Skip to main content

Boko Haram wateka watu zaidi ya 400 Nigeria


Bibi huyu akiwa amepigwa bumbuazi baada ya wanae na wajuu kutekwa nyara
Bibi huyu akiwa amepigwa bumbuazi baada ya wanae na wajuu kutekwa nyara
Ripoti kutoka Nigeria zinadai kuwa kundi la kigaidi la Boko Haram limewateka nyara watu zaidi ya 400 katika mji wa Damasak ulioko kaskazini mwa nchi hiyo.
Taarifa zaidi zinasema kuwa, Boko Haram liliwateka nyara watu hao na kuondoka nao wakati mji huo ulipokuwa ukikombolewa na vikosi vya Niger na Chad.
Watu zaidi ya 400 hawajulikani waliko wengi wao wakiwa wanawake na watoto na inasemekana kuwa, Boko Haram imeondoka na raia hao wakati walipolazimika kuukimbia mji huo.
Baadhi ya duru kutoka Damasak zinaripoti kwamba, zaidi ya watoto mia nne wenye umri wa takribani miaka 11 nao wametekwa nyara na Boko Haram.
Serikali ya Nigeria imechukua hatua kali za usalama kabla ya uchaguzi wa Rais na Bunge ulizopangwa kufanyika Jumamosi ijayo.

Comments