayo tu, Fungua “Press Release” tumeambatanisha kwa Lugha ya Kiswahili na Kingereza kufahamu mengi zaidi mazuri, tafadhali tusaidie kupata “Coverage”. Shukrani sana. Imetolewa na Shumbana Walwa| Social Media Administrator