Skip to main content

FARID WA AKADEMI AIPELEKA AZAM FC FAINALI KAGAME, KCCA YAFA 1-0 TAIFA


Shangwe za shujaa; Farid Malik Mussa akishangilia baada ya kuifungia bao pekee Azam FC leo dhidi ya KCCA 
Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
CHIPUKIZI aliyepandishwa kutoka akademi mwaka juzi, Farid Malik Mussa leo amekuwa shujaa wa Azam FC baada ya kufunga bao pekee lililoiwezesha timu hiyo kutinga Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame.
Farid mwenye umri wa miaka 18, alifunga bao hilo dakika ya 76 kwa ustadi wa hali ya juu, baada ya kuruka juu kwenda kuunganisha kwa guu la kushoto krosi ya Ame Ally ‘Zungu’.
Azam FC sasa itamenyana na Gor Mahia ya Kenya katika fainali Jumapili- hiyo ikiwa ni mara ya pili kwa timu hiyo ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake kufika hatua hiyo, baada ya awali, mwaka 2012 kufungwa na Yanga SC 2-0 Dar es Salaam pia.  
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Suleiman Ahmed wa Djibouti aliyesaidiwa na Yatayew Balachew wa Ethiopia na Nagi Ahmed wa Sudan, kipindi cha kwanza timu zote zilishambuliana kwa zamu.
Azam FC walipoteza nafasi mbili za kufunga dakika ya tisa Nahodha wake, John Raphael Bocco ‘Adebayor’ akimdakisha kipa wa KCCA, Opio Emmanuel na dakika ya 33 Kipre Herman Tchetche alipiga nje.
Farid Mussa akimtoka beki wa KCCA leo Uwanja wa Taifa
Beki wa KCCA, Hassan Wasswa akimzuia mshambuliaji wa Azam FC, Kipre Tchetche asiufikie mpira
Kiungo wa Azam FC, Mudathir Yahya akipambana na Nahodha wa KCCA, Tom Masiko
Mshambuliaji wa Azam FC, John Raaphael Bocco akimiliki mpira mbele ya beki wa KCCA
Beki wa Azam FC, Erasto Nyoni akiwatoka mabeki wa KCCA

Nafasi nzuri zaidi ambayo KCCA wataijutia kwa kushindwa kuitumia kipindi cha kwanza ilikuwa ni dakika ya 36, baada ya shuti kali la Isaac Sserunkuma kudakwa na kipa wa Azam FC, Aishi Salum Manula.
Kipindi cha pili, Azam ilikianza kwa mabadiliko, wakimpumzisha kiungo aliyefanya kazi nzuri Mudathir Abbas Yahya na kumuingiza mshambuliaji Ame Ally ‘Zungu’.
Mabadiliko hayo hakika yaliisaidia Azam FC, kwani iliongeza kasi ya mashambulizi langoni kwa wapinzani na hatimaye baada ya kosakosa kadhaa, Farid akaipeleka timu fainali dakika ya 76.
Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Aggrey Morris, Serge Wawa, Said Mourad, Erasto Nyoni/Shomary Kapombe dk65, Farid Mussa, Jean Baptiste Mugiraneza, Frank Domayo, Mudathir Yahya/Ame Ally ‘Zungu’ dk46, John Bocco na Kipre Herman Tchetche/Didier Kavumbangu dk75.
KCCA; Opio Emmanuel, Thom Masiko, Joseph Ochaya, Hassan Wasswa, Dennis Okoth, Muzamiru Mutyaba, Iven Ntege, Hakim Senkuma, Isaac Sserunkuma/Shaaban Kondo dk37, Timoth Awany na Habib Kavuma/Michael Birungi dk81.
Farid Mussa akishangilia na Said Mourad na Frank Domayo

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.