Skip to main content

Makamu wa rais Burundi atoroka


Makamu wa rais Burundi anaaminika kuwa ametorokea Ubeljiji 
 
Moja kati ya makamu wa rais wa Burundi ametoroka nchini humo baada ya kutangaza kuwa anapinga hatua ya rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Makamu wa pili wa Rais wa Burundi Gervais Rufikiri amekimbia baada ya kuiambia runinga ya France24 kuwa muhula huo wa tatu unakiuka sheria na katiba ya taifa hilo.
Rais Nkurunziza alitibua mzozo baada ya kutangaza kuwania muhula wa tatu
Msemaji wa serikali hata hivyo amekanusha madai hayo na kusema kuwa bwana Rufikiri amesafiri nje kwa ziara rasmi ya kikazi.
Bwana Rufikiri amesema amekimbilia usalama wake akidai kuwa maisha yake yamo hatarini.
Msemaji huyo wa serikali amesema iwapo bwana Rufikiri ametoroka Burundi ni kwa maslahi yake mwenyewe wala hakuna yeyote aliyemtishia maisha yake.
Umoja wa mataifa unaendelea na jaribio la kuwapatanisha mahasimu Burundi
Kutoroka kwake kunafwatia kutoroka kwa makamishna wa tume huru ya uchaguzi na jaji mmoja wa mahakama ya kikatiba.
Burundi imekumbwa na mzozo wa kisiasa tangu rais Nkurunziza atangaze hamu ya kuwania muhula wake wa tatu uongozini.
Wapinzani wake wanasema kuwa muhula huo wa tatu unakiuka katiba ya taifa.
Uchaguzi nchini humo umeratibiwa kufanyika Julai tarehe 15
Kwa upande wake rais Nkurunziza anashikilia kukutu kuwa kulingana na makubaliano ya kusitisha vita ya Arusha, muhula wa kwanza aliochaguliwa na viongozi na wajumbe waliowakilisha majimbo hakuchaguliwa na umma kama inavyoelezewa na katiba ya nchi hiyo.
Kufikia sasa makundi ya upinzani yamekuwa yakiandaa maandamano katika barabara za Burundi wakimshiniza rais huyo achie ngazi.
Makundi ya kuteteza haki za kibinafsi yanasema kuwa hadi kufikia sasa watu 70 wameaga dunia katika makabiliano baina ya polisi wa kupambana na fujo na waandamanaji.
Zaidi ya watu wengine 500 wamejeruhiwa katika kipindi hicho cha miezi miwili iliyopita.
Zaidi ya watu laki moja wametoroka nchini humo wakihofia fujo
Aidha zaidi ya watu laki moja wametorokea mataifa jirani kuepuka makabiliano na wengine kwa sababu ya hofu.
Mwezi uliopita jaribio la kumpindua madarakani bwana Nkurunziza lilitibuka.
Rais aliahirisha uchaguzi mkuu hadi tarehe 15 julai kufuatia shinikizo la viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki na kati.
Umoja wa mataifa unaendelea na jitihada za kuleta uwiano baina ya serikali na makundi ya upinzani.
Burundi imesema itafanya mazungumzo na wapinzani baada ya uchaguzi wa wabunge na madiwani, utakaofanyika Jumatatu ijayo.
Taarifa hii imekuja baada ya serikali kususia mazungumzo ya amani kati yake na wapinzani yanayosimamiwa na Umoja wa Mataifa, na kusisitiza kuwa uchaguzi utafanyika licha ya wapinzani na shinikizo la kimataifa.BBC

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...