Skip to main content

Magufuli Mgeni rasmi ufunguzi kagame Cup


Waziri wa Ujenzi akitabasamu mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi leo.
Waziri wa Ujenzi John Pombe Mgufuli ambaye pia ni Mgombea Urais kwa Tiketi ya CCM
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania limemtangaza rasmi Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni Mgombea Urais wa kwa Tiketi ya CCM John Pombe Magufuli kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa michuano ya Kagame katika mchezo utakao wakutanisha wenyeji  Yanga na  Gor Mahia ya Kenya mtanange utakao pigwa Tarehe 18 mwezi huu.
Akiongea na waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es Salaam Afisa habari wa TFF Baraka Kaziguto amesema kuwa magufuli atakuwa mgeni rasmi katika ufunguzi huo akiongozana na viongozi wengine wa serikali.Inatoka kwa mdau

Comments