Skip to main content

Makamu wa rais Burundi atoroka


Makamu wa rais Burundi anaaminika kuwa ametorokea Ubeljiji 
 
Moja kati ya makamu wa rais wa Burundi ametoroka nchini humo baada ya kutangaza kuwa anapinga hatua ya rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Makamu wa pili wa Rais wa Burundi Gervais Rufikiri amekimbia baada ya kuiambia runinga ya France24 kuwa muhula huo wa tatu unakiuka sheria na katiba ya taifa hilo.
Rais Nkurunziza alitibua mzozo baada ya kutangaza kuwania muhula wa tatu
Msemaji wa serikali hata hivyo amekanusha madai hayo na kusema kuwa bwana Rufikiri amesafiri nje kwa ziara rasmi ya kikazi.
Bwana Rufikiri amesema amekimbilia usalama wake akidai kuwa maisha yake yamo hatarini.
Msemaji huyo wa serikali amesema iwapo bwana Rufikiri ametoroka Burundi ni kwa maslahi yake mwenyewe wala hakuna yeyote aliyemtishia maisha yake.
Umoja wa mataifa unaendelea na jaribio la kuwapatanisha mahasimu Burundi
Kutoroka kwake kunafwatia kutoroka kwa makamishna wa tume huru ya uchaguzi na jaji mmoja wa mahakama ya kikatiba.
Burundi imekumbwa na mzozo wa kisiasa tangu rais Nkurunziza atangaze hamu ya kuwania muhula wake wa tatu uongozini.
Wapinzani wake wanasema kuwa muhula huo wa tatu unakiuka katiba ya taifa.
Uchaguzi nchini humo umeratibiwa kufanyika Julai tarehe 15
Kwa upande wake rais Nkurunziza anashikilia kukutu kuwa kulingana na makubaliano ya kusitisha vita ya Arusha, muhula wa kwanza aliochaguliwa na viongozi na wajumbe waliowakilisha majimbo hakuchaguliwa na umma kama inavyoelezewa na katiba ya nchi hiyo.
Kufikia sasa makundi ya upinzani yamekuwa yakiandaa maandamano katika barabara za Burundi wakimshiniza rais huyo achie ngazi.
Makundi ya kuteteza haki za kibinafsi yanasema kuwa hadi kufikia sasa watu 70 wameaga dunia katika makabiliano baina ya polisi wa kupambana na fujo na waandamanaji.
Zaidi ya watu wengine 500 wamejeruhiwa katika kipindi hicho cha miezi miwili iliyopita.
Zaidi ya watu laki moja wametoroka nchini humo wakihofia fujo
Aidha zaidi ya watu laki moja wametorokea mataifa jirani kuepuka makabiliano na wengine kwa sababu ya hofu.
Mwezi uliopita jaribio la kumpindua madarakani bwana Nkurunziza lilitibuka.
Rais aliahirisha uchaguzi mkuu hadi tarehe 15 julai kufuatia shinikizo la viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki na kati.
Umoja wa mataifa unaendelea na jitihada za kuleta uwiano baina ya serikali na makundi ya upinzani.
Burundi imesema itafanya mazungumzo na wapinzani baada ya uchaguzi wa wabunge na madiwani, utakaofanyika Jumatatu ijayo.
Taarifa hii imekuja baada ya serikali kususia mazungumzo ya amani kati yake na wapinzani yanayosimamiwa na Umoja wa Mataifa, na kusisitiza kuwa uchaguzi utafanyika licha ya wapinzani na shinikizo la kimataifa.BBC

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.