Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2015

FARID WA AKADEMI AIPELEKA AZAM FC FAINALI KAGAME, KCCA YAFA 1-0 TAIFA

Shangwe za shujaa; Farid Malik Mussa akishangilia baada ya kuifungia bao pekee Azam FC leo dhidi ya KCCA   Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM CHIPUKIZI aliyepandishwa kutoka akademi mwaka juzi, Farid Malik Mussa leo amekuwa shujaa wa Azam FC baada ya kufunga bao pekee lililoiwezesha timu hiyo kutinga Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame. Farid mwenye umri wa miaka 18, alifunga bao hilo dakika ya 76 kwa ustadi wa hali ya juu, baada ya kuruka juu kwenda kuunganisha kwa guu la kushoto krosi ya Ame Ally ‘Zungu’. Azam FC sasa itamenyana na Gor Mahia ya Kenya katika fainali Jumapili- hiyo ikiwa ni mara ya pili kwa timu hiyo ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake kufika hatua hiyo, baada ya awali, mwaka 2012 kufungwa na Yanga SC 2-0 Dar es Salaam pia.   Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Suleiman Ahmed wa Djibouti aliyesaidiwa na Yatayew Balachew wa Ethiopia na Nagi Ahmed wa Sudan, kipindi cha kwanza timu zote zilish

Ebu tupia macho mtazamo wa Ngasa kwa Yanga

KIUNGO mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mrisho Khalfan Ngassa amesema Yanga SC kwa sasa ina matatizo mawili makubwa ya kutatua haraka kabla ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kuanza. Tatizo la kwanza ni timu kukosa namba 10 na tatizo la pili ni ubinafsi wa washambuliaji ambapo kila mtu anataka kufunga peke yake. Ngassa aliyeondoka Yanga SC Mei mwaka huu kuhamia Free State Stars ya Afrika Kusini, amesema Yanga SC haina mchezaji wa kucheza nafasi ya namba 10 na pia wachezaji wote wa mbele wanataka kufunga. Akizungumza na mdau wa habari hizi , Ngassa alisema kwamba Yanga SC ina wachezaji wa aina moja tu ambao wote wanaweza kucheza kama namba 9.“Yanga SC inakosa namba 10. Mchezaji wa kupenya penya pale ndani, Malimi Busungu anaweza kutumika namna hiyo, lakini mechi na Azam alicheleweshwa kuingia uwanjani,”alisema Ngassa. Lakini pia mchezaji huyo wa zamani wa Yanga SC amesema kwamba kuna tatizo lingine katika safu ya ushambuliaji la Yanga, kila mchezaji anat

Kocha Simba Aanza kutengeneza nyota wa kuziba pengo la Okwi

Baada ya Emmanuel Okwi kutimka zake kwenda Denmark, kocha wa Simba Dylan Kerr, ameamua kufanya jambo la maana mapema kwa kugawa jukumu alililokuwa akilifanya Mganda huyo kwa mzawa Ibrahim Ajibu. Ajibu amepewa mikoba ya Okwi ya kupiga mipira ya faulo baada ya kuonesha umahiri mkubwa wa upigaji adhabu hiyo mbele ya kikosi maalumu cha upigaji faulo kilichochaguliwa na Kerr. Mbali na Ajibu, wachezaji wengine ambao wanashiriki zoezi hilo la upigaji faulo kwenye kambi inayoendelea visiwani Zanzibar ni Mussa Hassan ‘Mgosi’, Said Ndemla, Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ na Hamis Kiiza. Kocha Kerr alisema: “Ninaangalia ni wachezaji wapi wenye umakini wa kupima, pia wenye uwezo wa kupiga kwa nguvu na kwa maarifa. “Hao watano ndiyo nilioanza nao, nitaendelea kuangalia wengine kwani kila mmoja anaweza kufanya kazi hiyo.” Kocha huyo aliongeza kusema anavutiwa na Ajibu kwa uwezo wake wa kuyadanganya macho ya kipa pindi anapokuwa anapiga mpira. Naye Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola

Jamal Malinzi aipongeza Azam FC

  Kikosi cha Azam FC Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi ametuma salam za pongezi kwa klabu ya Azam FC kwa kufanikiwa kuingia katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Kagame inayotimua vumbi jijini Dar es Salaam. Katika salamu zake kwa uongozi wa klabu ya Azam, Malinzi amewataka kutobweteka na kuongeza bidii katika hatua hiyo ya nusu fainali ili waweze kufuzu kwa hatua ya fainali na kutwaa Ubingwa huo na kuwaomba watanzania wote kuwasapoti wawakilishi pekee wa nchi kwenye michuano hiyo TFF kwa niaba ya familia ya mpira na watanzania wote, inatwakia kila la kheri Azam FC katika mchezo wake wa kesho wa nusu fainali dhidi ya KCCA.

Imebaki Story toka kwa PHD

Muda wa uandikishaji BVR Dar waongezwa

Tume ya Uchaguzi (NEC) leo imetangaza kuongeza siku nne zaidi za uandikishaji wa wapigakura kwa kutumia teknolojia ya BVR baada ya idadi kubwa ya wakazi wa Dar es Salaam kuitikia wito wa zoezi hilo. Awali zoezi hilo lilikuwa likamilike leo, Julai 31, lakini sasa litaendelea hadi Agosti 4, mwaka huu ili kukabiliana na idadi kubwa ya watu waliojitokeza kujiandikisha. Kwa mujibu wa chombo hicho chenye mamlaka ya kusimamia shughuli zote za uchaguzi nchini, hadi jana, zaidi ya wakazi 1,000,000 walikuwa wamekwishaandikishwa jijini Dar es Salaam. Ikizingatia matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, Nec inatarajia kuandikisha jumla ya wakazi zaidi ya 2.8 milioni wa jiji hilo lenye idadi kubwa ya watu nchini Tanzania. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Nec, Jaji Damian Lubuva, hadi sasa jumla ya zaidi ya watu 18 milioni wamekwishajiandikisha wakati tume i

RAIS MUSEVEN AFUNGUA MKUTANO WA MARAIS WASTAAFU JIJINI DAR

Mh. Rais Yoweri Museveni wa Uganda akifungua rasmi mkutano wa Marais wastaafu wa Afrka AFRICA LEADERSHIP FORUM unaofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam Mkutano huo unaojumuisha marais wastaafu Benjamin Mkapa wa Tanzania , Olusegun Obasanjo wa Nigeria, Hifikepunye Lucas Pohamba wa Namibia, Festus Mogaye wa Botswana, Bakili Muluzi wa Malawi na Jerry Rowlings wa Ghana unajadili masuala mbalimbali ya maendeleo katika bara la Afrika na Changamoto zinazokabili barahilo na umeandaliwa na Taasisi ya Uongozi Institute.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM) Marais wastaafu Bakili Muluzi wa Malawi kulia na Jerry Rawlings wa Ghana wakiwa katika mkutano huo. Rais Mstaafu wa Nigeria Olusegun Obasanjo kushoto na Salim Ahmed Salim Katibu Mkuu Mstaafu wa AU na Waziri mkuu Mstaafu wa Tanzania wakiwa katika mkutano huo. (P.T) Baadhi ya waalikwa kutoka taasisi mbalimbali wakiwa katika mkutano huo. Gavana wa Benki KuuProf. Beno

CHADEMA Vs CCM...!

Chadema, Bulaya almanusura

Wabunge wawili waliohama CCM hivi karibuni, James Lembeli na Ester Bulaya wamepitishwa katika kura za maoni kuwania ubunge kupitia chama chao kipya. Wakati Lembeli akipitishwa kwa kura za kishindo kuwania ubunge katika Jimbo la Kahama Mjini, Bulaya alishinda katika nafasi ya viti maalumu baada ya kushindwa katika kinyang’anyiro cha Jimbo la Bunda Mjini. Wanasiasa hao sasa wanasubiri uteuzi wa Kamati Kuu ya Chadema utakaofanyika Agosti 5 na 6. Ushindi wa Lembeli Katika uchaguzi huo wa juzi, mbunge huyo wa zamani wa Kahama aliwabwaga wenzake 13 aliogombea nao akipata kura 168 kati ya 262 zilizopigwa, akifuatiwa na John Katibu aliyepata kura 45, Peter Shita (17) na Emmanuel Madoshi aliyepata kura 10. (P.T) Wengine ni Muta Nyerere (4), Felician Maige (4), Zacharia Obadia (3), Tadeo Mwati (2), Arnold Mtajwaka (2), Prosper Denga (2), Deusdedit Madinda (1), Reuben Macheyeki (1). Victor Mbwana na

Lowassa ni mzigo, Slaa angekuwa chaguo sahihi!

Johnson Mbwambo Lowassa ni mzigo, Slaa angekuwa chaguo sahihi! Toleo la 416 29 Jul 2015 WAKATI naandika makala hii, habari zilikuwa zimezagaa ya kuwa Umoja wa Vyama vya Upinzani nchini (Ukawa), na hasa Chadema walikuwa wamekubaliana kumpokea Edward Lowassa na kumfanya kuwa mgombea urais wao kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba. Nathubutu kueleza wazi kwamba hilo ni kosa ambalo watalijutia kwa miaka mingi. Sijui nini kilikuwa kinaendelea katika vichwa vya viongozi wa Ukawa wakati wakifanya maamuzi ya mwisho ya kumpokea Edward Lowassa na hata kumfikiria kuwa ndiye anayestahili kupeperusha bendera yao kumkabili Dk. John Magufuli wa chama tawala, CCM, kwenye patashika ya Oktoba ya kuwania kukamata dola. Najua ya kwamba ‘siasa ni mchezo mchafu’, lakini bado najiuliza maswali kibao kichwani mwangu ya ni hoja zipi Chadema ilizizingatia katika kumkubali Lowassa – mtu ambaye chama hicho kilimuorodhesha katika ile orodha ya Mwembe Yanga ya watuhumiwa wakuu wa ufisadi