Skip to main content

Posts

Showing posts from January, 2019

SOKO la Ilala Boma Jijini Dar es Salaam laja na muoarobani wa wanaovamia soko hilo

SOKO la Ilala Boma Jijini Dar es Salaam linaendesha zoezi lakuwasajili wafanyabiashara wote sokoni hapo wanao miliki vizimba na meza nakuwarasimisha katika mfumo wa kanzi data, mfumo huo unatajwa kuwa muoarobani wa kuvamia soko hilo. Mwandishi wa gazeti hili jana alishuhudia wafanyabiashara wakijisajili katika ofisi ya Ofisa Mkuu wa soko, kukamilika kwa kanzi data hiyo kutasaidia soko hilo kutoa huduma stahiki na kwa weledi wa hali ya juu na kusaidia katika tathimini ya ujenzi wa soko jipya. Akizungumza katika soko hilo Ofisa Mkuu wa soko , Seleman Mfinanga alisema Uongozi wa soko pia umedhamiria kuboresha mazingira ya soko hilo kwa kugawa namba kwa ajili ya kuwatambua wafanyabiashara wa soko hilo. Mfinanga alisema Uongozi wa soko hilo chini ya   Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala ipo katika mpango wakuboresha masoko yake   yote likiwemo la Ilala Bora. Akijibu malalamiko hayo Mfinanga alikiri kuwepo kwa baadhi ya changamoto zilizoainishwa nakuzitolea ufafanuzi nanamna

menejimenti ya Benki ya Posta ya Kenya upo nchini kwa ziara ya siku tatu

UJUMBE wa maofisa wa benki 7 na menejimenti ya Benki ya Posta ya Kenya upo nchini kwa ziara ya siku tatu kwa ajili yakujifunza namna yakuendesha benki kibiashara. Benki ya Posta Tanzania (TPB) imekuwa kimbilio la mabenki ya serikali ya nchi za Afrika Mashariki na kusini mwa Afrika ambapo baadhi ya nchi hizo huja nchini kujifunza katika Benki hiyo. Benki ya Posta Tanzania imejipambanua kuwa imerasimishwa kuwa benki ya Biashara miaka 3 iliyopita ikijiendesha kwa hisa za aslimia 86 kutoka serikalini wanahisa wa benki 8%, serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na asilimia 2 kutoka kwa wanahisa wa posta na simu Sacos. Hayo yamezihirika jana ambapo licha ya ujumbe wa maofisa wa hao 7 awali benki nyingine iliyokuja kujifunza TPB ni Benki ya Posta ya Botswana iliyokuja mwaka jana. Mwenyeji wa ujumbe huo ni Menejimenti ya Benki ya TPB ikiongozwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo Sabasaba Moshinge,ujumbe huo upo kwa dhumuni la kujifunza mambo mbalimbali yakibenki. “Ujumbe wa Benki

Serikali imejipanga kuendelea kukabiliana na majanga yanayoikumba nchi

 kwa ushirikiana na wadau wengine imejipanga kuendelea kukabiliana na majanga yanayoikumba nchi  Serikali kwa ushirikiana na wadau wengine imejipanga kuendelea kukabiliana na majanga yanayoikumba nchi ili kuhakikisha inashughulikia na kutatua majanga hayo pindi yanapotokea. Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Bunge na Waziri Mkuu, Maimuna Tarishi Januari 28, 2019 wakati akifungua warsha ya kupunguza madhara ya maafa nchini na kuimarisha uthabiti kwa nchi na jamii dhidi ya majanga ya asili katika ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara. Tarishi alibainisha jitihada zinazofanywa na Serikali ili kukabili maafa ikiwa ni pamoja na kuendelea kuelimisha umma juu ya umuhimu wa kuimarisha ustahimilivu wa majanga ya asili kwa kuongeza idadi ya wilaya zenye mipango ya kupunguza madhara ya maafa, kuboresha mifumo ya tahadhari za awali, kuongeza utoaji wa elimu kwa umma na kuimarisha shughuli za kujiandaa, kukabili na kuimarisha mfumo wa uratibu wa masua

Simba kuondoka leo majira ya usiku kuwafuata Al Ahly ya Misri

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Bara, Simba wanatarajia kuondoka leo wakiwa wamebeba matumaini ya kupata matokeo mbele ya wapinzani wao Al Ahly ya Misri kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa hatua ya Makundi utakaochezwa Februari 2. Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema msafara wa klabu utakuwa na wachezaji 20 pamoja na baadhi ya Viongozi utaondoka leo jioni kwa kupitia Addis Ababa nchini Ethiopia kisha kuelekea Mjini Alexandria nchini Misri. "Tunawaheshimu wapinzani wetu na tunatambua kuwa mchezo utakuwa mgumu, wachezaji wanatambua nafasi hii ni kwa ajili ya kuturejeshea furaha wana Simba, nina amini kwenye mpira chochote kinaweza kutokea," alisema Manara. Kwenye kundi D Al Ahly wanaongoza wakiwa na pointi nne huku Simba wakiwa nafasi ya tatu baada ya kukusanya pointi tatu katika mchezo wao wa kwanza mbele ya JS Saura ya Algeria. 

TIC:kimezitaka taasisi za serikali na sekta binafsi kushirikiana kikamilifu

Pichani ni Mkurugenzi wa kituo cha uwekezajiji   (TIC)  Geofrey Mwambe, akizungumza na waandishi wahabari pamoja na maafisa wa kituo hicho leo jijini Dar es slaam. WATANZANIA wametakiwa waepukana na dhana ya kuwa wawekezaji ni kutoka nje ya nchi pekee bali nao wanapaswa kuwekeza kwa kutumia fursa zilizopo kwani mazingira ya uwekezaji ni mazuri. Kituo Cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimezitaka taasisi za Serikali na sekta binafsi kushirikiana kikamilifu katika kukuza sekta ya uwekezaji hapa nchini ili kusaidia kuondoa wimbi la ukosefu wa ajira kwa vijana. Akizungumza na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam Wakati akitoa taarifa  ya kituo hicho kutoka kuwa chini ya Usimamizi wa Wizara ya viwanda na kuwa Wizara  ndani ya Ofisi ya Waziri Mkuu Mkurugenzi Mtendaji Bw. Geofrey Mwambe amesema kuwa  kwa sasa kazi yao kuu itakuwa ni kuratibu maswala mbalimbali ya kuboresha uwekezaji  ndani na nje ya nchi. “Umma wa watanzania unatakiwa kutambua kuwa

serikali nchini inaendelea na jukumu la ujenzi wa nchi kwa kushirikiana na sekta binafsi

Mwandishi wetu-MAELEZO Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kutoa fursa kwa watu wengi kwa kuwezesha utekelezaji wa miradi mingi kwa mapana, katika Taasisi za serikali na Taasisi binafsi. Akizungumza katika mjadala wa Clouds Media katika kipindi cha The Big Breakfast chenye kauli mbiu ya The power of Man yaani Nguvu ya Pamoja kilichofanyika leo Jijini Dar es Salaam katika hoteli ya Serena, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt Hassan Abbasi alisema kuwa serikali inaendelea na jukumu la ujenzi wa nchi kwa kushirikiana na sekta binafsi. “Tunatambua na kuheshimu nguvu ya wengi kama kauli mbiu hii inavyoeleza, katika dhana ya maendeleo kuna mengi Serikali inafanya ili kutekeleza azma yake kwa wananchi, mfano Ujenzi wa madaraja mbalimbali nchini, Miradi ya Maji, Miradi ya Umeme, Ujenzi wa vituo vya afya na Hospitali na kulete ndege, kwetu sisi haya ni maendeleo makubwa sana”, Dkt. Abbasi. Katika dhana ya Nguvu ya

Mbappe, Hazard, Higuain, Coutinho, Rodriguez na wengine sokoni

Mchezaji  wa West Ham Andy Carroll, mwenye umri wa miaka 30, ameibuka na kuwashangaza wengi kwa kupigiwa upatu kuichukua nafasi ya mshambulizi wa Tottenham kutokana na kujeruhiwa kwa wachezaji wa timu hiyo.’ (Sun) Eden Hazard hatojiunga na Real Madrid mwezi huu lakini mchezaji huyo wa miaka 28 anataka kukataa maombi mengine yoyote na ahamie katika klabu hiyo bingwa wa Uhispania mwishoni mwa msimu. (Marca, kupitia Mirror) Chelsea inatarajiwa kukamilisha usajili kwa mkopo wa mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, mwenye umri wa miaka 31, huku naye mlinzi Emerson Palmieri, mwenye miaka 24, huenda akavuka upande wa pili kwa thamani ya £15m. (Star) Ganzalo Higuan anatarajiwa kuwasili London kesho Jumanne kukamilisha uhamisho wake kutoka Juventus kwenda Chelsea Higuain anatarajiwa kuwasili London kesho Jumanne kukamilisha uhamisho wake kutoka Juventus kwenda Chelsea.(Express) Kocha wa Milan Gennaro Gattuso, aliyetarajia kuwa na Higuain kwa mkopo msimu huu, anasema anakubal

DTB yashinda kwa pointi 90-73

Mfungaji Bora wa mashindano ya kikapu kwa taasisi za fedha (BBL 2018/19), Kaikai Leka wa NMB, akipokea kombe dogo kama zawadi ya ufungaji bora kutoka kwa Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa NMB, Juma Kimori, baada ya pambano la fainali ya michuano hiyo Januari 19 kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam. Mshambuliaji wa NMB, Kaikai Leka, akipaa hewani kuifungia timu ya kikapu ya NMB wakati wa fainali ya Michuano ya Mabeki (BBL 2018/19), dhidi ya DTB, iliyopigwa Januari 19 kwenye Uwanja wa Gymkhana, jijini Dar es Salaam. DTB ilishinda kwa pointi 90-73. Mshambuliaji wa NMB, Kaikai Leka, akipaa hewani kuifungia timu ya kikapu ya NMB wakati wa fainali ya Michuano ya Mabeki (BBL 2018/19), dhidi ya DTB, iliyopigwa leo Januari 19 kwenye Uwanja wa Gymkhana, jijini Dar es Salaam. DTB ilishinda kwa pointi 90-73. Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa NMB, Juma Kimori, akimkabidhi nahodha wa timu ya kikapu ya NMB, Danford Kisinda, kombe la ushindi wa pili wa Michuano ya Mabeki (BBL 2018/19), dhidi ya

Dk.Jim Yonazi :TEHAMA imesaidia kutatua matatizo mengi ya kijamii na kiuchumi.

WAKATI jamii mbali mbali duniani wakiendelea kutumia mfumo wa teknolojia (TEHAMA) imeelezwa kuwa maarifa zaidi yataendelea kuongezeka kutokana na kuutumia mfumo huo. WANAFUNZI WA CHUO CHA USIMAMIZI WA FEDHA (IFM) WAKIFATILIA UZINDUZI WA ASASI YA HIFADHI YA JAMII ULIODHAMINIWA NA PSPF. NI MOJA YA TUKIO LA ZAMANI. Yapo mafanikio na moja ya mifano ya mafanikio ya Tehama ni kubuniwa kwa mfumo wakufuatilia madereva wanaoendesha mwendo wa haraka ambapo mfumo huo umesaidia kupunguza ajali ikilinganishwa na kipindi cha nyuma. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasialiano) Dk.Jim Yonazi amesema Tehama imesaidia kutatua matatizo mengi ya kijamii na kiuchumi. Dk. Yonazi aliyasema hayo juzi wakati wa semina ya siku mbili juu ya umuhimu wa Tehama katika kujiletea maendeleo iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam. “Tehama ina mchango mkubwa sana katika maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla hivyo hatun