Skip to main content

Posts

Showing posts from January, 2012

Jahffaray Kusitisha Utoaji wa Albamu

MSANII  kutoka katika kundi la Wateule Jafari Mshamu aka Jahffaray amesma kuwa kwa sasa amesitisha kutoa albamu ambapo atakuwa akitoa wimbo tu . Akizungumza usiku sikuchache zilizopita kwenye ukumbi wa Nyumbani Lounge Dar es Salaam Jafari alisema kuwa , kutoa wimbo na kusambaza msanii anapata faida mapema kupitia maonesho katika  mialiko. "Kwa sasa nimesitisha kuipua albamu kwani, maandalizi yaeke yanatumia muda mrefu , uku utoaji wa wimbo ni wa muda mfupi na unaingiza kwa haraka kipato cha msanii,"alisema. Tayari msanii huyo anatarajia kuachia nyimbo mbili zinazoitwa ‘Tembea na mimi’ na ‘Amsha Amsha', ambapo amesisitza kuacha kabisa kwa yeye kutoa albamu.

CUF WAZINDUA KAMPENI UZINI ZANZIBAR (JANA)

  Maafisa wa jeshi la polisi wakijiandaa kutoa ulinzi kwenye mkutano  Magari ya viongozi wa CUF   Muda mfupi kabla ya mkutano   Akina mama wakitumbuiza na kucheza mduara kabla ya mkutano kuanza  Bwana Salum Bimani, mkurugenzi wa haki za binadamu CUF akiwasili jukwaani  Naibu katibu mkuu Zanzibar na muwakilishi wa Mjimkongwe Mh.Ismail Jussa Ladhu ndiye alikuwa mgeni rasmi wakati wa mkutano wa kuzindua kampeni Baadhi ya wananchi wakiwa kwenye mkutano wa CUF jana Kiboje jimbo la Uzini Na mdau wa Mjengwablog,Zanzibar

MDAHALO WA KATIBA MPYA ZANZIBAR

Na Khadija Khamis –Maelezo 30/01/2012. Mjumbe wa Baraza la Katiba Zanzibar na Mwanasheria wa kujitegemea Ali Saleh amewashauri Wananchi wa Zanzibar kuwa makini katika kuwasilisha maoni yao ya kutetea maslahi ya Zanzibar na sio kuburuzwa na Wanasiasa ambao wanajali zaidi maslahi yao. Ushauri huo ameutoa wakati alipokuwa katika mdahalo wa kujadili dhana nzima ya marekebisho ya Katiba na Wananchi wa Mkwajuni Wilaya ya Kaskazini A Unguja. Mjumbe huyo alisema kuwa ndani ya mjadala wa Katiba kuna mambo mengi ya kujadiliwa lakini kwa upande wa Zanzibar la muhimu zaidi ni kujadili kero za Muungano kwani hii ndio nafasi pekee ya kuwakilisha mambo yanayowayima fursa Wazanzibar. Akifafanua zaidi alisema kuwa suala la Muungano ndio muhimu kwa Wazanzibari kwa sababu limewaunganisha na sehemu ya pili ya Muungano ambapo kuwekwa sawa kwake kutaleta mabadiliko makubwa ya Kisiasa na Kiuchumi kwa Zanzibar Alieleza kuwa kila si

JK abariki posho mpya za wabunge

Rais Kikwete KILA MMOJA KULIPWA 330,000 KWA SIKU, ZITTO, MAKAMBA, KIGWANGALA WASULUBISHWA KWA KUZIPINGA Waandishi Wetu, Dodoma WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amesema tayari Rais Jakaya Kikwete amesaini kuidhinisha ongezeko la posho za vikao (sitting allowance) kwa wabunge kutoka Sh70,000 hadi Sh200,000 kwa siku.  Kupitishwa kwa posho hizo ambazo ziliandikwa kwa mara ya kwanza na gazeti hili, kunafanya sasa mbunge kupokea Sh330,000 kwa siku; Sh200,000 zikiwa ni posho ya kikao, Sh80,000 posho ya kujikimu na Sh50,000 nauli. Taarifa za uhakika kutoka ndani ya kikao cha utanguzi cha wabunge jana, zilidai kuwa baada ya Pinda kutoa taarifa hiyo, wabunge walishangilia huku Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, akisimama na kudai kuwa taarifa alizonazo ni kwamba Rais Kikwete alikuwa hajasaini kuidhinisha posho hizo. Hatua hiyo ilisababisha Mbunge wa Kondoa Kaskazini, Juma Nkamia (CCM), kusimama na kuhoji iwapo Zitto ni miongoni mwa wasemaji wa Rais kabla ya Pin

Iz Blak Peeple Stoopid?: Rap and the Racial Inferiority Myth

by TRUTH Minista Paul    Tweet Share   View Comments             i   1 Vote Share with Shortlink:  ”I dumb down for my audience/ double my dollars…” – “Moment of Clarity”, Jay-Z Recently, students at Garvey University sponsored a debate between noted historian Dr. T. Asante Shakur and Professor Darwin J. Watson, author of the best selling book, Blacks Are Dumb…Get Over It ! While Dr. Shakur feverishly went through an hour long, high powered PowerPoint presentation, highlighting indisputable evidence of Black contributions to civilization over the last 5,000 years, Watson just listened quietly with a confident grin on his face. When it was his turn to speak, he just walked over to the podium, told the sound man to pum

MUONEKANO MPYA WA DHAHABU WA BIA YA SERENGETI LAGER WATIKISA JIJI LA DAR ES SALAAM

Meneja wa kinwaji cha Serengeti Lager kutoka kampuni ya bia ya Serengeti Bw. Allan Chonjo anayeendesha gari pamoja na Kanji ambaye pia ni mfanyakazi wa kampuni hiyo wakiongoza msafara wakati ulipopita mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es salaam leo, kuutambulisha muonekano mpya wa nembo ya bia ya Serengeti Lager huku ikiwa na ubora na viwango vilevile. Mkurugenzi wa FULLSHANGWE Bw. John Bukuku akisalimiana na Kamalade Ali Choki mkurugenzi wa bendi ya Extra Bongo na bendi yake ambaye ndiye anayetoa burudani katika promosheni hiyo jijini Dar es salaam. Mkurugenzi wa FULLSHANGWE akipiga stori na maafande wa kikosi cha usalama barabarani wakati walipokutana katika shughuli za promosheni hiyo kwenye makutano ya barabara za Shauri Moyo na Uhuru. Kamalade Ali Choki na mkundi lake la Extra Bongo wakifanya vitu vyao kwenye jukwaa la gari maalum. Mpiga gitaa la bass wa Extra Bongo akipiga gitaa huku mnenguaji wa bendi hiyo akicheza mbele yake wakati msafara huo ulipopita katika baraba

BREAKING NEWSSSS:DK HARRISON MWAKYEMBE AIBUKIA KWA MCHUNGAJI GWAJIMA KAWE

Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na Uzima lilloko Kawe Tanganyika Pakers akimkaribisha Dk Harrison Mwakyembe Mbunge wa Kyela na Naibu Waziri wa Ujenzi katika ibada iliyofanyika leo kwenye kanisa hilo na kuhudhuriwa na Waziri wa Afrika Mashariki mzee Samwel Sitta na baadhi ya wabunge kadhaa, Mzee Samwel Sitta amesema Mwakyembe amekwenda kanisani hapo ili kutoa ushuhuda kuhusu ugonjwa wake kwa ujumla ambapo FULLSHANGWE ilishuhudia tukio hilo. Dk. Harrison Mwakyembe ametoa ushuhuda akimshukuru mungu kwa kumbariki na kuendelea kumpa nguvu juu ya afya njema, Mwakyembe ambaye alikuwa amevalia kofia na Glovu katika mikono yake, ameongeza kwamba tangu alipokuwa ameondoka kwenda nchini India kwa matibabu Oktoba 9 mwaka jana hakuwahi kuvaa viatu, lakini leo amevaa, hivyo akamshukuru mungu kwa miujiza yake. Waziri wa Afrika Mashariki Samwel Sitta akiongea katika ibada hiyo na kumkaribisha Dk Harrison Mwakyembe ili kuzungumza machache na waumini wa kanisa hilo na kutoa ushuhuda wake.

CHANGAMOTO ZA MWAKA 2011 ZISIWAFANYE MKATEE TAMAA-MCHUNGAJI VOMO

NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE-ARUSHA IMEELEZWA kuwa pamoja na nchi kukabiliwa na majanga na changamoto mbalimbali hasa kwa mwaka 2011 wakristo hawapaswi kukata tamaa juu ya changamoto hizo bali wanatakiwa kuangalia imani na mahitaji ya Mungu Kwa mwanadamu ili aweze kupunguza na kuondoa changamoto hizo. Hayo yameelezwa mjini hapa na mchungaji Simion Vomo wakati akiongea na waumini wa kanisa la T.A.G Christian All Nation Church lilopo katika manispaa ya mji wa arusha mapema wiki hii. Aidha mchungaji Vomo alisema kuwa katika mwaka 2011 mambo mengi sana yalijitokeza hali ambayo iliwapelekea baadhi ya waumini kukata tamaa lakini katika mwaka huu mpya wa 2012 wanapaswa kumuangalia mungu zaidi kuliko matatizo yao binasi. Alibainisha kuwa hata katika matatizo mungu yupo na kwa hali hiyo kila mwanadamu anapaswa kuangalia mpango na mikakati mbalimbali ya mungu na kuachana na tabia ya kuona wameshindwa mbele

TWIGA STARS YAICHAPA NAMIBIA MAGOLI 5-2 UWANJA WA TAIFA

Mchezaji Mwanahamisi Omari a.k.a Gaucho akihojiwa na mwandishi wa habari wa BBC Eric David Nampesya baada ya kumalizika kwa mpira kati ya Twiga Stars na Namibia , Mwanahamis Omari 'Gaucho' ni mfungaji pekee wa mabao 2 kati ya 5 ya Twiga, katika mchezo wa kutafuta kufuzu kwa fainali za Afrika kwa Wanawake, zinazotarajia kufanyika mwezi Juni mwaka huu. Mchezo huo umemalizika muda mchache katika uwanja wa Taifa. Mabao ya Twiga yalifungwa na Mwnahamisi Omar katika dakika 21, Asha Rashid 'Mwalala', bao la pili dakika 46, bao la tatu Etoe Mlenzi, dakika ya 84, Asha Rashid,bao la nne dakika ya 88, na bao la tano, likifungwa tena na Mwanahamis, dakika ya 90. Mabao ya Namibia mawili ya yamefungwa na Beki wa Twiga, Etoe, aliyejifunga dakika ya 29 na bao la pili likifungwa na Juliana Skrywer, dakika 73. Kwa matokeo hayo sasa Twiga Stars inatarajia kukutana na mshindi kati ya Misri au Ethiopia ambapo Misri ilikuwa inaongoza kwa mabao 4-2 d

Vodacom Foundation yakabidhi madarasa 3 na madawati 100 S/Msingi Ruvu Darajani

Ofisa Mkuu wa masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba kushoto akipokea zawadi ya mbuzi toka kwa baadhi ya wazazi wa wanafunzi wa shule ya msingi ya Ruvu Darajani iliyopo mkoani pwani,mara baada ya kuwakabidhi rasmi vyumba vitatu vya madarasa na madawati 100 kwa ajili ya shule hiyo,Msaada huo uliotolewa na Vodacom Foundation umegharimu zaidi ya shilingi Milioni 98. Haya ndiyo madarasa ya shule ya msingi ya Ruvu Darajani iliyopo Mkoani Pwani yaliyojengwa na Vodacom Foundation. Mkurugenzi wa Wizara ya Elimu shule za Msingi,Zuberi Samataba mwenye suti akiongea jambo na 0fisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba,walipowasili katika shule ya msingi ya Ruvu Darajani iliyopo Mkoani Pwani kwa ajili ya kukabidhi msaada wa madarasa matatu na madawati 100 uliotolewa na Vodacom Foundation katika shule hiyo na kugharimu zaidi ya shilingi Milioni 98. Hili ndilo jiko la wanafunzi wa shule ya msingi ya Ruvu Darajani ili

Vodacom yatangaza promosheni ya punguzo la gharama

Wateja kupiga simu kwa robo shilingi. Kutuma SMS kwa 25/- Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania imetangaza promosheni ya aina yake ya punguzo la gharama za simu kupiga na kutuma ujumbe mfupi wa maneno- SMS itakayowahusisha wateja wa kampuni hiyo ambao sasa watapiga simu kwa gharama ya ROBO SHILINGI kwa sekunde. Promosheni hiyo ya siku saba kuanzia Jumatatu Januari 30, 2012 inahusu kupiga simu za ndani ya mtandao wa Vodacom yaani kupiga Vodacom kwenda Vodacom kati ya Saa nne usiku na saa moja asubuhi kila siku kwa wateja wote wa malipo ya kabla Aidha sanjari na ofa hiyo kamambe Vodacom imetoa pia punguzo la gharama ya kutuma ujumbe mfupi wa maneno hadi shilingi 25/- kwa ujumbe wakati wote wa siku kwenda mtandao wowote wa simu ya mkononi nchini kwa kipindi cha siku saba nayo pia kuanzia leo Jumatau Januari 30, 2012. Akitangaza promosheni hizo mbili Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Bw. Rene Meza amesema ni imani yake kwamb

Hot Stories from All Hip Hop

by Skyyhook     Tweet Share   View Comments             i   Rate This Share with Shortlink: I don’t think it’s a secret that in the last five to 10 years, social media has opened up access to celebrities and media personalities like never before. MySpace allowed us the amazing ability to “speak” to our favorites and actually get replies back! How gratifying it was the first time you sent someone that you truly enjoyed a message, and they responded!  The trend continued on through Facebook to a degree, but especially through Twitter. Twitter has allowed for celebs to be open and vulnerable with their fans in a way that they have never been previously. This should be a great thing for us all right? I thought so, too, but not so fast. Apparently, there is a price that celebs are paying for this ac

AIS DK. JAKAYA KIKWETE KATIKA MKUTANO WA (WORLD ECONOMIC FORUM) JIJINI DAVOS

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Bill and Melinda Gates Foundation Bw. Bill Gates wakati wa Kongamano la Uchumi Duniani mjini Davos, Switzerland  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje wa Australia Bw. Kevin Rudd wakati wa Kongamano la Uchumi Duniani mjini Davos, Switzerland Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika mazungumzo na Waziri Mkuu wa Thailand Bi. Yingluck Shinawatra wakati wa Kongamano la Uchumi Duniani mjini Davos, Switzerland Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Rais na Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Walmart Bw Doug Mc Millon wakati wa Kongamano la Uchumi Duniani mjini Davos, Switzerland Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikutana na Madame Sadako Ogata, Rais wa Japan International Cooperative Agency mjini Davos Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Waziri Mkuu wa Kenya Mh Raila Odinga baada ya kufanya naye mazungumzo mjini Davos Rais Jakay Mrisho Kikwete akiongea na Waziri Mkuu wa Uingereza Bw. David Cam