Skip to main content

Posts

Showing posts from March, 2015

Simon Sserunkuma ataka kuondoka Simba

Mshambuliaji wa Simba Simon Sserunkuma Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Simba, Simon Sserunkuma, amesema kuwa kwasasa hana furaha ndani ya klabu ya simba kutokana na kukosa nafasi ya kucheza kwenye kikosi cha kwanza cha kocha Goran Kopunovic. Nyota huyo alisajiliwa wakati wa msimu wa dirisha dogo msimu akitokea kwenye klabu ya Express ya Uganda, kipindi hiki amekuwa na wakati mgumu kutokana na kuwekwa katika risiti ya wachezaji wa akiba kwenye michezo mingi. Akizungumza na mwandishi wetu mchezaji huyo amesema kwasasa anatamani kuondoka klabuni hapo ili akatafute sehemu ambapo ataendelea kuimarisha kiwango chake.

Ivory Coast kutuma jeshi lake Nigeria

Rais wa Ivory Coast Alassane Quattara Ivory Coast kujiunga na Chad, Cameroon na Niger katika vita dhidi ya Boko Haram. Rais wa   Ivory Coast Alassane Ouattara amesema kuwa Ivory Coast itajiunga na nchi zingine za   Afrika   Magharibi katika kukabiliana na kundi la kigaidi la Boko Haram. Rais  Ouattara alisema hivyo katika kongamano la mabalozi mjini Abidjan ambapo aliahidi kutuma kikosi cha majeshi kujumuika na vikosi vya   Cameroon, Chad   na   Niger   katika kukabiliana na kundi hilo la kigaidi. Pia Ivory Coast itafanya mkutano na nchi wanachama wa   ECOWAS ili kupanga mkakati wa kukabiliana na Boko Haram.

Boko Haram wateka watu zaidi ya 400 Nigeria

Bibi huyu akiwa amepigwa bumbuazi baada ya wanae na wajuu kutekwa nyara Ripoti kutoka   Nigeria   zinadai kuwa kundi la kigaidi la Boko Haram limewateka nyara watu zaidi ya 400 katika mji wa Damasak ulioko kaskazini mwa nchi hiyo. Taarifa zaidi zinasema kuwa, Boko Haram liliwateka nyara watu hao na kuondoka nao wakati mji huo ulipokuwa ukikombolewa na vikosi vya Niger na Chad. Watu zaidi ya 400 hawajulikani waliko wengi wao wakiwa wanawake na watoto na inasemekana kuwa, Boko Haram imeondoka na raia hao wakati walipolazimika kuukimbia mji huo. Baadhi ya duru kutoka Damasak zinaripoti kwamba, zaidi ya watoto mia nne wenye umri wa takribani miaka 11 nao wametekwa nyara na Boko Haram. Serikali ya Nigeria imechukua hatua kali za usalama kabla ya uchaguzi wa Rais na Bunge ulizopangwa kufanyika Jumamosi ijayo.

KIPANYA

Aliyewahi kuwa Waziri Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mansour Himid Yussuf, ametangaza kujitosa katika kinyang’anyiro cha Uwakilishi katika jimbo la Kiembesamaki katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu kupitia chama cha wananchi CUF

Aliyewahi kuwa Waziri Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mansour Himid Yussuf --- Aliyewahi kuwa Waziri Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mansour Himid Yussuf, ametangaza kujitosa katika kinyang’anyiro cha Uwakilishi katika jimbo la Kiembesamaki katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Atachukua fomu ya kuwania jimbo hilo kupitia CUF. Mansour ambaye alifukuzwa uanachama ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Agosti 26 mwaka huu, baadaye alitangaza kujiunga na CUF. Akituhubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana katika Uwanja wa Bustanini, Kiembesamaki, alisema tayari amechukua fomu ya kuwania nafasi hiyo na ameirejesha. Mwanasiasa huyo alitumia mkutano huo kuwaomba radhi kwa matendo aliyokuwa akiyaona wakitendewa Wazanzibari, yakiwamo kupigwa na kudhalilishwa na Serikali wakati wote akiwa ndani ya Serikali. Akizungumzia safari yake ya kujiunga na CUF, Mansour alisema haikuwa rahisi kwake kwani wazee wa Kiembesam

Kauli ya JK kwa Polisi inahitaji ufafanuzi

Rais Jakaya Kikwete amelitaka Jeshi la Polisi nchini kujiandaa kikamilifu kukabiliana na vurugu zozote zitakazojitokeza wakati wa uandikishaji wa wapigakura, upigaji Kura ya Maoni kuhusu Katiba Inayopendekezwa pamoja na Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba, mwaka huu. Akizungumza juzi jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya maofisa warakibu wasaidizi iliyofanyika katika Chuo cha Taaluma ya Polisi, Rais Kikwete alisema dalili zinaonyesha kwamba kuna watu wamejipanga wakiwa na nia ya kuhatarisha amani wakati wa matukio hayo. Kwa tafsiri yoyote ile, kauli hiyo ya Rais Kikwete ni nzito na pengine ndio sababu wananchi wengi waliotupigia simu jana walionyesha hofu kwamba kauli hiyo inahitaji ufafanuzi, vinginevyo inaweza kuchukuliwa na Jeshi la Polisi kama agizo au kisingizio cha kuvunja haki za binadamu kwa kupambana na wananchi iwapo watapinga au kuhoji ukiukwaji wa sheria, taratibu na kanuni za uendeshaji wa matukio hayo muhimu kwa

THAMANI MJENGO WA DIAMOND BALAA

Mjengo huo wa Diamond uliopo maeneo ya Madale nje kidogo ya Jiji la Dar, unadaiwa kufikisha thamani hiyo kutokana na kuwa na vyumba vinne vya kulala, bwawa maalum la kuogelea (swimming pool), sehemu ya mazoezi (Gym), jakuzi, kaunta ya vinywaji, ukumbi wa kuchezea, studio ya muziki, uwanja wa mpira wa kikapu na sehemu ya kuchezea mchezo wa mishale (Darts) Kwa mujibu wa Diamond, nakshi za dhahabu alizoziweka katika kuta za bafu na chooni pekee, zimemgharimu sh. mil. 70 kitu kinachoendana na utabiri wa mkandarasi huyo kuwa nyumba hiyo inafikia thamani ya zaidi ya sh. mil. 400. Jikoni. Akiuzungumzia mjengo huo baada ya kuuona, mkandarasi mmoja ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini, alithibitisha kuwa mjengo huo unafikia sh. mil. 400 kwani umechukua nafasi kubwa, na 'material' yaliyojengea ni ya gharama. "Ukitazama kwa makini, material nyingi zilizotumika kwenye ujenzi ni zile ya daraja la

ZIARA YA KINANA JIMBO LA VUNJO MKOANI KILIMANJARO

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Kwa Mangi kata ya Kibosho Kati ambapo aliwaambia wananchi waache kujipitisha pitisha kugombea nafasi za uongozi kabla ya muda kuisha na kutangazwa. Zaidi ya wanachama 335 wamejiunga na CCM kwenye mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na mwanafunzi Elia PeterUlomi wa shule ya sekondari ya Somsom. Jengo la chuo cha KVTC kama lionekavyo kwa nje,ambapo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alitembelea Shamba la Mpunga lililopo Mabogini. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wanafunzi alipotembelea chuo cha KVTC-Kibosho Moshi vijijini. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupanda mti wa kumbukumbu kwenye chuo cha Ufundi KVTC,Kibosho wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana a

Wanasoka wa nje kupunguzwa England

Baadhi ya wachezaji wa kiafrika watakaathirika na sheria hiyo. Shirikisho la kanda kanda nchini England FA sasa linakusudia kuandaa sheria itakayo kupunguza idadi ya wachezaji kutoka nje ya nchi za Umoja wa Ulaya watakaosajiliwa katika ligi za nchi hiyo. Mwenyekiti wa shirikisho hilo Greg Dyke asema kwamba ligi kuu ya England ipo kwenye hatari ya kutowasaidia wachezaji raia wa Uingereza kama hatua hazitachukuliwa. Katika mpango pia itaweka sheria ngumu kwa wachazaji wenye vipaji waliokulia nchini humo. Mikakati hiyo yote ni ya kuimarisha timu ya taifa ya England ambayo imekuwa haifanyi vizuri kwenye mechi za kimataifa.Source BBC.

Minziro kutibua sherehe Yanga leo?

Fred Felix Minziro Yanga inaumana na JKT Ruvu ya Fred Felix Minziro leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, lakini ni kocha mkuu wa kikosi hicho cha wanajeshi anayeweza kutibua hesabu za mwenzake wa Yanga, Hans Pluijm kusaka ubingwa. Minziro aliyekulia na kucheza soka Yanga kwa maisha yake yote ya miaka 13, aliinoa timu hiyo kabla ya kutimuliwa, anakutana nayo (Yanga) ikiongoza ligi ikiwa na pointi 37 na kufuatiwa na Azam yenye pointi 36 na Simba ni ya tatu ikiwa na pointi 32. Kocha huyo alisema Yanga wasitarajie mteremko kwao na watakomaa nao leo kuhakikisha wanaondoka na pointi tatu. "Tuko vizuri na Yanga wasitarajie mteremko kwetu, tutacheza kwa kiwango kikubwa kuhakikisha tunaibuka washindi, najua ni timu nzuri na inaongoza ligi lakini hata sisi tuko pabaya tunahitaji kujinasua na kupanda nafasi za juu ili kukwepa kushuka daraja," alisema Minziro. Kwa upande wake, Pluijm amekiri kuwa hautakuwa mchezo rahisi kuikabili JKT Ru

Soma Kauli ya Sheikh Mkuu wa Bagamoyo kuhusu Masheikh waliokwenda kwa Lowasa

  Inatoka Hakingowi.com

NINAPOITAFAKARI CCM NA SERIKALI YAKE NACHANGANYIKIWA KABISA

"Masikio hayawezi kuvuka kichwa, kiongozi wa serikali usiyetaka kuambiwa ukweli na chama nenda kalale, acha kazi." Hii ni kauli ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi, Nape Nnauye aliyoitoa wakati akikemea ule aliouita uzembe wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu. Nape na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana bado wanaendelea kupaza sauti kuwa baadhi ya wateule wa mwenyekiti wao wa chama, Jakaya Kikwete hawaendani na kasi ya kutumikia jamii.Mwaka jana waliibuka na kibwagizo kuwa, serikali yao inayoongozwa na Rais Kikwete ina rundo la mawaziri mizigo, utashi wao ukawa ni kumtaka mwenyekiti awatimue wasikigharimu chama. Wakati kionjo hicho cha mawaziri mizigo kikionekana kupoa, wameibua kingine kinachoi

Bunge: Zitto kulipwa mafao yake yote

Kaimu Kiongozi wa serikali shughuli za bunge pia ambaye ni Waziri wa Uchukuzi ,Samuel Sitta, akiagana na aliyekuwa mbunge wa Kioma Kaskazini ,Zitto Kabwe. Ikiwa ni siku moja tangu Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kutangaza kung'atuka katika nafasi yake ya ubunge, Bunge limeeleza kuwa mbunge huyo atapata mafao yake yote kama wabunge wengine. Zitto ambaye alitangaza juzi bungeni kuwa anaondoka baada ya kuvuliwa unanachama wa Chadema aliahidi kuwa 'Mungu akipenda' atakuwa tena ndani ya chombo hicho cha kutunga sheria Novemba mwaka huu baada ya uchaguzi mkuu. Kuondoka kwa mbunge huyo pia kunaifanya nafasi ya uenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali(PAC) kuwa wazi kwa kuwa ndiye aliyekuwa akiishikilia hadi alipotangaza rasmi juzi kuachia ubunge. Akizungumzia uamuzi wa Zitto na juu ya mafao yake baada ya kuamua kuondoka mwenyewe, Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge, John Joel alisema kuwa mbun

Ryan Reynolds Reveals His Daughter's Name

The Huffington Post  |  By Leigh Blickley        Ryan Reynolds and Blake Lively have kept mum about the moniker of their little girl since she came into the world over the holiday season. But in an interview with the "Today Show," the actor confirmed that her name has been out there for a while . After joking with Willie Geist about names like Excalibur Anaconda Reynolds and Butternut Summersquas

ZIARA YA WAZIRI WA ARDHI MH. WILLIAM LUKUVI BABATI MKOANI MANYARA

Mkuu wa mkoa wa Manyara ,Mhe.Joel Nkaya Bendera akizungumza katika kikao cha viongozi wa wilaya zote za mkoa huo kilichofanyika ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Babati,kushoto ni Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Mhe.William Lukuvi na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Babati,Crispin Meela.Mhe.Bendera amesisitiza nidhamu ya kazi katika kuhudumia wananchi na ameapa kuwaondoa watendaji wabovu mkoani humo. Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Mhe.William Lukuvi akizungumza katika kikao cha viongozi wa wilaya zote za mkoa wa Manyara kilichofanyika ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Babati.Ameuagiza uongozi wa mkoa huo kumaliza migogoro ya ardhi ifikapo mwezi Mei mwaka huu. Mratibu wa Tume ya Waziri Mkuu ya kuhakiki na kuweka mipaka kwenye maeneo yenye migogoro ya ardhi mkoani Manyara,ambaye pia ni Mrasimu Ramani Mwandamizi,Bw.Benedict Mugambi akitoa maelezo ya hatua waliyofikia katika kuweka mipaka mkoani Manyara na kusema kuwa migog

Magazeti ya Leo

BABA HAJI: KANUMBA AMEONDOKA NA SANAA YA BONGO

Hamida Hassan na Shani Ramadhani/Risasi-GPL NYOTA wa filamu za Kibongo, Haji Adamu Rajabu ‘Baba Haji’ amefunguka kuwa, soko la filamu  Bongo kwa sasa linashuka siku hadi siku  na sababu kubwa ni  wasanii kutopenda kwenda shule kujiendeleza kielimu na kujua ni jinsi gani filamu inatakiwa kutengenezwa. Nyota wa filamu za Kibongo, Haji Adamu Rajabu ‘Baba Haji’. Akizungumza na Risasi Jumamosi,  Baba Haji alisema anakubaliana na kila mtu anayesema soko limeshuka kwa sababu wasanii wanapenda kukopi,  pia hawapendi kuandika miswada ya filamu na kupendelea kuingiza mambo ya kizungu, ingawa wengi wanamtaja msanii Steven  Kanumba kuwa ameondoka na soko hilo. Baba haji anafunguka kama hivi… (P.T) Risasi Jumamosi: Vipi, mbona kimya kingi? Soko la filamu limekwenda na Kanumba au unalionaje? Baba Haji: Tunaweza kusema hivyo, kwa sababu yeye alikuwa anajitoa kwa hali na mali, anatoa pesa zake kwa ajili ya filamu, ni tofauti na wasa

Andy Murry kuuaga ukapera

Ni mwaka wenye hadhi na uzito kwa mcheza tennis Andy Murray, hali hiyo si tu kutokana na matumaini yake ya kuongeza taji la pili la Grand Slam bali ni mpango alionao wa kufunga ndoa na mpenzi wake Kim Sears April mwaka huu. Mchezaji huyo raia wa Scotland amerejea katika nafasi ya nne duniani baada ya awali kuporomoka kutokana na upasuaji wa mgongo aliofanyiwa. Furaha ya mchezaji huyo inachagizwa zaidi kutokana na rekodi mpya aliyojiwekea baada ya kufanikiwa kutinga nusu fainali katika mashindano ya Indian Wells yanayoendelea huko California Marekani.

MASTAA NA SIASA

Chande abdallah ILIKUWA kama kitu cha ajabu baada ya mastaa wa fani mbalimbali nchini hasa wa muziki na filamu, kutangaza nia zao za kujiingiza kwenye masuala ya siasa ambapo mpaka sasa mastaa kama Profesa Jay na Afande Sele wameweka wazi nia zao huku mastaa kama Joseph Mbilinyi 'Sugu' ambaye ni Mbunge wa Mbeya Mjini na Vicky Kamata ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum wakiwa ni baadhi ya mastaa waliotinga bungeni tangu uchaguzi uliopita. Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi 'Sugu'. Bongo siyo nchi pekee ambayo suala hilo limejitokeza, bali hata kwenye nchi mbalimbali za Afrika, Ulaya na Marekani limewahi kutokea ambapo kwa nyakati tofauti mastaa wakubwa wamewahi kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali huku wengine wakishindwa na wengine kushinda nafasi za kuwakilisha wananchi katika nyadhifa mbalimbali. Wafuatao ni baadhi ya mastaa wakubwa wa majuu ambao wamewahi au wanaendelea kushiriki kwenye sia