Skip to main content

Posts

Showing posts from June, 2015

Ghana yazindua gari lake

Wakati unapoangazia swala la utengezaji magari mataifa ya Afrika kwa kawaida hayaorodheshwi katika swala hilo. Lakini hilo sasa huenda likabadilika kufuatia kuwasili kwa kampuni ya magari ya Ghana Kantanka ambayo hivi karibuni yataanza kuingia katika soko. Miongoni mwa magari ya kampuni hiyo ni lile la lita mbili aina ya 4 by 4 ambalo linatarajiwa kuuzwa kwa takriban pauni 14,000. Lakini je,kampuni hiyo itaweza kukabiliana na ushindani mkubwa kutoka kwa magari kama vile Toyota,Land Rover na BMW?. Kwadwo sarfo ni mwana wa mmiliki wa magari hayo. Babaake ni m'bunifu ambaye pia ni kiongozi wa dini.Hupata fedha kutokana na kilimo na uchimbaji. Magari ya Kantanka yanafananishwa na magari makubwa kama vile Toyota Prado ama MItsubishi Pajero.

Kutoka Facebook

  Jaffarai Jaffarhymes Nipo na wanangu @fidq @mwanadsm @mlelandro @djommycrazy ‪#‎ Jaffaraiscarwash‬

Msome hapa Happiness Millen :Hapata Tuzo ya kwanza ya heshima ya Global Good ya BET Awards 2015

ALIYE wai kuwa Miss Tanzania, 2001, Happiness Millen Magese anatajwa kuwa hatimaye ametunukiwa tuzo ya kwanza ya heshima ya Global Good ya BET Awards 2015. l Millen amepewa tuzo hiyo kutokana na jitihada zake za kampeni ya ugonjwa wa endometriosis ambao pia amekuwa nao katika maisha yake yote tangu awe msichana. Tatizo hilo limempelekea kuwa mgumba. Pamoja na hivyo Millen amekuwa mstari wa mbele kutoa misaada mbalimbali kwa wasiojiweza

Ally Kiba Sasa Aanza na Mbele

Kile kichupa kilicho kuwa kikisubiriwa kwa muda mrefu toka kwa Ali Kiba mfalme mwenye kiti kilichokosa mfutaji vumbi na kukikalia jumatatu anazindua video hiyo kupitia chanel ya trace na nyinginezo nchini.Huu ni mwanzo wa kujibu mashambulizi ya video kali kwenye gemu la muziki kwa sasa.

Kocha Mzungu atua Dar kunoa Chama la Msimbazi

kerr (kushoto)  Kocha mpya wa Simba, Dylan Kerr ametua leo mchana jijini Dar es salaam tayari kuanza kazi ya kuiandaa timu kwa ajili ya ligi kuu soka Tanzania bara. Kocha mpya wa Simba akiongea na waandishi Kerr, raia wa Uingereza ana uzoefu wa zaidi ya miaka 30 katika fani ya mpira wa miguu huku pia akiwa na umahiri wa kufundisha klabu mbalimbali duniani zikiwemo Hai Phong FC Vietnam, Hamilliton Academicals FC na Greennock Morton FC zote kutoka Scotland.  Kerr pia ana uzoefu wa kufundisha na kufanya kazi Afrika, ameshawahi kufanya kazi na kufundisha timu za South Africa NFD Nathi Lions FC na  South Africa Thanda Royal Zulu FC kutoka Afrika Kusini Kerr ana leseni ya daraja A na B ya ukocha aliyotunukiwa na Shirikisho la soka la Ulaya (UEFA) huku pia akiwa na uzoefu wa utawala katika fani ya michezo.

Nguli wa Hip Hop Kupata Mtoto wa Kiume

Jumba la David de Gea kupigwa bei

Jumba la vyumba sita la David de Gea lililopo Cheshire kuuzwa Mmiliki wa nyumba ya De Gea ameamua kuuza nyumba hiyo Nyumba hiyo ina vyumba sita vilivyogawanywa katika varanda nne tofauti Jikoni David de Gea anatarajiwa kurudi Hispania kwa ajili ya kuwa karibu na mpenzi wake Edurne Garcia Nyumba hiyo ina thamani ya pauni milioni 2.75 na ipo Cheshire, nje ya jiji la Manchester Tangazo la kuuzwa lipo nje ya nyumba hiyo Nyumba ina mabafu matano Moja ya bafu ya nyumba hiyo Jakuzi, kama Ramos atahamia United huenda akaishi katika nyumba hii Nyumba hiyo ina ngazi tatu

Siku ya kwanza Davido kulala kwenye nyumba yake ya Marekani

 Davido amemaliza kurekebisha nyumba yake iliyopo Atlanta, Georgia huko Marekani. Nyumba hii imeripotiwa kuwa na gharama ya pesa za Nigeria Naiea milioni 33. March mwaka 2015 Davido alisema anatafuta nyumba Marekani. Album yake mpya ‘The Baddest’ inatoka June, 2015.

LINAH AJIWEKA KWA KAKA’AKE ZARI WA DIAMOND!

Staa wa Muziki wa kizazi kipya, Estelinah Sanga ‘Linah’ akiwa ameketi na William Bugeme ‘Boss Mtoto’ ambaye ni kaka wa Zarina Hassan ‘Zari’ kiukoo. MREMBO anayefanya poa kunako Bongo Fleva, Estelinah Sanga ‘Linah’, anadaiwa ‘kujiegesha’ kimahaba kwa shemeji yake Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ aitwaye William Bugeme ‘Boss Mtoto’ ambaye ni kaka wa Zarina Hassan ‘Zari’ kiukoo. Ndani ya Ukumbi wa Triple 7 uliyopo Kawe jijini Dar hivi karibuni, paparazi wetu aliwaona wakiingia sambamba na kukaa beneti kama mtu na mpenzi wake jambo lililozua maswali kibao kutoka kwa wateja waliokuwepo ukumbini hapo. Linah na Boss Mtoto katika pozi la kimahaba.  Mbali na kunaswa siku hiyo, pia paparazi wetu amekuwa akiwashuhudia mara kadhaa wawili hao wakiwa pamoja katika kumbi mbalimbali za starehe jijini Dar. Mara ya mwisho, Linah na Boss Mtoto walikuwa pamoja kwenye hafla ya utoaji wa Tuzo za Kili Music zilizofanyika ndani ya Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar,

ZITTO AKAGUA SOKO KUU WILAYANI MASASI LILOTEKETEA KWA MOTO

Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akimsikiliza Mwenyekiti wa Soko Kuu wilayani Masasi Mkoani Mtwara, Abdallah Mandoma, lililoteketea kwa moto usiku wa kuamkia jana, mjini humo ambapo  chanzo cha moto huo kimeelezwa ni hitilafu ya umeme. Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akisaidia kuzima moto ambao uliteketeza Soko Kuu la Masasi Mkoani Mtwara, usiku wa kuamkia jana wafanyabiashara zaidi ya 1000 wamepata hassara. ………….. AJALI Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akisalimiana na askari  aliposhuka kuwapa pole abiria waliopata ajali eneo la Kata ya Mtua Kijiji cha Kilimahewa A, Mkoani Lindi jana, ambapo watu wawili walipoteza maisha. Chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa basi akijaribu kumkwepa muendesha  baskeli.  (DK) Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akizungumza na wananchi wa eneo ilipotokea ajli hiyo.inatoka http://www.mjengwablog.com

Pili Pili WAPO FITI

Bonge la picha Mkurgenzi wa Pili Pili katikati akiwa na wadau maarufu katika filamu za mapigano nchini

Makamu wa rais Burundi atoroka

Makamu wa rais Burundi anaaminika kuwa ametorokea Ubeljiji    Moja kati ya makamu wa rais wa Burundi ametoroka nchini humo baada ya kutangaza kuwa anapinga hatua ya rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu. Makamu wa pili wa Rais wa Burundi Gervais Rufikiri amekimbia baada ya kuiambia runinga ya France24 kuwa muhula huo wa tatu unakiuka sheria na katiba ya taifa hilo. Rais Nkurunziza alitibua mzozo baada ya kutangaza kuwania muhula wa tatu Msemaji wa serikali hata hivyo amekanusha madai hayo na kusema kuwa bwana Rufikiri amesafiri nje kwa ziara rasmi ya kikazi. Bwana Rufikiri amesema amekimbilia usalama wake akidai kuwa maisha yake ya

Soma Taarifa hii kuhusu TRA na Vilabu

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeviagiza vilabu vinavyoshiriki Ligi kuu ya nchini (mpira wa kulipwa) Tanzania, kuhakikisha kuwa wanalipa kodi kutokana na kuajiri makocha na wachezaji kutoka ndani na nje ya nchi. Kamshina wa TRA ameliagiza Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) kupitia kwa katibu mkuu wake kuwa, vilabu vyote vya mpira wa miguu nchini vinavyoajiri walimu, wachezaji kutoka ndani na nje ya nchi wahakikishe wanaweka kipengele cha kodi katika mikataba wanayoingia kuwaajiri. Vilbu vya vinapaswa kuwasilisha mikataba yote ya ajira ya wachezaji na walimu wao ili kukokotoa kodi stahiki kwa kila mmoja wao na mikataba yao kugongwa muhuri na stempu. Kwa mujibu wa sheria za Kodi ya Mapato ya mwaka 2004, kufungu namba 7, kila mtu anayepata mapato yatokanayo na ajira katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anawajibika kulipa kodi ya mapato kulingana na kipato chake. Aidha kwa mujibu wa Sheria ya Ushuru wa stempu ya mwaka 1973, kifungu namba 5 kikisom

Nyota katika soka waonekana wakila bata batani

Ronaldo akiwa na washikaji zake nchin Ufaransa Ronaldo akijurusha majini ili kuanza kuogelea Cristiano Ronaldo hapa alikuwa nchini Ufaransa Enrique akiwa amekaa kwenye boti Jose akionesha uso wa tabasamu na mpenzi wake Mchezaji wa klabu ya Barcelona Jose Enrique akiwa na mpenzi wake kwenye bahari ya mediterania Mchezaji wa klabu ya Aston Villa Jack alionekana pande hizi akiwa na madada wawili Kocha mkuu wa klabu ya Bayern Munich Pep Guardiola akisaini kitabu cha mwandishi wa habari wa nchini Vietnamu Pep akiwa na mke wake nchini Vietnamu

Uturuki yamnasa Etoo

Samuel Etoo Mshambuliaji wa zamani wa klabu za Everton na Chelsea Samueli Etoo amejiunga rasmi na klabu ya Uturuki, Antalyaspor kwa mkataba wa miaka 2. Hapo kabla Etoo alikuwa amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu ya Sampdoria

Inshu ya maisha ya Ngasa kwa sasa inaenda hivi

  Mshambuliaji mpya wa Free State Stars ya Afrika Kusini, Mrisho Khalfan Ngassa akiwa mbele ya gari la kutumia alilopewa na klabu yake hiyo baada ya kuwasili mjini Bethlehem leo yalipo makao makuu ya klabu hiyo ya Ligi Kuu ya nchini humo Mke wa Ngassa, Radhia Mngazija akiwa jikoni kwenye nyumba yao baada ya kuingia leo Radhia 'Nish' akiwa mlango wa nyuma wa nyumba yao mjini Bethlehem Mrisho akiwa kwenye sebule ya nyumba yake mjini Bethlehem

WANA CCM 120,335 WAMDHAMINI LOWASSA ARUSHA

Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa (wa tatu kulia) sambamba na Mkewe Mama Regina Lowassa, wakiongozana na viongizi mbali mbali wa Chama wa Mkoa wa Arusha waliofika kumpokea kwenye Uwanja wa Ndege wa KIA, wakati akitokea Mkoani Dodoma kuhudhulia vikao cha Bunge na kupigia kura bajeti kuu ya Serikali  kwa mwaka wa fedha 2015/2016. Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akimjulia hali Mjumbe wa Halmshauri Kuu ya CCM, Mathias Manga, aliyejeruhiwa kwa risasi jana usiku na watu wasiofahamika, wakati walipokutana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa KIA, Mkoani Kilimanjaro leo Juni 24, 2015.   (DK)