Skip to main content


MWANDISHI wa habari wa Kampuni Mwananchi Communications Limited (MCL), Beatus Kagashe (31), pichani, amefariki dunia juzi usiku.Kifo cha mwandishi huyo aliyekuwa akiandikia gazeti la The Citizen, kilitokea katika Hospitali ya Ocean Road, Dar es Salaam ambako alikuwa amelazwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa saratani ya damu baada ya kutibiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Aga Khan kwa miezi miwili.

Msemaji wa familia ya marehemu Gasper Mikimba alisema, Kagashe alifariki mnamo saa 2:45 usiku na kwamba familia iko katika mipango ya mazishi ambayo yatafanyika Bukoba mkoani Kagera. Alisema mwili wa marehemu unatarajiwa kusafirishwa kwenda huko Jumanne na mazishi kufanyika Jumatano.

“Bado tunaendelea na mipango ya mazishi... lakini nadhani tutasafirisha mwili wa marehemu kwenda nyumbani Bukoba siku ya Jumanne kwa ajili ya mazishi,” alisema Mikimba.

Alisema kifo cha Kagashe kimeacha mshtuko mkubwa katika familia,jamii pamoja na taifa kwa ujumla hasa ikizingatiwa kwamba alikuwa bado kijana aliyetarajiwa kulijenga taifa lake.

Marehemu Kagashe alizaliwa Februari 23, 1981 mkoani Kagera na alipata elimu ya msingi katika Shule ya Bilele iliyoko Bukoba Mjini kati ya mwaka 1990 na 1996, alijiunga na Shule ya Sekondari Ihungo kuanzia mwaka 1997 mpaka 2000 kabla ya kujiunga na Shule Sekondari Mpwapwa kwa masomo ya kidato cha tano na sita.

Mwaka 2004, alichaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kusoma kozi ya uandishi wa habari (Bachelor ofn Arts Journalism) katika Taasisi ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kwa Umma (IJMC) alipohitimu mwaka 2007. Alijiunga na masomo ya shahada ya uzamili katika masuala ya utawala (Masters in Public Administration) katika Chuo Kikuu cha Mzumbe mwaka 2010 na kuhitimu Novemba mwaka jana.

Mhariri Mtendaji wa Gazeti la The Citizen, Bakari Machumu alisema amepokea kifo cha marehemu Kagashe kwa masikitiko makubwa. Alimwelezea kama kijana aliyekuwa mpenda watu na mwenye kusimamia alichokiamini.

“Tulidhani alikuwa anaendelea vizuri na matibabu... nimepata mshtuko kusikia kwamba Kagashe ameaga dunia. Nilikutana naye hospitali wiki moja iliyopita alionekana kuwa na nguvu ya kupambana na ugonjwa wake,” alisema Machumu.

Alisema idara yake imepoteza hazina ambayo Mwananchi Communications Limited ilikuwa imewekeza kwa manufaa ya kampuni pamoja na gazeti.

Alisema marehemu Kagashe alikuwa ni zao la utaratibu wa kusaka vipaji kutoka vyuo vya elimu ya juu, programu iliyoanzishwa na Kampuni ya Mwananchi mwaka 2007 akiwa miongoni mwa vijana watano wa kwanza wa kundi la kwanza la programu hiyo.

“Kagashe alitokana na mpango wa kusaka vipaji katika vyuo vya elimu ya juu...mamia ya wahitimu wa vyuo vikuu nakumbuka walijitokeza lakini Beatus Kagashe alikuwa miongoni mwa wanafunzi watano bora, hivyo kujiunga na kozi maalumu huko Nairobi,Kenya,” alisema Machumu.

Kagashe aliajiriwa aliajiriwa na Mwananchi Communications Limited, kampuni inayochapisha magazeti ya The Citizen, Mwananchi na Mwanaspoti mnamo mwaka 2008. Ameacha mjane, Doroster Kagashe na mtoto Emmanuel Mujuni ambaye ana umri wa mwaka mmoja.
Chadema wamlilia
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kimepokea kwa majonzi na masikitiko makubwa, taarifa za kifo cha Kagashe.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mwenezi wa chama hicho, Tumaini Makene imesema: “Kwa wale waliokuwa wakimfahamu marehemu Kagashe, watakubali kuwa alikuwa mmoja wa waandishi makini, waliokuwa wakiamini jamii ya Watanzania inaweza kufanya mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi na kijamii.”

Alisema kwa kutumia vema taaluma yake, akiongozwa na maadili ya tasnia ya habari, alishirikiana na Watanzania wenzake katika kuelimisha, kuhabarisha, kuhamasisha na kuburudisha umma, katika masuala mbalimbali kupitia kalamu yake.

“Tunatoa pole kwa ndugu, jamaa, marafiki na wafanyakazi wenzake na kuwaombea kwa Mungu awape moyo wa subira katika wakati huu mgumu wa majonzi kwa kuondokewa na mpendwa wao,” alisema Makene.Itoka kwa mdau Mjengwa.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...