Skip to main content

Minaj awalalamikia MTV kwa uteuzi wa tuzo


Rapa anaye wakilisha Young Money Nicki Minaj amefunguka yake yaliyomkwaza kwa kutumia akaunti yake ya twitter.
nicki-black-559x520
Minaj, amewauliza swali waandaji wa tuzo za MTV kwa upande wa nchi ya Marekani , ni kwa nini hawajaitaja video yake alioishirikiana na Beyonce “ Feeling Myself “ kuingia kwenye kipengele cha video bora ya mwaka ?.
Licha ya kushukuru kutajwa kwake kwenye vipengele vitatu ambavyo ni Best Female Video, Best Hip Hop Video “Anaconda”, na Best Collaboration “Jessie J, Ariana Grande, Nicki Minaj – “Bang Bang” “ , lakini Nicki Minaj bado alihoji uwepo au kutajwa kwa video ya Feeling Myself.
Nick Minaj aliandika “Hey guys @MTV thank you for my nominations. Did Feeling Myself miss the deadline or…? akimaanisha kwamba je video ya Feeling Myself ilichelewa kutoka au ?.
Tuzo hizo za MTV, za huko Marekani zinatarajiwa kutolewa siku ya jumapili ya augost 30 katika jiji la Los Angeles huku Miley Cyrus, akitarajiwa kuwa host wa onyesho jilo.

Comments