Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2017

Mali watwaa ndoo mabingwa wapya fainali za U 17 Gabon

Timu ya taifa ya vijana ya Mali iliyo chini ya umri wa miaka 17 imetwaa Ubingwa wa michuano ya AFCON hapo jana baada ya kuifunga timu ya Ghana kwa jumla ya magoli 2- 1 nchini Gabon Mali, imeibuka na ushindi huo mwembamba katika mchezo ulio kuwa na upinzani mkubwa kwa pande zote mbili kuhitaji kuchomoza na ushindi , na hatimae timu hiyo ilipata goli la pekee kupitia kwa mchezaji wake Momadou Samake , lililo dumu hadika dakika 90 za mchezo. Baada ya kuingia katika fainali hizo kwa mara ya kwanza baada ya miaka 12, kocha wa Ghana Paa Kwesi Fabin alipanga kikosi chake cha kwanza ambacho kiliifunga Niger 6-5 katika hatua ya penati  kwenye hatua ya nusu fainali. Ghana walianza kwa kasi kipindi cha kwanza baada ya Eric Ayiah kupata nafasi ya wazi lakini hakuweza kufunga Kocha wa Ghana Ghana Paa Kwesi Fabin amesema pamoja na kupoteza mchezo huo, wachezaji wake walifanya jitihada za kutosha ila bahati haikuwa upande wake.

Azam FC walivyo mwacha Bocco

Timu ya soka ya Azam FC imeachana na mshambuliaji wake tegemeo wa muda mrefu John Raphael Bocco baada ya mkataba wake kumalizika, lakini ukweli ni kuwa tumezoea kuona wachezaji waliodumu kwa muda mrefu wakiagwa kwa heshima kitu ambacho hakijafanywa na Azam FC. Mchambuzi wa michezo Shaffih Dauda ameguswa kwa namna ambavyo John Bocco ameondoka Azam FC na ametoa ushauri baada ya uongozi wa klabu hiyo kuthibitisha hawatakuwa na Bocco kuanzia msimu ujao na kuanzia sasa JB nimchezaji uru. Unaweza kuangalia video hapa chini kwa story zaidi kuhusu kilakitu ambacho amekiongea Shaffih Dauda kuhusu issue ya John Bocco na Azam FC.

Msome hapa Bale napicha ya kutishaaa kwa Juventus

Bado siku chache tu twende Cardiff ambapo pale litapigwa pambano la kumtafuta mfalme wa michuano ya Champions League msimu huu kati ya Real Madrid dhidi ya klabu ya Juventus. Juventus wenyewe wanaelekea katika dimba la Millenium Stadium wakiwa kikosi chao kiko fiti 100% lakini Real Madrid wenyewe hawako fiti 100% kutokana na majeruhi muhimu. Walinzi wao wa kati Pepe na Varane waliumia na hawana uhakika wa kuwa fiti kabisa kuikabili Juventus lakini huku mshambuliaji wao Gareth Bale naye akiwa haijulikani kwamba atacheza au vipi. Kutocheza kwa Gareth Bale kunaweza kuwa jambo jema kwa Juventus kwani amekuwa mwiba mkali kwa kila timu ambayo inacheza dhidi ya Real Madrid. Lakini Bale ametuma picha mtandaoni ambayo inaweza kuwanyima raha mashabiki wasiopenda Real Madrid na kuwakatisha tamaa kuhusu hatma ya yeye kucheza au kutocheza Jumamosi. Bale ametuma picha akionekana yuko mazoezini akipasha na wenzake hali inayoashiria kwamba pengine Bale yuko ta

Wadu waelezea nguvukazi ya Fransesco Totti

Huu ndio mwaka ambao kwa mara ya kwanza Totti alivaa jezi ya As Roma na kuanza kucheza soka, alikuwa kijana mdogo wa umri wa miaka 16 tu na mchezo wake wa kwanza wa ligi kuu ya Italia ulikuwa dhidi ya Brescia ambapo Roma walishinda kwa mabao 2 kwa 0. 1998.Alikuwa na umri wa miaka 21 tu na akaweka rekodi ya kijana mdogo wa kwanza kupewa cheo cha unahodha wa timu ya As Roma kwa mara ya kwanza kabisa. 2001.Huu ndio mwaka ambao Totti alibeba ubingwa wa ligi kuu Italia Serie A na huu ulikuwa ubingwa wake wa kwanza na wa mwisho wa ligi hiyo nchini Italia,akifunga goli katika ushindi wa mwisho wa 3 kwa 1 dhidi ya Parma. 2004.Alivunja rekodi ya Roberto Pruzzo ya ufungaji wa muda wote katika klabu ya As Roma baada ya kufikisha jumla ya mabao 169 na kuwa mfungaji bora wa muda wote katika klabu hiyo. 2006.Alicheza michezo yote 7 ya timu ya taifa katika kombe la dunia huku akifunga bao moja na kutoa assists zaidi ya tatu katika michuano hiyo mikubwa dunia

Mecky Maxime aanza kuzungumziwa Yanga

YANGA inatarajia kufanya maamuzi magumu ya kumchukua kocha Mecky Maxime lakini mwenyewe ametangaza utamu kwamba akitua klabu hiyo itavuna vipaji vingi kutoka katika jicho lake. Akiongea na saluti5, mmoja wa vigogo wa Kamati ya usajili amesema katika kikao cha awali na kocha huyo kijana mwenye mafanikio, amewaambia kwamba endapo watakamilisha haraka mchakato wa kumchukua, Yanga itanufaika na kazi yake ya kuvumbua vipaji.  Bosi huyo amesema Maxime amewahakikishia kwamba anajua wapi vinapatikana vipaji bora ambapo Yanga itakuwa bora zaidi kwa kuwapatia wachezaji wapya wenye uwezo zaidi ya Shiza Kichuya, Muzamir Yassin na Mohammed Ibrahim “MO” wanaotamba Simba wakitoka katika uvumbuzi wake. Aidha bosi huyo amesema ujio wa Maxime ndani ya Yanga utaambatana na usajili wa mshambuliaji wa Kagera Sugar, Mbaraka Yusuph ambaye nae anatakiwa na kocha George Lwandamina. “Tunamtaka kweli Maxime, unajua sisi tunataka kufanya maboresho makubwa katika benchi letu na jicho letu

NZEGA MKOANI TABORA

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi, Alhaj Abdallah Bulembo, ameendelea na ziara yake ya Kichana katika mikoa mitano ambapo leo ziara hiyo imemfikisha katika Wilaya za Igunga na Nzega mkoani Tabora, ambako amefazungumza katika vikao vya ndani na Wajumbe wa Halmashauri Kuu za CCM za wilaya hizo, Mabalozi na watendani wa CCM na Serikali.

WAZALISHAJI WATAKIWA KUHAKIKI UBORA WA BIDHAA ZAO KUPITIA MAABARA ZA TBS

Frank Mvungi MAELEZO DAR ES SALAAM SERIKALI imewataka wazalishaji na wajasiriamali nchini kuhakikisha kuwa bidhaa wanazozalisha zinakidhi viwango vya ubora vilivyowekwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ili kuchochea ukuaji wa uchumi. Kauli hiyo imetolewa Leo Jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Kitengo cha Maabara ya Uhandisi wa Ujenzi ya Shirika la Viwango Nchini, Mhandisi Stephen Minja wakati wa ziara ya waandishi wa habari kutembelea na kujionea namna maabara za shirika hilo zinavyotekeleza jukumu lake la kuhakiki viwango vya ubora hapa nchini. Akifafanua zaidi Minja amesema kuwa mabara za shirika hilo zipo kwa ajili ya kuhudumia wazalishaji wa bidhaa mbalimbali na wale wanaoingiza bidhaa kutoka nje ya nchi lengo ili kuhakiki ubora wa bidhaa zote ili kuepusha athari zinazoweza kujitokeza kwa watumiaji. “Maabara yetu ina viwango vya kimataifa na gharama zake ni nafuu ambazo kila mwananchi anaweza kumudu lengo likiwa ni kutoa huduma kwa wananchi na kuchangia kuchochea

Kante atwaa tuzo nyingine kubwa

Ngolo Kante ni jina linalozidi kukua siku hadi siku huku akizidi kujizolea tuzo kutokana na kiwango bora anachokionesha tangu ajiunge na klabu ya Chelsea. Kante ambaye ameisaidia Chelsea kutwaa ubingwa msimu huu na hilo likiwa kombe lake mara mbili mfululizo na timu tofauti, usiku wa jana alijinyakulia tuzo mpya. Kante amefanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa waandishi wa habari za soka, tuzo ambayo huandaliwa kila mwaka na waandishi wa masuala ya soka nchini humo. Tuzo hizo ambazo zilitolewa katika hotel ya Landmark nchini Uingereza zilishuhudia Mfaransa huyo akiweka kabatini tuzo yake kubwa ya pili ndani ya mwezi mmoja. Kante ambaye msimu uliopita pia alifanikiwa kubeba kombe la Epl akiwa na Leicester City ameweka wazi ugumu ambao wanaweza kukabiliana nao katika msimu ujao wa ligi. “Msimu ujao tutakuwa na changamoto mpya kwani ukiwa bingwa na huku uko katika michuano mingi ni wazi kwamba unaweza kuwa na wakati mgumu uwanjani” al

Soma hapa VPL 2016/17 walioshuka daraja

Ligi kuu Tanzania bara imehitimishwa leo Mei 20, 2017 kwa mechi zote nane za mwisho kuchezwa katika viwanja tofauti. Timu tatu za ligi kuu Tanzania bara zimeshuka daraja ambapo msimu ujao zitacheza ligi daraja la kwanza. JKT Ruvu ilikuwa timu ya kwanza kushuka daraja baada ya kuchapwa na Toto Africans, JKT Ruvu ikafungwa tena mechi zake mbili za mwisho la kutupwa ligi daraja la kwanza. Mechi yao ya mwisho walikua ugenini kucheza dhidi ya Ndanda FC ambayo pia ilikua inahitaji pointi tatu ili kukwepa mkasi wa kushuka daraja. Ruvu ikapoteza mechi hiyo kwa kufungwa mabao 2-0. Toto Africa yenyewe pia ilihitaji ushindi katika mechi ya leo kuangalia kama inaweza kunusurika na kusalia kwenye ligi kuu Tanzania bara. Wakati Toto wakipambana kupata ushindi wakajikuta wakichezea kichapo cha magoji 3-1 na kushuka daraja hadi ligi daraja la kwanza. African Lyon nayo imeshuka daraja baada ya kubanwa ugenini na kutoka suluhu na Tanzania Prisons kwenye uwanja w