Skip to main content

Taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu CUF na UKAWA


Taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu CUF na UKAWA
Viongozi wa UKAWA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
15 Julai 2015
CUF NA UKAWA
Waheshimiwa waandishi wa Habari
Chama cha wananchi CUF tukiwa sehemu ya UKAWA tunaendelea na vikao vya kuafikiana na maamuzi kwa hoja mbalimbali zinazohusu uimarishaji wa malengo ya uanzishwaji wa UKAWA.
Katika kikao cha UKAWA kilichofanyika tarehe 14 Julai 2015 Collesium Hotel Dar es Salaam, CUF hatukuweza kushiriki kikao hicho.
Sababu za kutoshiriki kwetu katika kikao hicho, kumetokana na sababu za kikatiba za ndani ya CUF kwa kuwa katika maamuzi yote yanayohusu masuala mazito ya kinchi kama haya,tuna desturi ya kukaa na kujadiliana kama chama kwanza katika kuafikiana na jambo lolote lile muhimu kwa maslahi ya taifa kama vyama vingine vinavyofanya.
Baada ya kikao cha UKAWA cha 11/07/2015 CUF tume kuwa na vikao vinavyohusisha viongozi wakuu wa chama yaani Mwenyekiti,Naibu Katibu Mkuu na wakurugenzi na jana tumeendelea na kikao.
Na ndio maana katika kikao cha UKAWA Mwenyekiti Prof.Lipumba na sisi viongozi wa kuu hatukuweza kuhudhuria.
Kutohudhuria kwa kikao cha tarehe 14 Julai 2015, hakuna mahusiano yoyote na uvumi kwamba CUF imesusia au kujitoa katika UKAWA kama baadhi ya mitandao ya kijamii au vyombo vya habari vilivyoripoti pamoja na maneno ya chini kwa chini yanayoendelea kwa wananchi, bali ni kutokana na baadhi ya Wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la taifa kutoka mikoani na wanachama wetu maeneo mengi ya nchi kuutaka uongozi wa Chama kusitisha kwa muda kuhitimisha maamuzi ya kumpata mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupeperusha bendera ya UKAWA mpaka kuwepo kwa ridhaa ya Chombo hicho cha kikatiba.
Aidha Chama kinatambua kwamba hivi sasa tumebakiwa na muda mfupi kabla ya kuingia katika mchakato rasmi wa kuchukua fomu za serikali kuomba kuteuliwa kuwania uongozi, hivyo Chama kimeitisha kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la taifa hapo tarehe 25 Julai 2015 ilikupata Baraka ya chombo cha maamuzi kama ambavyo wenzetu washirika wa UKAWA wamekwishapitia hatua hizi katika vyama vyao.
Watanzania watambue kwamba Nchi inapitia katika kipindi kigumu sana, ongezeko la majimbo 26 ya Uchaguzi yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi,kwa kipindi cha chini ya siku 45 kabla ya kuanza kampeni ni changamoto ambazo UKAWA tunapaswa kuyafanyia kazi ili kuona namna gani tunajipanga kwa mazingira haya.
CUF tuanaamini kwamba kwa maridhiano ya pamoja ndani ya vyama vyetu na ndani ya UKAWA tutajenga UKAWA imara na hatimaye kuwa na mgombea mmoja wa Urais,Wabungena madiwani wa UKAWA na hivyo kuiangusha CCM kwenye uchaguzi wa Oktoba 25.
HAKI SAWA KWA WOTE
Magdalena Sakaya
Naibu Katibu Mkuu, Bara.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.