Skip to main content

Rais JK: azindua jengo jipya la CCM Dodoma


Rais Jakaya Kikwete akizindua jengo jipya la CCM mkoani Dodoma
Rais Jakaya Kikwete akizindua jengo jipya la CCM mkoani Dodoma
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi – CCM Rais Jakaya Kikwete amezindua rasmi jengo jipya la chama chake mjini Dodoma.
Akizindua jengo hilo lenye uwezo wa kuchukua watu mpaka elfu tatu kwa wakati mmoja Rais Kikwete amesema jengo hilo halitatumika na CCM pekee bali litakuwa pia ni kitega uchumi kwa chama hicho.
Rais Kikwete akipeana mkono na Katibu Mkuu CCM Abdulrahman Kinana baada ya kuzindua jengo la chama hiko Dodoma siku ya Alhamisi
Rais Kikwete akipeana mkono na Katibu Mkuu CCM Abdulrahman Kinana baada ya kuzindua jengo la chama hiko Dodoma siku ya Alhamisi
Ameeleza kuwa CCM inavitega uchumi vingi na hivyo ni vyema viongozi wa chama hicho wakaona haja ya kuviendeleza badala ya kuviacha kama vilivyo hivi bila kuingiza fiada yeyote.
Ukumbi huo unatarajiwa kutumika mara ya kwanza siku ya jumamosi tarehe 11 Julai, 2015 katika mkutano mkuu wa chama hicho utakao toa jina la mgombea urais kwa tiketi ya CCM.
Jengo jipya la CCM mkoani Dodoma
Jengo jipya la CCM mkoani Dodoma

Comments