Skip to main content

Posts

Showing posts from June, 2017

Wasanii nchini watakiwa kujisajili

KATIBU mkuu wa chama cha muziki wa kizazi kipya (TUMA) nchini,Bwana Samwel Mbwana amehimiza wasanii na vikundi vya sanaa kujisajili wao pamoja  na kazi zao kwa lengo la kulinda,kudumisha sheria na maadili yaliyopo. Kauli hiyo imesemwa jana jijini Dar es salaam mbele ya waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO. Katibu huyo alisema ni jambo nzuri kwa wasanii pamoja na vikundi vyote vya sanaa kujisajili kwenye Baraza la Sanaa la Taifa  (BASATA)  sambamba na kuzisajili kazi zao kwenye kitengo mahususi kinacholinda na kusimamia haki miliki na haki shiriki ikiwa ni nguzo ya kulinda zisipotee au kudhurumiwa. TUMA ina idadi ya wanachama wapatao 400 kimejipanga kuzunguka mikoani kwa lengo la kuhamasisha na kuelimisha wasanii kujiunga kwenye chama hicho ambapo TUMA wamejipanga kubadilisha fikra na mitazamo isiyo rasmi miongoni mwa wasanii kwa  kuwashirikisha NHIF,BASATA,COSOTA na TRA. Nae katibu mtendaji wa BASATA Bwana Godfrey Mngereza amepogeza jitihada zilizofanywa na TUM

Taarifa

Massaba: Kata yangu inahudumia shule ya Bunge

DIWANI wa Kata ya Kivukoni Mh. Henry Sato Massaba kupitia chama cha mapinduzi (CCM) amesema kuwa inahudumia  katika bajeti yake  shule moja ya msingi  Bunge. Ameita ja kuwa shule hiyo ni ya kihistoria  na kwa sasa imezeeka  na kuwa changamoto  nyingi zimejitokeza kutokana na uzee  wa shule yenyewe na pia shule ya elimu bure imechangia ongezeko la wanafunzi. Akizungumza Dar es Salaam sikuchache zilizopita  Massaba alisema  katika kikao na wananchi wa Kivukoni alisema kuwa mkutano huo unamaana ya kipekee kwa sababu kwa historia na Jiografia  ya kata hiyo  ni muda mrefu  sana  ni muda mrefu tangu kiitishwe kikao kama hicho. Alisema wananchi wa kata hiyo ni mchanganyiko wa wakazi ambao ni wafanya kazi na wafanya biashara muda mwingi  wako kwenye shughuli  mbali mbali  za kimaendele. "Nichukue  fursa hii kumpongeza Mwananchi  wetu namba moja ,Rais wetu mpendwa wa awamu ya tano Mh.John Pombe Magufuli kwa kusimamia  vye,ma sera  hiyo ya elimu bure,kwa hakika imesaidia s

Muungano wa upinzani nchini Kenya NASA waahidi mabadiliko

Email   Add new comment Vigogo wa NASA kuanzia kulia, Isaac Ruto, Kalonzo Musyoka, Raila Odinga, Musalia Mudavadi na Moses Wetangula Wanawake na vijana  nchini humo pia wameahidiwa kupewa nafasi kubwa katika serikali ya NASA na kutobaguliwa. Pamoja na hilo, vita dhidi ya ukabila, ni mojawpao ya suala ambalo Odinga amesema atalishughulikia kwa kuhakikisha kuwa nafasi ya kazi zinagawanywa kwa usawa ili kuhimiza umoja wa kitaifa. Baada ya uzinduzi wa ilani ya chama tawala Jubilee na muungano wa NASA, kampeni zinaendelea kama kawaida katika maeneo mengi ya nchi hiyo, kuelekea Uchaguzi Mkuu tarehe nane mwezi Agosti. Dokta Brian Wanyama, mchambuzi wa siasa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kibabii nchini Kenya, anasema pamoja na kuzinduliwa kwa Ilani hizo, wananchi wengi huenda wasibalishe mitazamo na maamuzi  yao kwa sababu siasa za Kenya zinaegemea ukabila na ukanda. “Itakuwa vigumu sana kwa Wakenya kubadilisha mitazamo yao kwa sababu za siasa za kikabila,” asema Wan

Saoma tetesi za chichini

Kulikuwa na tetesi za chichini kwamba huenda Anthony Martial akaondoka United na kujiunga na Arsenal lakini leo Mfaransa huyo kutumia ukurasa wake wa Twitter aliandika “Les Remuers Sont Fausses” akimaanisha “tetesi zote ni uongo.” Pierre Aubemayang inasemekana amepanga kuvitosa vilabu vya Ulaya vinavyomtaka na kusaini nchini China katika klabu ya Tianjin Quanjin ambayo inataka kumsajili Mgabon huyo kwa dau la euro mil 70. Lakininpia taarifa zinasema mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata ambaye alikuwa visiwa vya Ibiza katika Honeymoon na mkewe ameamua kukatisha Honeymoon hiyo ili kurudi mjini Madrid kujaribu kufanikisha dili lake kuhamia Manchester United. Wiki iliyopita tetesi zilisema klabu ya Juventus iko tayari kumuuza Alex Sandro kwenda Chelsea kutoka na ofa waliyotuma, lakini sasa dili hilo linaonekana kuwa gumu baada ya Manchester City nao kudaiwa kutuma ofa ya kumnunua Sandro. Raisi wa Lyon Michel Aulas ameibuka na kudai kwa sasa Arsenal wasahau kuhusu Alexandre