Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2010

Kizazi Kipya Yatoa Sapoti ... Extra Bongo

NGULI katika muziki wa kufoka foka nchini Prof Jay naye alitoa sapoti kwa Extra Bongo. TONYA timu alikuwepo kutoa sapoti kwa bendi hiyo ya muziki wa dansi katika usiku huo.

Wengena Extra Bongo Watimua Vumbi New Msasani Club

KIONGOZI wa bendi ya muziki wa dansi katika bendi ya Extra Bongo akiwa amebebwa juu wakati akiingia katika jukwaa la bendi hiyo kwenye ukumbi huo , mambo yalikuwa makubwa , wakati bendi hiyo ilipofanya makamuzi kwa ajili ya kutamburisha rasmi bendi hiyo. HAPO ni katika hatua flani usiku huo ambapo Wenge Tonya Tonya wakitoa sapoti mwishoni mwa wiki iliyopita katika ukumbi wa New Msasani Club jijini Dar es Salaam. HAPA bendi hiyo ikifanya mambozzz, yaliyotalajiwa kuwa hivyo katika usiku huo.

Bw.Donald Kaberuka Achaguliwa Tena Rais wa Benki

Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika leo tarehe 27 mwezi mei hapa Abidjan imemchagua tena Bw.Donald Kaberuka kuwa Rais wa Benki hiyo kwa kipindi cha pili. Bw. Kaberuka alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuwa Rais wa Benki hiyo mwaka 2005. Kuchaguliwa kwake kwa kipindi cha pili kumetokana na mafanikio makubwa ambayo ameyaleta katika benki hiyo na kuleta maendeleo katika taasisi hiyo muhimu ya kifedha na kwa bara la Afrika. Hii ilibainika kutoka kwa Magavana waliotaka Rais huyo kuendelea na wadhifa wake. Katika kukubali kuthibitishwa kwake katika cheo hicho. Bw Kaberuka aliwashukuru Magavana hao kwa kuwa na imani na uongozi wake katika benki. “Nina farijika sana kuona kuwa ninyi Magavana mna imani kubwa na mimi hadi kunichagua tena ili niweze kuiongoza taasisi hii muhimu, kwa kweli nina shukuru sana”,alisema. " Ningependa kutoa shukrani zangu za pekee kwa uongozi na wafanyakazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika kwani wao ndio wamenifikisha hapa kwani mimi ni Rubani tu. Alisem

Rythm za Top Band Live Katika Kiwanja Kipya

Extra Bongo Kuwasha Moto leo New Msasani Club

EEE ... sana tu !! , ni Wengena Extra Bongo , hii ni kazi moja wapo hapo pichani ya ukali wa bendi hiyo wamejipanga wakionesha makamuzi siku chache zilizopita , leo kutakuwa na shoo kali New Msasani Club ambapo Wenge Tonya Tonya toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imetua kuwasapoti Extra Bongo katika utamburisho wake rasmi nchini hapa chini ya Mkurugenzi wa bendi hiyo Ali Choki.

Tukutane Kesho Ndani ya Groove Back :Dj Peter Moe Kuamsha

KWA mara ya kwanza mzaziiiiii .. eeee ni pale Zhonghua Gareden Barabara ya Ali Hassan Mwinyi jijini Dar kutafanyika kufuru , mtatuzi wa yote ni macho yako mzazii siunajua ubishoo wa mastaa wa Bongo katika kujiachia mwisho wa wiki , basi mng'ao wako utakuwa wa maana sana kesho kwani Goroove Back Divas Night na disco la kufamtu usikose kesho njoo uonane na wadau watakao amsha chini ya Djs Peter Moe na Kelvin Twisa.

Rais Karume Akiwa Ziarani China

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk Amani Abeid Karume,na Mkewe Mama Shadya Karume,wakipata maelezo walipotembelea Bustai ya Mji Mkongwe wa Shanghai,China YU Garden

Time For Change?

TIME FOR CHANGE? Dear Tanzanians, I, as Tanzanian, am proud to have achieved another milestone... The Tanzanian Shilling is now equal to more than 1,400 to 1 US$!!!! Congratulations to all of us Tanzanians for: 1) Using Chinese toilet paper rather than Rexa or Tanpack... 2) Buying ice cream made in Kenya or South Africa rather than Azam 3) Using Omo rather than Foma 4) Eating Heinz baked beans rather than Dabaga or Red gold 5) Using Shoprite as your favourite shopping destination since "expired" South African goods are better than FRESH Tanzanian products 6) Using Anchor butter/cheese on your bread rather than ASAS or AZAM 7) Using Colgate and CloseUp as they make your teeth brighter rather than Whitedent 8) For drinking Heineken and Red Bull rather than a good old Kili....its a matter of image in it! 9) For drinking St.Anne, Namaqua and Overmeer than Dodoma wine 10) For using Farmer's choice sausages than Beef Vienna from Arusha 11) For using Kangaroo matches than KIBO m

TFF Yatangaza Kuwasili Kwa Tiketi za Kombe la Dunia Nchini

Afisa habari wa Shirikisho la Mpira wa miguu nchini TFF Frolian Kaijage ameongea na vyombo vya habari leo na kusema kwamba tiketi za kombe la dunia kwa watanzania walionunua zimeshawasili ambapo shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA limetuma tiketi 380 ambazo zilinunuliwa na watanzania. Akionyesha tiketi hizo kwa waandishi wa habari , Kaijage a limesema kwa wale walionunua tiketi hizo wanatakiwa kwenda kuchukua wakiwa na risiti ili waweze kupatiwa tiketi hizo na baada ya kupatiwa tiketi hizo ili kupata viza katika ubalozi wa Afrika Kusini wanatakiwa kwenda na Tiketi ya ndege, tiketi ya kuingilia mpirani, Paspoti ya kusafiria pamoja na picha moja itakayotumika kwa utambulisho wa mhusika kwa usalama zaidi na taarifa mbalimbali wakati yuko katika fainali hizo endapo kutatokea lolote akiwa nchini Afrika Kusini Wakati huohuo Rais wa Shirikisho hilo la TFF Reodger Tenga amesema bado wako kwenye mazungumzo na timu ya taifa ya Brazil ili iweze kuja hapa nchini kwa mchezo mmoja wa kira

Meli ya Mafuta ya Ufaransa Yafanyiwa Uharamia

Matukio ya uharamia ya utekeji nyara wa meli bahari ya Hindi karibu na Tanzania, unaofanywa na maharamia wa Kisomali, yanazidi kupamba moto, baada ya ile meli ya Uingereza kuwatimua wiki iliyopita, na meli nyingine kuvamiwa majuzi, leo meli ya Mafuta ya Ufaransa imevamiwa. Balozi wa Ufaransa atazungumza na Waandishi wa habari kesho Saa 6:30 mchana hapa Umoja House huku akisindikizwa na mabalozi wa Uingereza, Ujerumani, Uholanzi na Jumuiya ya Ulaya.

muandishi: JOHN BUKUKU tarehe: 5/25/2010 0 maoni Rais Kikwete alihutubia Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki

Rais Mwai Kibaki wa Kenya akimkaribisha Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Jakaya Kikwete katika ikulu ya Nairobi ambapo viongozi hao wawili walifanya mazungumzo mafupi kabla ya Rais Kikwete kulihutubia bunge la Jumuiya ya Afrika Masharik.

Extra Bongo Kuja na Maufundi Mapyaaaaa.

HUU ni mwonekano wa bendi ya muziki wa dansi Extra Bongo wakiwa wamejiachia kwa sasa bendi hii inajipanga kufanya mambo makubwa yatakayokuwa yakichengua mashabiki wake.

Azam yafanya Kufuru Yafanya Bonge la Usajiri : Yaanika Hadharani Nyota Wake Wapya

AZAM FC yamnyakua mlindamlango wa JKT Ruvu na timu ya Taifa Jackson Chove,(Pichani ) Mwenyekiti wa Azam FC Said Mohamed Said akimkabidhi UZZZZZ wa timu hiyo , tayari kukipiga rasimi. SASANGAZA kukipiga rasimi Azamu FC , Mwenyekiti wa Azam FC Said Mohamed Said, jana alimkabidhi Mrisho Ngasa Jezi namba 16 yenye jina la timu hiyo na kuondoa hali ya utata juu ya mchezaji huyo kwa mashabiki waliokuwa wanahamu ya kufahamu mchezaji huyo atakipiga kweli chama la Azamu ama ..... , Mwenyekiti Said alisema Ngasa ametua Azam kwa kitita cha Sh milioni 58 makubwa haya DUUU Kweli Azam tishio nchini na wengine wajaribu. MWENYEKITI wa Azam Said Mohamed FC akiongea na waandishi wa habari.

Aishwarya Wakabidhiwa Kitita cha 1.8 na Vodacom ni Baada ya Mbuzi wao Kushinda

George Rwehumbiza(kulia) ambaye ni Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania akimkabidhi Aishwarya Nair wa Traince Asyla Attorneys charities(kushoto) hundi yenye thamani ya Tsh 1,800,000,baada ya mbuzi wao kuibuka kidedea na wapili toka kulia Mtaalamu wa Mambo ya Habari wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu, John William, Afisa udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude. .Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania George Rwehumbiza(kulia)akimkabidhi Aishwarya Nair wa Traince Asyla Attorneys charities(kushoto) hundi yenye thamani ya Tsh 1,800,000,baada ya mbuzi wao kuibuka kidedea na wapili toka kulia Mtaalamu wa Mambo ya Habari wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu, John William, Afisa udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude. Ultimate Security katika kushiriki kwenye mbio za mbuzi zilizofanyika barabara ya Kenyata oysterbay jijini Dares Salaam , Vijana wakiwa na mbuzi kwa lengo la kuchangisha fedha na kuwasaidia watoto yatima na wasiojiweza,Ultimate Security walitoa Hundi yenye thaman

The Decision of the Fair Competition Commission on Complaint No 2 of 2009 on Abuse of Dominance Involving SBL and TBL.

Parsuant to section 58(1), (3) and (6) of the fair competition Act, 2003, the Commission imposes the following oders. I, that the understandings and arrangements in any from between Tanzania Breweriers Limited and Serengeti Breweriers Limited on yhe use of Euro bottles and their carrying crates are void and hence nullified. II, That Both TBL and SBL to adhere to each one's marketing startegies there have to be no any kind of agreement between TBL and SBL as competitors on the shearing of the carculating Euro bottles and their carrying crates, or whatever agreements which may likely harm competition, Each company has to seek and implement possible mechanism to ensure that its crates and bottles are clearly identifiable to their intended customers. III, That each company to publish three times in the local dailies circulating nationally on working days, (both English and Swahili) TV and Radio media explaining how the dispute has been decided by the commission and inform the public ab

Jeshi Lamaliza Ukalabati Daraja la Munisagala

Mnadhimu Mkuu wa majeshi Jenerali Abdurahman Shimbo akiwa ameongozana na Katibu Mkuu wa wa Wizara ya Miundombinu Eng.Omar Chambo wakikagua darala la Munisagala . Pichani ni Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jenerali Abdurahman Shimbo akimpa maelezo katibu mkuu wa Wizara ya Miundombinu wakati wa kukabidhi reli ya kati baada ya ukarabati wa reli hiyo hapo jana kwa Wizara ya Miundombinu iliyoharibiwa na mvua mwishoni mwa mwaka jana (dec 2009) kati ya maeneo ya Gulwe hadi Kilosa mkoani Morogoro. Ukarabati huo wa 68 km umegharimu shilingi 15.6 bilioni (tz) , ambao Jeshi la wananchi limekamilisha agizo la RaisJakaya Kikwete kulitaka kukamilisha ukarabati huo kwa haraka ili wananchi kuondokana na kero ya usafiri pamoja na kuiletea taifa mapato ya uchumi.Kwa wakati huu itaanza kutumika kwa treni za mizigo hadi itakapotangazwa rsami kuanza safari za abiria. Picha zote na Mwanakombo Jumaa -MAELEZO

JK Meets EU Foreign Minister Baroness Cathy

President Jakaya Mrisho Kikwete in conversation with EU Foreign Minister Baroness Cathy Ashton at Dar es Salaam State House in Dar es Salaam today morning.

Tamko kwa Vyombo vya Habari Mei 2010

Siku ya Jumapili, tarehe 16 Mei, mnamo saa 2.30 usiku, mvulana mwenye umri wa miaka 15 alikimbia na kumpita mlinzi aliyekuwa mbele ya Ubalozi wa Marekani, akawasha moto kwenye chupa iliyokuwa na mafuta ya taa na kisha kuirusha chini ya moja ya malori mawili ya kubebea maji yaliyokuwa yameegeshwa nje ya ukuta wa Ubalozi. Chupa hiyo ilivunjika lakini haikuweza kulipua moto. Walinzi wa Kampuni ya KK wanaolinda ubalozini hapo walimkamata mara moja kijana huyo kabla hajaweza kurusha chupa ya pili. Hakukuwa na mtu yeyote aliyejeruhiwa wala mali yoyote iliyoharibiwa katika tukio hilo. Askari wa Jeshi la Polisi la Tanzania aliwasili sehemu ya tukio sekunde chache baadaye na kumkamata mtuhumiwa. Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi. Baadhi ya maelezo yanayotolewa kuhusu tukio hili si sahihi, yamekuzwa na kutiwa chumvi mno na yasiyo ya kweli, yakidai kuwa mvulana huyo aliingia ndani ya ubalozi. Hii si kweli. Hakukuwa na mtu yeyote aliyeweza kuingia ndani ya Ubalozi wa Marekani. Taratibu zetu

Watumishi wa Umma Wametakiwa Kufanya Kazi Kwa Bidii :Ilikuoingeza Ufanisi Kazini

Na Veronica Kazimoto – MAELEZO Dar es SalaamWafanyakazi katika ngazi ya utumishi wa umma wametakiwa kufanya kazi kwa juhudi na maarifa ili kuboresha huduma ya utendaji kazi na hatimaye kufikia malengo ya utoaji haki kwa wananchi wote na kwa wakati muafaka. Akisoma hotuba kwa niaba ya mwanasheria mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema wakati akifungua mkutano wa wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali uliofanyika Dar es Salaam leo, amewaambia wafanyakazi hao kuwa juhudi na maarifa katika kazi ndio silaha muhimu katika kutekeleza majukumu ya utendaji kazi. “Ili tuweze kupata mafanikio ni wazi kwamba kada zote za utumishi wa ndani ya ofisi hii zinapaswa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ili kuleta tija na ufanisi katika sehemu zetu za kazi,” Amesema Jaji Werema. Jaji Werema ameliambia baraza hilo kuwa lina wajibu wa kutambua na kujadili vipaumbele vya Ofisi hiyo ili kuhakikisha kwamba fedha zinatengwa kwa majukumu na madhumuni ya kuboresha huduma na kuo

Simba Yashindwa Kubishana na Sofapaka Yachapwa 1-0

SOFAPAKA yaitungua Simba 1-0 .

TGNP Yafanya Semina Leo Kama Kawaida

MADA kuhusu uchaguzi Ujao zawa na Mgawanyiko, wadau wajadili Kilimo Kwanza.

Jeshi la Polisi Tanzania la Ahidiwa Misaada Zaidi korea

IGP Said Mwema akihojiwa na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya jeshi hilo yaliyopo Wizara ya Mambo ya Ndani mara baada ya kusaini mkataba huo jana. Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi DAR ES SALAA , Serikali ya Korea Kaskazini, imeahidi kulisaidia Jashi la Polisi hapa nchini katika Nyanja mbalimbli zikiwemo za mafunzo ya upelelezi dhidi ya makosa ya kigaidi na yale yatokanayo na wizi kupitia mifumo ya mitandao ya kompyuta. Ahadi hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Balozi wa Korea hapa nchini Bw. Jae Young Kim, wakati wa hafla fupi ya kulitiliana saini makubaliano hayo iliyofanyika Makao makuu ya Jeshi la Polisi Jijini Dar es Salaam. Bw. Kim ambaye ni Afisa wa Ubalozi huo wa Korea kaskazini hapa nchini, amesema kuwa, kutokana na mabadiliko ya teknolojia na jitihada zinazoonyeshwa na Jeshi la Polisi nchini Tanzania katika kukabiliana na makosa mbalimbali Serikali ya Korea kupitia Kampuni ya Misaada kwa nchi za Kiafrika ya Koica, itasaidia kuwapatia elimu na ujuzi mbalimbali makacher

Klabu ya Yanga Imemtimua Amir Mafutah

YANGA kupitia Uongozi wake imemfukuza mchezaji AMIR MAFTAH na kuvitka vilabu vinavyotaka kumsajiri mcheza huyo kuwa huru kusajiri. Mwenyekiti wa YANGA IMAN MADEGA amesema mchezaji huyo amekuwa na utovu wa nidhamu mara nyingi lakini klabu imekuwa ikimvumilia. MADEGA amesema uamuzi wa kumfukuza mchezaji huyo umetokana na kupiga mchezaji wa SIMBA wakati wa mchezo wa ligi kuu TANZANIA BARA kati ya SIMBA na YANGA AMIR alipewa kadi nyekundu wakati wa mchezo na kuisababishia timu ushindi baada ya kubakiwa na wachezaji nane. KANAVARO NA NGASA WAPEWA ONYO KALI. MADEGA amesema anamshagaa mchezaji NGASA akidai anataka kwenda kuchezea klabu ya AZAM wakati mkataba wake unamalizika 2012 baada ya kusaini mkataba wa miaka minne tangu mwaka 2008 . Pia amesema mchezaji KANAVARO baada ya kumalizika kwa mkataba wa zamani mchezaji huyo alisaini mkataba mpya ambao unaisha 2012 ,hivyo wachezaji hao ni wachezaji halali wa YANGA. lakini MADEGA amesema iwapo timu yoyote ile inawataka wachezaji hao wanatakiwa

Hawa Wamechangia Chama Chetu Wewe Je?

Hivi Ndivyo Hali Ilivyokuwa Disembar 23 Mwaka Jana Diamond!!

Hii ni kazi ambayo iliandaliwa na kampuni ya Msama Promotion ya jijini Dar es Salaam miezi michache iliyopita na kufanikiwa kiasi hiki, hapa ni Diamond Jublee. Eee ebwana mtoto huyu naye alikuwepo na alibahatika kusalimiana kwa kushikana mkono na Spika wa Bunge la Tanzania Samwel Sitta.

Utalii Waipaisha Tanzania Kimataifa

Kaimu Mkurugenzi wa Masoko Bodi ya Utalii (TTB)Geofrey Meena akiongea na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa bodi hiyo uliofanyika leo wakati alipokuwa akielezea tuzo yao waliyoipata kwenye maonyesho ya Utalii ya Kimataifa ya INDABA Nchini Afrika Kusini hivi karibuni. Kaimu Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii nchini TTB Geofrey Meena kushoto na Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa bodi hiyo Mussa Kopwe katikati wakionyesha tuzo ya INDABA waliyoipata kwenye maonyesho ya Utalii yaliyofanyika nchini Afrika kusini hivi karibuni anayeshuhudia kulia ni Edward Mbwiga Meneja wa Fedha TTB. Bodi ya Utalii Tanzania TTB leo imeonyesha kwa waandishi wa habari TUZO waliyopata siku za hivi karibuni wakati wa maonyesho ya Utalii yaliofanyika mjini Durban, nchini Afrika Kusini kuanzia tarehe 8 hadi 11 Mei 2010. Maonyesho haya yanajulikana “INDABA, Travel Show” na yanafanyika kila mwaka nchini Afrika Kusini. Maonyesho ya INDABA ni kati ya maonesho makubwa matatu ya utalii duniani, maonyesho m

Dogo Rama Aipua Albamu

RAMADHAN Athuman kutoka African Stars ama Twanga Pepete AMEIPUA albamu yake nje ya kundi ameteta na blog hii kuwa inaitwa Kilomita 10, 000 ambapo mimi King Kif ndiye promota wa kupushi mzigo huu . Kwa mawasiliano unaweza kuingia dogo.rama@yahoo.com ama piga simu 0653 860618, twende kazi.

DJ Victor Anavyo Waeusha Mashabiki Club Masai

NI raha ya kufa mtu katika kuizimia mikito mashabiki wengi wanakubali kiwanja cha Club Masai mvuto wa kupagawa toka kwa madj wakali ndio gumzo ya Club , Dj Victor akiangusha urefu wa shuguli katika kuporomosha burudani inayoambatana na track bomba .... jama ana maujanja ya kutatisha ilembayaaaaaaa.

Ni Usiku Zhonghua Garden na Wadau

NI Usiku katika kiwanja cha Zhonghua Garden kutoka kushoto ni Mr Edger Masatu na Mie Machibya kulikua na mambo mengi yaliyofanya tuondoke mida mibovuuu , uku Dj Peter Moe akiwajibika katika Udj , mambo ua babu kubwa katika kiwanja cha Zhonghua kila Jumamosi usiku.

Wanafunzi Wafuatilia Vocha Zao Wakiwa Makundi Makundi

BAADHI ya wanafunzi waliomaliza kidado cha Sita wakiwakatika Bank ya CRDB mchana wakifuatilia Vocha zaozinazotolewa na Serikalibarabara ya Azikiwe .

Tix Katika Mikao ya Makamuzi

DJ TIX akiwa katika anga za udj Club Masai usiku wa Juzi.

Hii ni Twanga Wanakutwanga na Kupepeta

BENDI ya Twanga Pepeta ikiwa mzigoni Club Blicanas Dar es Salaam.

Ghorofa Ili Nikati ya Maghorofa Marefu Zaidi Bongo

MOJA ya maghorofa yenye urefu mkubwa yanayojengwa Bongo .

Wajua Vinyago Vya Uzwa Wapi Kwa Wingi Dar!!

NI moja ya mchora katika maduka ya kuuza vinyago katika eneo la mwege jijini Dar es Salaam. HAPA jamaa wanachonga vinyago eneo la mwenge vinyago , ni mchana leo saa nane na pembeni maduka ya vinyago yanaonekana yakiuza vinyago.

Cheki Mvuja Jasho Anavyoenyeka !!

NI muda wa asubuhi katika barabara moja Dar es Salaam mvuja jasho , akiwa amepakiza kabeachi katika mkokoteni na juu yake amepakiwa mwanadamu hii ni shughuli pevu .

Eeee Soma Hapa

Msanii Nguli Sean Kingston Atua Bongo

SEAN king ston akisongesha na wenzake katika lango la TBL leo. MASHINE za kisasa Zikiwa (Mzigoni ) katika kuzalisha vinywaji za TBL. Mwanamuziki maarufu Sean Kingston akisaini , katika chupa ya bia ya Kilimanjaro TBL leo

Wadau Waliofika Jana TGNP !!

ILI ni bango linalo elekeza ulipo mtandao wa Jinsia Barabara ya Mabibo Dar es Salaa. WANANCHI wakiwa katika Semina inayotolewa kila siku za Jumatano Jioni Mabibo ulipo mtandao huo, waliosimama ni wachangiaji wa mada jana .

Ooo yaaaa Niko na Mdau wa Hip Hop Kutoka Kino

NKO na mwana harakati Kalapina toka Kikosi cha ....... Block 41.

Ajali Mbaya yatokea Fire Dar

NAMBA ya Daladala iliyokuwa ikitoka Ubungo kwenda Karia Koo . NAMBA za gari dogo zilisomeka kama huonavyo juu. DALADALA ilivyo gongana na gari dogo eneo la Fire Dar es Salaam na tukio ili liliweza kuzua foleni za magari mengine . NI bara bara ya Morogoro Road Daladala itokayo Ubungo iligongana na gari dogo eneo la Fire katika kona ya kuelekea barabara ya Msimbazi muda wa mchana .