Skip to main content

FARID WA AKADEMI AIPELEKA AZAM FC FAINALI KAGAME, KCCA YAFA 1-0 TAIFA


Shangwe za shujaa; Farid Malik Mussa akishangilia baada ya kuifungia bao pekee Azam FC leo dhidi ya KCCA 
Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
CHIPUKIZI aliyepandishwa kutoka akademi mwaka juzi, Farid Malik Mussa leo amekuwa shujaa wa Azam FC baada ya kufunga bao pekee lililoiwezesha timu hiyo kutinga Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame.
Farid mwenye umri wa miaka 18, alifunga bao hilo dakika ya 76 kwa ustadi wa hali ya juu, baada ya kuruka juu kwenda kuunganisha kwa guu la kushoto krosi ya Ame Ally ‘Zungu’.
Azam FC sasa itamenyana na Gor Mahia ya Kenya katika fainali Jumapili- hiyo ikiwa ni mara ya pili kwa timu hiyo ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake kufika hatua hiyo, baada ya awali, mwaka 2012 kufungwa na Yanga SC 2-0 Dar es Salaam pia.  
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Suleiman Ahmed wa Djibouti aliyesaidiwa na Yatayew Balachew wa Ethiopia na Nagi Ahmed wa Sudan, kipindi cha kwanza timu zote zilishambuliana kwa zamu.
Azam FC walipoteza nafasi mbili za kufunga dakika ya tisa Nahodha wake, John Raphael Bocco ‘Adebayor’ akimdakisha kipa wa KCCA, Opio Emmanuel na dakika ya 33 Kipre Herman Tchetche alipiga nje.
Farid Mussa akimtoka beki wa KCCA leo Uwanja wa Taifa
Beki wa KCCA, Hassan Wasswa akimzuia mshambuliaji wa Azam FC, Kipre Tchetche asiufikie mpira
Kiungo wa Azam FC, Mudathir Yahya akipambana na Nahodha wa KCCA, Tom Masiko
Mshambuliaji wa Azam FC, John Raaphael Bocco akimiliki mpira mbele ya beki wa KCCA
Beki wa Azam FC, Erasto Nyoni akiwatoka mabeki wa KCCA

Nafasi nzuri zaidi ambayo KCCA wataijutia kwa kushindwa kuitumia kipindi cha kwanza ilikuwa ni dakika ya 36, baada ya shuti kali la Isaac Sserunkuma kudakwa na kipa wa Azam FC, Aishi Salum Manula.
Kipindi cha pili, Azam ilikianza kwa mabadiliko, wakimpumzisha kiungo aliyefanya kazi nzuri Mudathir Abbas Yahya na kumuingiza mshambuliaji Ame Ally ‘Zungu’.
Mabadiliko hayo hakika yaliisaidia Azam FC, kwani iliongeza kasi ya mashambulizi langoni kwa wapinzani na hatimaye baada ya kosakosa kadhaa, Farid akaipeleka timu fainali dakika ya 76.
Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Aggrey Morris, Serge Wawa, Said Mourad, Erasto Nyoni/Shomary Kapombe dk65, Farid Mussa, Jean Baptiste Mugiraneza, Frank Domayo, Mudathir Yahya/Ame Ally ‘Zungu’ dk46, John Bocco na Kipre Herman Tchetche/Didier Kavumbangu dk75.
KCCA; Opio Emmanuel, Thom Masiko, Joseph Ochaya, Hassan Wasswa, Dennis Okoth, Muzamiru Mutyaba, Iven Ntege, Hakim Senkuma, Isaac Sserunkuma/Shaaban Kondo dk37, Timoth Awany na Habib Kavuma/Michael Birungi dk81.
Farid Mussa akishangilia na Said Mourad na Frank Domayo

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...