![]() |
| Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila |
WANANCHI
wa Jimbo la Kigoma Kusini wamefungua kesi ya kikatiba katika Mahakama
Kuu, Kanda ya Dar es Salaam wakiiomba iamuru kusitishwa kwa matumizi
ya Ibara ya 71 (1) (f) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano juu ya mbunge
aliyefukuzwa uanachama katika chama chake.
Pia
wapiga kura hao wameiomba Mahakama iliamuru Bunge litunge sheria
inayoruhusu mbunge aliyefukuzwa uanachama katika chama chake atambuliwe
kuwa mbunge huru au aruhusiwe kuhama na ubunge wake kwenda chama
chochote atakachotaka.
Kesi
hiyo imefunguliwa siku chache tangu Mbunge wa Kigoma Kusini, David
Kafulila avuliwe uanachama wa NCCR-Mageuzi, hatua ambayo kikatiba
inamvua ubunge wake. Kafulia alivuliwa uanachama Novemba 20, mwaka
jana. Hata hivyo, amefungua kesi kupinga hatua hiyo.
Kadhalika,
siku tatu zilizopita, Baraza Kuu la Uongozi la Chama cha Wananchi
(CUF), lilimvua uanachama wa chama hicho Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid
Mohamed hatua ambayo inamfanya apoteze nafasi yake ya ubunge.
Jana,
CUF waliwasilisha barua katika Ofisi ya Spika wa Bunge, kumwarifu
kuhusu uamuzi wa kumvua uanachama Hamad, huku mbunge huyo akisema
uamuzi wa huo ni batili kwani ulikiuka amri ya mahakama iliyokuwa
ikizuia kufanyika kwa kikao chake.
Kesi ya Kikatiba
Wapiga
kura watatu wa Kigoma Kusini ndiyo waliofungua kesi hiyo ya kikatiba na
kila mmoja anatoka katika chama tofauti cha siasa. Mmoja ni mwanaCCM,
mwingine CUF na wa tatu anatoka NCCR Mageuzi. Walifungua kesi hiyo kwa
niaba ya wananchi wengine wa jimbo hilo dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa
Serikali na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...Soma
zaidi mwananhi.co.tz

Comments