Skip to main content

SOKO la Ilala Boma Jijini Dar es Salaam laja na muoarobani wa wanaovamia soko hilo


SOKO la Ilala Boma Jijini Dar es Salaam linaendesha zoezi lakuwasajili wafanyabiashara wote sokoni hapo wanao miliki vizimba na meza nakuwarasimisha katika mfumo wa kanzi data, mfumo huo unatajwa kuwa muoarobani wa kuvamia soko hilo.
Mwandishi wa gazeti hili jana alishuhudia wafanyabiashara wakijisajili katika ofisi ya Ofisa Mkuu wa soko, kukamilika kwa kanzi data hiyo kutasaidia soko hilo kutoa huduma stahiki na kwa weledi wa hali ya juu na kusaidia katika tathimini ya ujenzi wa soko jipya.
Akizungumza katika soko hilo Ofisa Mkuu wa soko, Seleman Mfinanga alisema Uongozi wa soko pia umedhamiria kuboresha mazingira ya soko hilo kwa kugawa namba kwa ajili ya kuwatambua wafanyabiashara wa soko hilo.
Mfinanga alisema Uongozi wa soko hilo chini ya  Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala ipo katika mpango wakuboresha masoko yake  yote likiwemo la Ilala Bora.
Akijibu malalamiko hayo Mfinanga alikiri kuwepo kwa baadhi ya changamoto zilizoainishwa nakuzitolea ufafanuzi nanamna zitakavyotatuliwa hivi karibuni.
“Kwa uchakavu wa miundombinu ninakubaliana nalo, “nikweli mitaro ina kina kidogo , wakati wamvua huibua tafrani na mafuriko lakini wakati huu wa kiangazi mitaro hiyo huwa safi,”
Mfinanga alisema Kampuni iliyopewa zabuni yakukusanya taka na ushuru wa soko hilo inajitahidi kadri iwezavyo tofauti na kampuni iliyopita,kuhusu ushuru sheria inayoongoza soko hilo inaeleza bayana pasipo ujazo kuwa taka zitalipiwa ushuru wa sh500iwe gunia, kisafleti au tenga vyote ni sh500 tu.
Mfinanga aliongeza kuwa changamoto kubwa ya soko hilo nikukokosekana kwa ukuta kiasi kwamba wanashindwa kujua idadi kamili ya wafanyabiashara sokoni hapo kwakuwa huingia kiholela lakini ukuta utakapojengwa tatizo hilo litakwisha.

“Gari la usafi hukusanya taka kila siku saa nne asubuhi, kuna wafanyabiashara wa aina mbili kuna ambao wana meza na kuna ambao hupanga bidhaa chini, gari ya taka hifika saa 10.00 asubuhi kwa ajili ya kukusanya taka na wafanyabiashara walioweka bidhaa chini wanalipisha likiondoka wanarudi tena lazima kuwe na uchafu ukipita majira ya alasiri na jioni,”alisema
Malalamiko mengine yaliyo ainishwa na wafanyabiashara sokoni hapo kwa shariti la kutoandikwa majina yao ni pamoja na soko hilo kukosa uongozi wa mwenyekiti , katibu na mweka hazina wao kama ilivyo kwa masoko mengine.
Akijibu malalamiko hayo Mfinananga alisema rasimu imekwishaandaliwa na viongozi wa umoja wa wafanyabiashara wa vitengo mbalimbali sokoni hapo walishiriki katika rasimu hiyo ambayo hivi karibuni itakuwa moja ya sheria katika sheria ndogondogo za halmashauri.
“Tumewashirikisha viongozi wa vitengo na wenyewe wamependekeza kikomo cha uongozi wa uwenyekiti wa soko nikipindi cha miaka 3 na uwezekano wakuchaguliwa kuongoza kipindi kingine, rasimu hiyo imefuata michakato na miongozo yote ya sheria inayoongoza halmashaururi ya manispaa ya Ilala,”

Comments