NaHamad Hija Maelezo zanzibar
MABINGWA
wa soka Tanzania Bara timu ya Yanga ya Dar es salaam jana ilifufua
matumaini ya kuendelea na michuano ya kombe la Mapinduzi baada ya
kuifunga timu ya Kikwajuni ya Zanzibar mabao 2-0 katika mchezo
uliyochezwa katika kwenye uwanja wa Amani mjini Zanzibar
Katika
mechi hiyo ambayo Yanga ilishinda hapo jana kunako dakika ya 24 ya
kipindi cha kwanza ndipo Yanga walipoandika goli la kwanza kupitia kwa
mshambuliaji wao Jerry Tegete ambaye aliukwamisha mpira huo wavuni
ukimuacha mlinda mlango wa kikwajuni akiwa hana la kufanya
Yanga
ambayo inashiriki katika michuano hiyo ya Mapinduzi Cup jana ilishinda
mchezo huo ambapo katika kipindi cha pili katika dakika ya 85 walipata
goli la pili lilofungwa na mchezaji Pius Kisambale ambaye alifunga bao
hilo na hivyo kuifanya yanga kuondoka na ushindi wa mabao 2-0
Kabla
ya mchezo wa hapo jana Mabingwa hao wasoka Tanzania bara wanaoshiriki
kombe la mapinduzi tayari wamefungwa na timu ya Mafunzo bao 1-0 katika
michuano hiyo inayoendelea huko katika uwanja wa Amani mijini Zanzibar
ambao ni mabingwa wa soka wa Zanzibar
Habari
tulizozipata kutoka vyanzo mbali mbali vya habari ni kwamba timu ya
yanga inarajia kuongeza nguvu katika mashindano hayo kwa kuleta
wachezaji wengine wa timu hiyo ya Darsalaam
Huku
ikiwa Mabingwa hao wa soka wa Tanzania bara wakiwa wameshinda mechi
hiyo hapo jana mahasimu wao simba na mabingwa wa kombe hilo juzi
walipoteza mchezo kwa kufungwa mabao 2-1 na timu ya Jamhuri yenye
maskani yake Kisiwani Pemba
Kwa
kufanyika kwa mashindano haya kuadhimisha miaka 48 ya mapinduzi ya
Zanzibar yamekuja katika kipindi muafaka kwani kati ya timu zinashiriki
mashindano hayo timu ya yanga simba Jamhuri Mafunzo ni mashindano
ambayo yatawasaidia sana kwani ni timu zinazotuwakilisha katika
mashindano mbali mbali
Timu
ya Yanga ambao ni mabingwa Tanzania bara wanatukilisha katika klabu
bingwa ya Afrika ambapo timu ya simba inashiriki katika kombe la
shiriisho wakati timu ya Mafunzo mabingwa wa soka wa Zanzibar
wanashiriki klabu bingwa ya Afrika ambapo Jamhuri ambao ni makamo
bingwa wa ligi ya Zanzibar wanatuwakilisha katiksa kombe la shirikisho
Katika
sherehe hizi za maadhimisho ya miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar timu
zinazoshiriki mashindano hayo ni pamoja na Mabingwa wa soka wa Tanzania
Bara timu ya Yanga Simba na Azamu ambazo zote hizi zipo jijini Darsallm
huku timu ya Jamhuri Kikwajuni Miembeni United kmkm ni kutoka zanzibar .Inatoka kwa mdau mjengwa.
Comments