Skip to main content

BABA HAJI: KANUMBA AMEONDOKA NA SANAA YA BONGO

Hamida Hassan na Shani Ramadhani/Risasi-GPL
NYOTA wa filamu za Kibongo, Haji Adamu Rajabu ‘Baba Haji’ amefunguka kuwa, soko la filamu  Bongo kwa sasa linashuka siku hadi siku  na sababu kubwa ni  wasanii kutopenda kwenda shule kujiendeleza kielimu na kujua ni jinsi gani filamu inatakiwa kutengenezwa.
Nyota wa filamu za Kibongo, Haji Adamu Rajabu ‘Baba Haji’.
Akizungumza na Risasi Jumamosi,  Baba Haji alisema anakubaliana na kila mtu anayesema soko limeshuka kwa sababu wasanii wanapenda kukopi,  pia hawapendi kuandika miswada ya filamu na kupendelea kuingiza mambo ya kizungu, ingawa wengi wanamtaja msanii Steven  Kanumba kuwa ameondoka na soko hilo.
Baba haji anafunguka kama hivi…(P.T)
Risasi Jumamosi: Vipi, mbona kimya kingi? Soko la filamu limekwenda na Kanumba au unalionaje?
Baba Haji: Tunaweza kusema hivyo, kwa sababu yeye alikuwa anajitoa kwa hali na mali, anatoa pesa zake kwa ajili ya filamu, ni tofauti na wasanii wengine ingawa pia alikuwa akitumia sana ‘media’ kueleza kila anachokifanya.
Risasi Jumamosi: Unadhani ni kwa nini wasanii wengi wanapenda kufanya kazi na Wanaigeria?
Baba Haji: Kwa sababu wao wanalipwa tu ila nchi nyingine wana sheria kali, kufanya kwao filamu ni mpaka uwe na digrii ya sanaa.
Risasi Jumamosi:  Wewe umejipanga vipi kwa hilo? 
Baba Haji: Mimi nimejipanga vizuri kwa sababu nilikwenda Shule Bagamoyo (Pwani) kwa muda wa miaka mitatu na nilifanikiwa kupata diploma ya sanaa, wakati nakwenda shule nakumbuka Kanumba aliniambia napoteza muda kwani soko ndiyo lilikuwa limechanganya ila namshukuru Mungu hata niliporudi sijapotea sana kwa mashabiki.
Risasi Jumamosi: Una kipimo gani kinachoonesha hujapotea?
Baba Haji: Filamu nilizocheza ni nyingi na juzi nimegundua bado nipo baada ya filamu yangu ya Jamila na Pete ya Ajabu kutoka na kupokelewa na mashabiki vizuri mpaka wamelibadili jina langu kwa sasa wananiita Baba Jamila.
Risasi Jumamosi: Matarajio yako ya baadaye ni yapi?
Baba Haji: Mungu akipenda mwezi wa tisa narudi shule  kwa ajili ya kuchukua digrii ya sanaa ambayo nina uhakika itanipeleka mbali zaidi na nimefanikiwa kufungua kampuni yangu inayoitwa Hapa Production ambayo imeandaa filamu yangu ya kwanza ya Mama si Mama itatoka hivi karibuni Mungu akipenda.
Risasi Jumamosi: Unadhani ni kwa nini mnashindwa kupasua anga za kimataifa zaidi ukiacha ishu ya Kanumba kujitolea pesa zake mfukoni?Baba Haji: Nawashauri wasanii wajinoe zaidi kwenye lugha ya kigeni kwani na yenyewe inachangia wao kushindwa kufanya vizuri kwenye soko la kimataifa.
Marehemu Steven  Kanumba enzi za uhai wake.
Risasi Jumamosi: Unaweza kunipatia historia yako fupi ya sanaa tangu ulipoanzia mpaka sasa?
Baba Haji: Nilianza kuigiza 1998, nilianzia kundi lililoitwa Mtanzania ambalo lilikuwa chini ya Chama cha  Mapinduzi (CCM), mwaka 2000 nikaenda Nyota Academia kundi lililokuwa likiongozwa na mwalimu marehemu George Otieno ‘Tyson’, mkurugenzi akiwa ni Singo Mtambalike ‘Richie’.
Sikuishia hapo, mwaka 2002 tulianzisha Kundi la Kamanda Family nikiwa na Richie Mtambalike ambapo tulicheza michezo mbalimbali kisha tukaamua kuanza kucheza filamu ambapo tulicheza filamu ya Masaa 24 tukaona filamu ndiyo mpango mzima.
Mwaka 2003 nilicheza filamu ya Miss Bongo niliyoshirikiana na Aunt Ezekiel, iliyofuata ilikuwa ni Jeraha ya Ndoa, nilicheza na Monalisa.Mwaka 2004 nilikwenda Bukoba (Kagera) ambapo nilichukuliwa na Abantu Vision kwa ajili ya kufanya sinema iliyohusiana na mambo ya HIV ilivyoingia Tanzania. Filamu hiyo ilifanikiwa kuchukua Tuzo ya Ziff kama Filamu Bora ya mwaka 2005.
Mwaka 2010 nilijiunga na Chuo cha Sanaa Bagamoyo ambapo nilisoma mpaka kumaliza mwaka 2013.
Mwaka 2014 nilifanikiwa kucheza filamu nyingi kama vile Barbara, Kitoga, Don’t Cry, Mary Mary, Charles Mvuvi, Mwandishi wa Habari, Jamila na Pete ya Ajabu na Wa Mwisho Wewe.
Mwaka huu ndiyo wa mavuno kwangu kwani nimejiandaa vema kutoa filamu zangu mwenyewe ambazo zitakuwa na changamoto kubwa kwani nimesoma kwa ajili ya kuja kuvifanyia kazi na kuibadili kabisa tasnia ya filamu.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.