Skip to main content

Posts

Showing posts from November, 2011

Picha Hii ni Kuhusu Maandamano

Mmoja wa askari polisi akiwa kazini wakati Chadema walipoahirisha maandamano yao Kimara Dar es salaam sikuchache zilizopita.

Ebu Wacheki wakali wa Milazo!!

Hapa ni Dj John Charles aki shoo luv na Dj Kevin katika moja na mbili, Jumapili wiki ijayo kundi hili litapiga shoo bab ' kubwa na African Stars Band .

Utouh Apitishwa Kuwa Mjumbe Wa Bodi Ya Wakaguzi Ya Hesabu Za Umoja Wa Mataifa

  Na Mwandishi Maalum   New York Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali   kutoka   Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Ludovick    Utouh amependekezwa na kupitishwa kwa kauli Moja kuwa Mjumbe wa Bodi ya wakaguzi wa Hesabu za Umoja wa Mataifa. Bw.   Utouh   amepitishwa na   wajumbe wa Kamati ya Tano   ya Utawala na Fedha ya Baraza Kuu la 66 la Umoja wa Mataifa, katika kikao chake kilichofanyika siku ya Ijumaa,   hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, Jijini New York, Marekani. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali, Bw. Utouh   atakuwa mjumbe wa Bodi hiyo kwa kipindi cha miaka sita kuanzia Julai Mosi 2012. Bw. Ludovick Utouh anachukua nafasi   itakayoachwa wazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu kutoka Afrika ya Kusini anayemaliza muda wake mwezi Juni mwakani. Tanzania inakuwa nchi ya   tatu kutoka Afrika   kuingia katika Bodi hiyo tangu   ilipoanzishwa. Nchi nyingine kutoka Afrika   ambazo z

FFU wa Ngoma Africa band wameachia CD "Shangwe 50 Uhuru Annivesary"

Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya "Ngoma Africa band" aka FFU,yanye makao yake nchini Ujerumani,wameachia hewani CD mpya yenye nyimbo za miaka 50 ya Uhuru.Nyimbo zilizomo katika CD hiyo ni utunzi na uimbaji wake kiongozi wa bendi hiyo Kamanda Ras Makunja akiimba kwa kushirikiana na Chris-B,mpiga solo wa kikosi hiko,habari za uhakika zimetonya kuwa nyimbo hizo zimetua pia katika blog mashuuri ya Michuzi,pia vituo vya Redio vya Deutche Welle mjini Bonn,Radio VOA ya Washington, Radio Free Africa,Mwanza,vimepoke nyimbo hizo ambazo wakati wowote zinaweza kutoa burudani kwa wananchi katika shamra shamra za miaka 50 ya uhuru. Nyimbo hizo mbili     (1) Miaka 50 Uhuru(rumba) na 2. 50 Uhuru Shangwe, Zinasikia pia at www.ngoma-africa.com

Hip-Hop Culture

Alridge, Derrick P. "From Civil Rights to Hip Hop: Toward a Nexus of Ideas." Journal of African American History 90 (Summer 2005): 226-252. Aldridge, Derrick P. and James B. Stewart. "Introduction: Hip Hop in History: Past, Present, and Future." Journal of African American History 90 (Summer 2005): 190-195. Baker, Houston A., Jr. "Beyond Artifacts: Cultural Studies and the New Hybridity of Rap." In Ezell, Margaret J. M. and Katherine O'Brien O'Keefee, eds. Cultural Artifacts and the Production of Meaning: The Page, the Image, and the Body. Ann Arbor, MI: University of Michigan Press, 1994. 252 p. Baldwin, Davarian L. "Black Empires, White Desires: The Spatial Politics of Identity in the Age of Hip Hop." Black Renaissance/Renaissance Noir 2 (Summer 1999): 138-159. Bartlett, Andrew. "Airshafts, Loudspeakers, and the Hip Hop Sample: Contexts and African American Musical Aesthetics." African American Review 28 (

How to Rob an Industry…2011

by TRUTH Minista Paul Scott October 31st, 2011 @ 9:56pm “To the sellouts living it up, one way or another you’ll be givin’ it up.”   Tupac on “Holla if ya Hear Me” A decade ago, 50 Cent had the industry shook when he put out “How to Rob;” a song where he threatened to hit cats up for their jewels. In 2011, people are threatening to hit them up for their stocks and bonds. For years, snatchin’ somebody’s gold chain was seen as the ultimate diss in Hip Hop. Now, the symbolic act has taken on a political significance. Naw son, we don’t want your Jesus piece, you gotta give up that NASDAQ money! There has always been an element of class conflict within Hip Hop since the Sugarhill Gang blew up because of the commercial success of “Rapper’s Delight.” This did not sit well with hood cats such as the Cold Crush Brothers and others who felt that Sugarhill did not really rep the streets. Perhaps the closest that Hip Hop came in addressing class-i

Air Tanzania yaanza safari zake tena

Monday, 31 October 2011 18:22 Mwandishi wetu SHIRIKA la Ndege Tanzania (ATCL), leo linatarajia kuanza safari zake mikoa ya Tabora na Kigoma. Akizungumza Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Paul Chizi, alisema ndege hiyo itakuwa ikienda moja kwa moja kwenye mikoa hiyo na safari hizo zitakuwa za kila siku. “Matayarisho yote yamekamilika na ndege tunatarajia itaanza safari zake kama kawaida kuanzia kesho (leo) Novemba Mosi... tunaomba Watanzania watoe ushirikiano kwa shirika lao kwa kuchagua kusafiri na ATCL, maana ni usafiri wa moja kwa moja wa uhakika na salama,” alisema Chizi. Chizi alisema Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), tayari imelipatia shirika cheti cha kuruka kiitwacho Air Operators Certificate (AOC) baada ya kuridhishwa jinsi lilivyotekeleza masharti yake. Hivi karibuni shirika hilo lilizindua mpango wa biashara (Business Plan) ambao unaeleza jinsi lilivyojizatiti kuhakikisha linamudu ushindani wa usafiri wa anga kipindi cha miaka mit

Mwadini, Kapombe ndani, Boko, Kado njeMonday, 31 October 2011 18:43 0diggsdigg [kocha wa timu ya Taifa,Jan Poulsen] kocha wa timu ya Taifa,Jan Poulsen Sosthnes Nyoni KOCHA wa timu ya taifa, Taifa Stars, Jan Poulsen jana ametangaza rasmi kikosi chake akimuita kwa mara ya kwanza kipa, Mwadini Ally ikiwa uthibitisho sahihi wa mwitikio wa kelele za wadau wa soka nchini waliokuwa wakimpigia debe ajumuishwe. Kipa Ally, anaungana na chipukizi Shomari Kapombe katika orodha ya wachezaji wapya walioitwa na Poulsen tayari kwa mechi dhidi ya Chad. Poulsen alikuwa kwenye wakati mgumu mwanzoni mwa mwezi uliopita alipoamua kuwateua makipa Shabaan Dihile na Shabaan Kado kwenye kikosi chake wakiwa hawana namba katika klabu zao na kumwacha Mwadini ambaye amekuwa na mchango mkubwa kwa timu yake Azam msimu huu. Pia, Stars itaendelea kumkosa nahodha wake Shadrack Nsajigwa anayesumbuliwa na majeruhi yaliyomweka nje ya uwanja kwa zaidi ya wiki tatu sasa. Kikosi cha Stars itaingia kambini rasmi Novemba 3 kujiandaa na mechi ya mchujo ya kuwania kushiriki fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Chad itayofanyika Novemba 11 jijini N'Djamena. Poulsen aliwarejesha kundini beki wa kulia wa Yanga, Godfrey Taifa pamoja na mshambuliaji wa TP Mazembe, Thomas Ulimwengu. Kurejea kwa Ulimwengu katika kikosi hicho kumemfanya Mdenmark huyo kumtupia virago kinara wa ufungaji wa Ligi Kuu Tanzania mshambuliaji John Boko. Mshambuliaji huyo wa Azam ameshafunga mabao saba hadi sasa, lakini kiwango kiduni alichoonyesha kwenye mchezo wa kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika 2012 dhidi ya Morocco umesababisha kuachwa. Mbali ya Boko wengi walioachwa kwenye kikosi cha wachezaji 22 ni beki wa Simba, Victor Costa, makipa Shaaban Kado wa Yanga na Shaaban Dihile wa JKT Ruvu, kiungo Jabir Aziz wa Azam. Poulsen aliitaja sababu ya kuwaacha Nsajigwa na Costa kuwa ni kutokana na wachezaji hao kutokuwa timamu kiafya huku akisema nyota wengine amewaaacha kutokana kuporomoka viwango, ufinyu wa nafasi na wengine kukosa nafasi a kucheza kwenye timu zao. "Nimemwacha Nsajigwa na Costa kwa sababu bado hawako fiti kwa asilimia mia, lakini pia kuna suala la kuporomoka, ufinyu wa nafasi na wengine hawapati nafasi kwenye timu zao, kwa mfano Shaaban Kado ni kipa mzuri tu lakini muda mrefu hachezi,"alisema Poulsen. Akizungumzia pambano hilo,Poulsen alisema kuwa litagumu gumu kwa vile wanacheza na timu wasiyoijua na ambayo nayo inatafuta nafasi. Kikosi cha Taifa Stars ni pamoja makipa Juma Kaseja (Simba) na Mwadini Ally (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Juma Nyoso (Simba), Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya), Erasto Nyoni (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Godfrey Taita (Yanga) na Juma Jabu (Simba). Viungo:Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Nurdin Bakari (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam), Ramadhan Chombo (Azam) na Shomari Kapombe (Simba). Washambuliaji:Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada), Mrisho Ngassa (Azam), Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu(TP Mazembe, DR Congo), Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam), Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden), na Hussein Javu (Mtibwa Sugar). Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF), Boniface Wambura kikosi cha Stars kinatarajia kuondoka nchini Novemba 9 kuelekea Chad kikiwa na msafara wa watu 35 na kurejea nchini Novemba 12 siku moja baada ya mchezo.

Monday, 31 October 2011 18:43 kocha wa timu ya Taifa,Jan Poulsen Sosthnes Nyoni KOCHA wa timu ya taifa, Taifa Stars, Jan Poulsen jana ametangaza rasmi kikosi chake akimuita kwa mara ya kwanza kipa, Mwadini Ally ikiwa uthibitisho sahihi wa mwitikio wa kelele za wadau wa soka nchini waliokuwa wakimpigia debe ajumuishwe. Kipa Ally, anaungana na chipukizi Shomari Kapombe katika orodha ya wachezaji wapya walioitwa na Poulsen tayari kwa mechi dhidi ya Chad. Poulsen alikuwa kwenye wakati mgumu mwanzoni mwa mwezi uliopita alipoamua kuwateua makipa Shabaan Dihile na Shabaan Kado kwenye kikosi chake wakiwa hawana namba katika klabu zao na kumwacha Mwadini ambaye amekuwa na mchango mkubwa kwa timu yake Azam msimu huu. Pia, Stars itaendelea kumkosa nahodha wake Shadrack Nsajigwa anayesumbuliwa na majeruhi yaliyomweka nje ya uwanja kwa zaidi ya wiki tatu sasa. Kikosi cha Stars itaingia kambini rasmi Novemba 3 kujiandaa na mechi ya mchujo ya kuwania kushiriki fainali za K

NBC Na Mabenki Sita Ya Biashara Yaingia Makubaliano Na (NHC)

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof Anna Tibaijuka (katikati, nguo nyekundu), Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemiah Mchechu (wa nne kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa benki saba zilizosaini makubaliano ya ushirikiano na NHC