Skip to main content

Tume ya Uchaguzi ya Burundi imepanga Julai 15 kuwa tarehe mpya kwa ajili ya uchaguzi



Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza
Tume ya Uchaguzi ya Burundi imepanga Julai 15 kuwa tarehe mpya kwa ajili ya uchaguzi wa utata wa urais.
Tarehe hiyo iliyopendekezwa imekuja baada ya wito uliofanywa na viongozi wa kanda kuchelewesha uchaguzi huo, ambapo awali ulipangwa Juni 26, angalau wiki sita zimesogezwa mbele.
Burundi ilikumbwa na maandamano na mapinduzi yaliyoshindikana kumuondoa Rais Pierre Nkurunziza aliyetangaza kuwania muhula wa tatu mwezi Aprili.
Anahitaji kuthibitisha tarehe mpya kabla ya uchaguzi huo kufanyika.
Nkurunziza amekataa wito wa kutogombea tena. Pamoja na wahisani wa Magharibi kukata baadhi ya misaada kwa taifa hilo maskini Afrika.

Comments