Skip to main content

Posts

Showing posts from November, 2016

WIZARA YA MAJI KUJENGA MTAMBO WA MAJITAKA UTAKAOGHARIMU BILIONI 200

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge akitoa hotuba ya uzinduzi wa Mkutano Mkuu wa kutathmini maendeleo ya sekta ya maji uliowashirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo kutoka ndani na nje ya nchi. Mkutano huo umefanyika leo katika ukumbi wa arnautoglo uliopo maeneo ya Mnazi Mmoja, Jijini Dar es Salaam. Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa maendeleo wa sekta ya maji walioshiriki katika Mkutano Mkuu wa kutathmini maendeleo ya sekta hiyo uliofanyika leo katika ukumbi wa arnautoglo uliopo maeneo ya Mnazi Mmoja, Jijini Dar es Salaam. Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO Wizara ya Maji na Umwagiliaji imejipanga kuanza ujenzi wa mtambo mkubwa wa majitaka katika maeneo ya Ilala Jijini Dar es Salaam ili kuzuia uchafuzi wa mazingira nchini. Hayo yamesemwa leo

Pep Guardiola:Awataka wachezaji kufanya tendo la ndoa na madem za

Samir Nasri alisema kitu ambacho kili make headline kubwa wiki hii kwamba manager Pep huwa anawambia wachezaji wafanye mapenzi kabla ya usiku wa manane ili wapate muda mrefu wa kupumzika. Nasri sasa hivi yupo kwenye mkopo Sevilla na hana dalili za kurudi City. Mambo mengine ambayo yapo wazi ni kwamba Pep alikata internet access kwenye eneo la mazoezi la Manchester City ili wachezaji waweze kuongea wao kwa wao na kuacha kutumia simu zao kwa muda mrefu. Kuhusu kufanya mapenzi mapema kabla ya usiku wa maneno sio kocha wa kwanza kuwa na imani hizo. Makocha wengi wanaamini kwamba kufanya tendo hilo mapema badala ya asubui humfanya mchezaji kuwa na nguvu za kutosha akiwa uwanjani. Kwenye mkutano wa waandishi wa habari bila kupoteza nafasi waandishi wa habari walimuuliza kocha Pep kuhusu maneno hayo ya Nasri. Jibu la Pep kuhusu yeye kuwaagiza wachezaji kufanya mapenzi mapema alijibu kwa mkato na kuendelea kuacha maswali mengi. Pep alisema, “Ni vigumu kwa mchezaji kuwa mch

Arsene Wenger : Awatuliza Mzuka mashabiki atianeno hakuna kupanic

Manager wa Arsenal amewambia mashabiki wa club yake kwamba haina haja ya kupanic baada ya kutoa draw na wakiwa kwenye harakati za kumaliza juu ya group lao la UEFA. Manager Wenger alisema, “Haina haja ya kupanic kwasababu hatujapoteza mechi lakini tumepoteza kasi ya ushindi kidogo kwenye group letu. Nadhani tuna hali nzuri kwenye timu yetu. Kwa sasa hivi tuna asilimia 90 za kumaliza nafasi ya pili na hatujapoteza mechi yoyote. Itakua mbaya kutomaliza namba moja kwenye group letu?, sijui. Kitu kinachoniumiza ni kwamba tulitakiwa kushinda mechi lakini hatujashinda “. Mechi inayofuata ya Arsenal kwenye UEFA ni dhidi ya FC Basel ambayo itafanyika 6/12/2016 kwenye uwanja wa St Jakob Park huko Basel. Mechi iliyopita Arsenal walishinda kwa magoli 2-0 kwenye uwanja wa Emirates.

Upinzani DRC waanzisha kampeni ya "Kwaheri Kabila"

Zaidi ya vyama kumi vya upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo vimeungana kuanzisha kampeni ya kumshinikiza Rais Joseph Kabila kuondoka baada ya muda wake kukamilika mnamo tarehe 20 Disemba.Kampeni hiyo iliyopewa jina la "Kwaheri Kabila" inamtaka rais huyo anayeshutumiwa kwa kuchelewesha chaguzi, kuondoka madarakani bila ya masharti yoyote na kutangaza waziwazi kuwahatong'angania madaraka.SOMA ZAIDI; http://www.dw.com/sw

FA: Sioni Faida ya Kudandia Muziki Kama Singeli Wakati Naamini Aina ya Muziki Naoufanya.

Rapa Mkongwe Hamis ‘Mwana FA’ Mwin’juma, amefunguka na kusema kuwa anaamini aina ya muziki anaoufanya haoni sababu ya kudandia dandia aina ya miziki inayo ‘Trend’ kwa sasa ikiwemo Singeli.Akiongea kupitia kipindi cha Twenzetu cha Times Fm jana, FA amedai hana mamlaka ya kumkataza msanii yeyote kufanya aina ya muziki anayoitaka lakini kwa yeye hatoweza kufanya Singeli. “Kama mtu ameamua kurap juu ya mdundo wa Singeli mi ni nani hadi nimkataze? Kulikuwa na kipindi kila anayerap anataka kuimba, sio mbaya kwenda na Trend, mimi sifikirii kufanya Singeli nauamini sana mziki wangu” Alisema FA.Katika hatua nyingine rapa huyo amedai wimbo wake mpya wa ‘Dume Suruali’ ni muendelezo wa ‘Bado nipo nipo’ kwani yule bachela asiyetaka kuoa ameoa lakini hataki kuonga.

PRESHA ZA MASHABIKI SIMBA ZATULIA TSHABALAL AONGEZA MKATABA MPYA

Hatimaye uongozi wa Simba umewashusha presha mashabiki wake baada ya kumsainisha tena beki wake Mohamed Hussein Zimbwe kutokana na kuonesha umahiri katika kikosi cha kocha Joseph Omog. Zimbwe maarufu kama Tshabalala amesaini mkataba wa miaka miwili baada ya makubaliano yaliyofanyika wiki moja na nusu iliyopita. Simba ilikubaliana na Zimbwe mbele ya baba yake mzazi na meneja wake, Herry Mzozo na leo ametia saini mbele ya Rais wa Simba, Evans Aveva. Tshabalala ambaye alishindwa kuaminiwa na Azam FC alifanya vizuri akiwa na Kagera Sugar kabla ya kusajiliwa na Simba ambapo kazi yake imeendelea kuonekana ndani ya klabu hiyo kongwe kwenye soka la Tanzania na Afrika kwa ujumla. Mkataba huo mpya kati ya Simba na Tshabalala sasa unakata kelele zote kuhusu nyota huyo kujiunga na klabu yoyote kat