Skip to main content

Msome Wambura Kupata Picha ya Simba Kunani!!


Na John Bukuku .

Michael Richard Wambura, aliyekuwa mgombea uenyekiti wa klabu ya Simba akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Malelezo juu ya kufungua kesi katika mahakama mbili Mahakama kuu na mahakama ya Kisutu kuhusu kukatwa jina lake kuwa mgombea wa nafasi hio.

Amesema Katiba ya Simba imekiukwa kwani Simba ilitakiwa kuunda kamati ya Rufaa ambayo ndiyo ingekuwa na mamlaka ya kushughulikia matatizo ya Simba juu ya uchaguzi.

Amesema kamati hiyo pamoja na kamati ya Uchaguzi iliyopo sasa zilitakiwa kupewa baraka ama kuthibitishwa na kamati ya utendaji ya Simba kitu ambacho hakijafanyika hivyo hata kamati ya uchaguzi ya Simba ya sasa ni Batili kwa mujibu wa katiba ya Simba.

Wambura amesema wamefungua kesi mbili katika Mahakama Kuu na Mahakama ya Kisutu ili kutafuta haki.

Anasema kwa kutolea mfano wa hukumu moja iliyowahi kutolewa na Jaji Bubeshi wa mahakama kuu ya mwaka 1996 iliyokuwa ikimkabili Muhidin Ndolanga na Baraza la Michezo.

Akinukuu moja ya kifungu katika hukumu hiyo Wambura anasema "kifungu hicho kilieleza kwamba kama unanyang'anywa haki usingoje muda upite itafute hata mahakamani kwa kipengele hicho, anasema mahakama imemruhusu kutafuta haki yake huko, lakini pia anasema kwa kuwa katiba ya Simba inatambua Katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania hivyo imeruhusu mwanachama yeyote kwenda mahakamani kudai haki yake".

Ameongeza kwamba ameliarifu Shirikisho la Soka Afrika CAF na Shirikisho la Soka la Dunia FIFA kuwa kuna mgogoro katika klabu ya Simba na TFF hivyo amekwenda mahakamani kudai haki yake. Pia, amewalaumu TFF kwa kuingilia kanuni za tararibu za katiba ya klabu hiyo na kwamba shirikisho hilo halikupaswa kuwa na kipengele cha pingamizi kukatwa kwenye Kamati ya Uchaguzi.

Alisema walipokiangalia kipengele hicho walipaswa kuwarudishia Simba ili wakirekebishe, lakini wao waliamua kuwafunga mdomo watu kwa kutokiondoa kipengele hicho.

Wakati huo huo, hakimu wa mahakama ya Ilala, Janeth Kinyage, ameitaka kamati ya utendaji ya klabu hiyo kukutana na kutafuta wakili baada ya mawakili watatu waliowekwa na watu tofauti kudai kila mmoja kuwa yeye ndiye mwenye mamlaka ya kuitetea kamati hiyo dhidi mwanachama Juma Mtemi kutaka uchaguzi usifanyike.

Hakimu huyo alichukua hatua hiyo baada ya kamati ya utendaji ya Simba kuendelea kujichanganya kuhusu wakili ambaye anaitetea kamati hiyo ikitaka uchaguzi uendelee.

Alisema awali alipokea barua ya mawakili kutoka kampuni mbili kwa makundi mawili ambayo ni ya uongozi ambaye alipewa barua na katibu mkuu wa Simba, Mwina Kaduguda, ambaye ni wakili Majura Magafu na mwingine kutoka kwa wajumbe wa kamati ya utendaji wakiwakilishwa na wakili Peter Swai.

Alisema kuwa tangu aanze kazi ya kusikiliza kesi mbalimbali hajawahi kukutana na kesi kama hiyo ambayo ina mawakili watatu na kila mmoja hataki kushirikiana na mwenzake na kila mmoja kudai kuwa yeye ndiye mwenye mamlaka ya kusikiliza na kuitetea kamati hiyo ya utendaji.

Hivyo, Kinyage aliitaka kamati hiyo ikutane na kukubaliana ni wakili yupi asimame na kuitetea kamati hiyo na wawasilishe kwanza mwakilishi huyo .

Alieleza kuwa bila kufanyika hilo atamsimamisha kizimbani mwenyekiti wa Simba (Hassan Dalali) mwenyewe bila mwakilishi kwa kuwa haki yao ya msingi ya kutetewa watakuwa wameipoteza,

Jambo lingine ambalo lilizuka mahakamani ni baada ya wakili wa Juma Mtemi ambaye amefungua kesi hiyo, Mh. Jerome Msemwa, kuikana barua iliyowakilishwa mahakamani hapo ya kufuta kesi.

Alisema kuwa barua hiyo haijaandikwa na mteja wake, hivyo kuitaka mahakama ichukue hatua kwa wale wote waliohusika na kughushi barua hiyo ikiwemo saini ya mteja wake

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...