Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2018

Sethi :Miezi sita hajaonana na mke wake

  Na Mwandishi Wetu Aliyekuwa mmiliki wa IPTL Harbinder Singh Sethi ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa ana miezi 6 hajaonana na mke wake. Sethi ambaye yupo katika gereza la Ukonga ameyaeleza hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi baada ya Wakili wa serikali Mwanaamina Kombakono kueleza kuwa kesi ilipangwa kwa ajili ya kutajwa. Baada ya Wakili Kombakono kueleza hayo, Wakili wa Sethi, Dorah Mallaba aliieleza mahakama kuwa bado hawajapata kibali kwa ajili ya mshtakiwa Sethi kuonana na mkewe. Hata hivyo Wakili Mallaba aliiomba mahakama iruhusu hata kwa dakika 5 Sethi aonane na mkewe. “Naomba mahakama itumie busara kwa kuwa mke wake yupo hapa mahakamani, aweze kuonana naye hata kwa dakika 5,”ameomba. Wakili Kombakono baada ya kusikiliza hoja ya wakili Mallaba, alieleza kuwa kuna taratibu za kumuona mahabusu hivyo zifuatwe. Kutokana na maombi hayo Hakimu Shahidi amesema taratibu za kuwatunza mahabusu z

Agnes Kijo: Ni muhimu watoa huduma ya chakula kuzingatia sheria

Watoa huduma ya chakula kwenye mikusanyiko ya watu wametakiwa kuzingatia sheria na kanuni bora za usafi ili kuhakikisha chakula kinachoandaliwa kinakuwa salama jambo ambalo litasaidia kulinda afya ya jamii. Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa mkutano wa watoa huduma ya chakula, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Agnes Kijo,  amesema kuwa ni muhimu watoa huduma ya chakula kuzingatia sheria katika utendaji wao. Kijo amesema kuwa uandaaji wa chakula pasipo kuzingatia matakwa ya sheria na kanuni usababisha uchafuzi wa vimelea vya maradhi kwa watumiaji wa chakula hicho. Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chukula na Dawa (TFDA) Agnes Kijo akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wadau mbalimbali wanaotoa huduma ya chakula kwenye mikusanyiko ya Watu. "Kama mtoa huduma wa chakuka hajazingatia usafi anaweza akasababisha madhara ya kiafya kama vile kuhara, kuhara damu, homa ya matumbo, minyoo pamoja na kipi

China wameonesha nia ya kuwekeza kwa kujenga viwanda vya kutengeneza madawa na vifaa tiba

Makampuni matano kutoka Korea Kusini na China wameonesha nia ya kuwekeza kwa kujenga viwanda vya kutengeneza madawa na vifaa tiba. Makampuni hayo yameonesha  nia ya kuwekeza baada ya Mkurugenzi wa Mtendaji wa kituo cha Uwekezaji (TIC)Geoffrey Mwambe kwenda nchini Korea Kusini pamoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushiriki kongamano la biashara na uwekezaji liliofanyika China Agost I6 mwaka huu kwa ajili ya kuhamasisha wawekezaji. TIC katika kuwajenga wajasiriamali kimetaja kuwa uwekezaji ndio njia sahihi ya kufikia uchumi wa viwanda kwa kuzingatia hilo kimetaja kuwa ni wazi kwamba wanajukumu la kujenga sekta binafsi ambayo ni nyenzo kuu katika uwekezaji. kizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana  Mwambe alisema kuwa kupitia ziara ya kikazi aliyofanya mwezi huu nchini Korea kusini wamefanikiwa kuhamasisha wawekezaji na kuonesha nia ya kuwekeza. Alisema  kuwa akiwa korea ameshiriki kongamano la Biash

Vijana ni nguvu kazi ya Taifa hivyo wakitumiwa vizuri watakuwa msaada

SERIKALI imesema kulingana na vijana wengi duniani katika nyakati za sasa kuonekana ni tatizo katika kujihusisha na mambo ya uvunjifu wa amani imehimiza kuwapa fursa NAIBU Katibu Mkuu Wizara Elimu Sayansi na Teknolojia Dk.Ave Maria Semakafu amesema Vijana wakitumiwa vizuri wanaweza kuwa suluhisho la vitendo vya uvunjifu wa amani Barani Afrika. Dk.Ave Maria aliyasema hayo jana Dk.Ave Maria wakati wa uzinduzi wa utafiti uliofanywa na Idara ya Sayansi ya Siasa ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM),utafiti ulio hoji “Vijana kujihusisha na matukio ya kihalifu. “Vijana ni nguvu kazi ya Taifa hivyo wakitumiwa vizuri watakuwa msaada mkubwa katika kukabiliana na matukio ya uhalifu lakini wasipotumika vizuri na kuandaliwa kukua katika maadili ya kumtukuza Mungu watakuwa wakishiriki vitendo hivyo.”Alisema Dk.Ave Maria. Alisema kuwa asilimia kumekuwepo na wimbi la matukio ya kiuhalifu Barani Afrika hufanywa na Vijana kutokana kuthibitika huko Wataalamu wa tafiti kutoka UDSM wakao

Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wamlilia Monica Magufuli

  IDADI kubwa ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana walijitokeza kwenye Mazishi ya Dada wa Rais John Joseph Magufuli, Bi Monica Magufuli aliyefariki dunia asubuhi ya tarehe 19 Agosti, 2018 katika hospitali ya Bugando Jijini Mwanza alipokuwa amelazwa kwa matibabu. Wabunge na viongozi mbalimbali wakiongozwa na Marais wastaafu walianza kuingia Mkoani Geita kuanzia juzi tarehe 20 Agosti 2018 ili kuwahi mazishi hayo. Katika ibada ya mazishi iliyoongozwa na Askofu mkuu Mwandamizi Yuda Thaddeus Ruwaichi, Wabunge waliwakilishwa na Mheshimiwa Mwigulu Nchemba Mbunge wa jimbo la Iramba Mashariki pamoja na wabunge wengine wakiongozwa na Mbunge wa Manonga Seif Gulamali,  Mbunge wa Bukoba vijijini Jason Rweikaza, Mbunge wa Namanyele Ally Kessy, Medard Kalemani Mbunge na Waziri wa Nishati na Mbunge wa Karagwe Innocent Bashungwa. Aidha mazishi hayo yalihudhuriwa na kiongozi mkuu wa upinzani nchini Kenya na Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga ambaye alivutiwa na

Jeshi nchini uganda limeomba msamaha kutokana na kitendo cha askari wake kuonekana kwenye video akimpiga mwandishi

Jeshi nchini uganda limeomba msamaha kutokana na kitendo cha askari wake kuonekana kwenye video akimpiga mwandishi wa habari ambaye alikuwa akitimiza wajibu wake kwenye maandamano ya kushutumu kukamatwa kwa mbunge Bobi Wine Agosti 20 mwaka huu. Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi (CDF), Jenerali David Muhoozi, ameagiza askari waliohusika kuwapiga wanahabari  waliokuwa wakitimiza majukumu yao kukamatwa. Mbali na hatua hiyo ya jeshi hilo jumuiya ya kimataifa zimeshaanza kuwashutumu askari wa Jeshi la Ulinzi (UPDF) kwa ukatili na manyanyaso  ya waandishi wa habari ambao walikuwa wakiandika habari za kampeni katika Jimbo la Manispaa ya Arua hivi karibuni. Imeelezwa kuwa kisa cha kukamatwa kwa wanasiasa na kuibuka vurugu katika maeneo mengi ya jiji la Kampala Jumatatu. Msemaji wa UPDF Brigeduia Richard Karemire katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari amesema uongozi wa jeshi unalaani ukatili uliofanywa na as

Yanga Mtibwa Sugar leo Uwanja wa Taifa Dar es Salaam

Kikosi cha Yanga kinashuka dimbani kucheza na Mtibwa Sugar leo ukiwa ni mchezo wa kwanza kwa timu zote mbili kwa msimu wa wa 2018/19. Kuelekea mechi hiyo itakayopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili na Mashindano, Hussein Nyika, ameahidi kuwa Yanga itauwasha moto mkali. Nyika amepata jeuri hiyo baada ya kuwamaliza USM Alger kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika uliopigwa Agosti 19 ambapo waliweza kuibuka na ushindi wa mabao 2-1. Mwenyekiti huyo anaamini Yanga itaonesha maajabu zaidi ya yale waliyompatia Alger kwa kuwa wana malengo ya kurejesha kikombe chao ambacho kilikwenda kwa wekundu wa Msimbazi, Simba. Mechi hiyo itachezwa majira ya saa 12 za jioni ambapo pia itakuwa mubashara kupitia king'amuzi cha Azam TV.

JAMII SINGIDA WAASWA KUACHA MILA POTOFU

Wakazi wa Mkoa wa Singida wanaoendeleza mila potofu ya ukeketaji, wameaswa kuachana na mila hiyo, badala yake waanzishe vilabu kwa lengo la kuwafundisha wasichana umuhimu wa kufanya kazi halali na maadili mema kupunguza kasi ya mmomonyoko wa maadili.  Mwito huo ulitolewa na Dk Getrude Mughamba kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Singida wakati wa warsha iliyohudhuriwa na vikundi kazi na watendaji wa kata, wanaoshiriki utekelezaji wa mradi wa kutokomeza vitendo vya ukeketaji. Mradi huo unaotekelezwa katika kata nne za halmashauri hiyo, unaendeshwa na Shirika la Empower Society to Transform Lives (ESTL) kwa ufadhili wa Shirika la Foundation for Civil Society. Dk Mughamba alieleza kuwa kupitia vilabu hivyo, wasichana watapata fursa ya kufundishwa mapishi bora, usafi na utunzaji wa mazingira na namna bora ya kuishi na mume; hivyo kurejesha nidhamu na maadili mema ya namna ya kuishi katika jamii iliyostaarabika. Alisema

Serikali yawatahadharisha watanzania kuhusu mlipuko wa Ebola

WIZARA ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto imewatadharisha wananchi waishio mpakani mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya kongo (DRC) kuwa  makini na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola ulioripotiwa katika nchi hiyo . Akizungumza nawaandishi wa habari jijini Dar es salaam jana Waziri wa afya na maendeleo yajamii jinsia wazee nawatoto Ummy Mwalimu amesema kuwa kumekuwa namlipuko wa ugonjwa huo katika nchi ya DRC kama ilirivyoripotiwa na shilika la afya duniani WHO Katika maeneo ya kivu kasikazini katika nchi hiyo . ''Wizara inapenda kutoa tahadhari kubwa yaugonjwa huu kwa wananchi wote katika mikoa yote  hasa inayopakana na nchi ya jirani ya DRC hasa mikoa ya Mwaza ,kagera Kigoma katavi Rukwa pamoja nasongwe,"Alisema  Ummy Mwalimu . Alisema kuwa kufuatia mlipuko wa wa ugonjwa huo katika nchi ya DRC serikali kwakushirikiana na shilika la afya duniani inafanya juhudi mbalimbali katika kudhibiti  ugonjwa huo kwa kuongeza hali ya ufuatiliaji wa wasafiri wanao pita katika mipaka

Dkt. Baghayo: Wageni zaidi ya 350 kutoka mataifa zaidi ya 30 kuhudhuria mkutano wa OESAI Arusha

Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa 41 wa umoja wa kikanda wa makampuni ya bima ya nchi za Mashariki na kusini mwa Afrika (OESAI) ukiwa na lengo la  kuendeleza  vipaumbele vya kukuza soko la bima. Katika mkutano huo Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mipango anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Mkutano wa 41 wa Umoja wa Kikanda na Makampuni ya Bima ya Nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika(OESAI) unaotarajiwa kufanyika kwenye Hoteli ya Mount Meru kuanzia Agosti 27 hadi 29 mwaka huu. Pichani   kamishna wa bima wa mamlaka ya usimamizi wa shughuli za bima nchini (TIRA) Dkt. Baghayo Saqware wakati akitoa taarifa ya mkutano huo  mbele ya waandishi wa habari hawapo pichani leo. Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na   Kamishna wa  Mamlaka ya usimamizi wa shughuli za bima nchini (TIRA) Dkt. Baghayo Saqware  wakati akitoa ufafanuzi kwa wanahabari kuhusiana na mkutano huo. Amesema Mamlaka ya Usimamizi wa Bima nchini (TIRA) kwa kushirikiana na umoja huo

Dr Faustine Ndungulile:Sekta ya Afya nchini ni miongoni mwa sekta muhimu katika serikali ya Awamu ya tano

SERIKALI imesema kuwa sekta ya Afya nchini ni miongoni mwa sekta muhimu katika serikali ya Awamu ya tano na kuwa ndani ya bajeti hospitali za Wilaya 67 zimejengwa huku hospitali za Rufaa zikiboreshwa. Naibu Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile amewataka Mfuko wa taifa wa bima ya afya nchini (NHIF) kuhakikisha 2020  watanzania wote wanapata huduma ya bima ili kuweza kupata matibabu kwa urahisi na wakati sahihi. Hayo yamesemwa Dar es Salaam jana na Ndungulile alipokwenda kukabidhi cheti cha Cheti cha mfumo wa uhakiki ubora wa huduma cha kiwango cha kimataifa cha ISO ambapo NHIF imeweza kushinda. Alisema serikali bado inapigania wanachi kununua dawa akiitaja kuwa ni moja ya changamoto kuna humuhimu  wa kutoa huduma za juu iliku dhidi kushawishi wananchi kujiunga na Mfuko wa taifa wa bima ya afya nchini (NHIF). Dr Ndungulile alisema NHIF wanatakiwa kujitanua zaidi ikiwemo kujitangaza na amewasifu kwa huduma nzuri wanazozitoa k

Musa Kafana alivyo timuka CUF na Kuhamia CCM

NAIBU Meya wa Jiji la Dar es Salaam(CUF) Musa Kafana na Mwanasheria  Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu Hashim Mziray jumamosi wameng'atuka na kutangaza kujiunga na Chama cha Mapinduzi. Viongozi tayari wameendeleza wimbi la viongozi wengine waliotangaza nia zao za kujiunga na CCM wakitokea katika vyama vya upinzani nchini. Akitangaza  rasmi maamzi yake  jijini Dar es Salaam juzi  bele ya waandishi wa habari Musa Kafana alisema kuwa anaipongeza serikali ya chama cha mapinduzi CCM kwa kuendelea kuwa na ustawi mzuri katika kuendeleza mambo mbali mbali ya kijamii kwa wananchi wake. Alisema tangu achanguliwe kuwa Diwani wa Kiwalani mwaka 2015 ameshirikiana vema na serikali kuleta maendeleo katika kata hiyo. "Ukiangalia leo hii kisarawe imekuwa na maendeleo mazuri na nimekuwa nikishirikiana vema na Mkuu wa Mkuoa wa Dar es Salaam kuleta maaendeleo yanayoonekana kwa sasa,"alisema Kafana . Kafana alisema kuwa moja ya maendel

CRDB, Tawi la Temeke Jijini Dar es Salaam lawataka wananchi kuchangamkia fursa za mikopo

WAFANYABIASHARA wadogo, wakati na wakubwa  wa benki ya CRDB, Tawi la Temeke Jijini Dar es Salaam wametakiwa kuchangamkia fursa za mikopo zitolewazo katika Tawi hilo. Meneja wa CRDB Temeke, Andrew Augustine aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati, alipokuwa akifunga mafunzo ya maboresho kwa wafanyabiashara wa Manispaa ya Temeke yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Utalii Tandika jijini humo. Alisema kuwa  amewataka wafanyabiashara hao kutumia fursa hiyo yakujipatia mkopo kupitia tawi la CRDB Temeke kwa riba nafuu ya  19% na kuwahakikishia kuwa hakuna ukiritimba katika utoaji wa mikopo katika Benki hiyo inayoongoza kwakutoa huduma za kibenki nchini. “Kwa habari njema ya wafanyabiashara wadogo, wakubwa na wakati Mkurugenzi Mkuu wa CRDB Dk. Charles Kimei,  ameitdhinisha Sh Bilioni 2, kwa ajili ya kuwakopesha wafanyabiashara wa CRDB Temeke lakini mwitikio ni mdogo,"Alisema Augustine Wakati huo huo Augustine aliwatoa hofu wafanyabiashara hao kuhusu uchu

Kamati ya kudumu ya Bunge Viwanda, Biashara na Mazingira yafanya Ziara yake ya kutembelea Viwanda katika Mkoa wa Pwani

 Kamati ya kudumu ya Bunge Viwanda, Biashara na Mazingira yaendelea na Ziara yake ya kutembelea Viwanda katika Mkoa wa Pwani ili kusikiliza changamoto mbalimbali za Viwanda, Kamati leo tarehe 16 Ogasti, 2018 imetembelea kiwanda cha Bakhresa Food Products Ltd (BFPL) kiwanda kinachosindika matunda na vinywaji baridi, maji ya kunywa na juisi inayotokana na matunda yanayozalishwa nchini. Kiwanda kina uwezo wa kusindika matunda tani 330 kwa siku kwa matunda yanayotoka katika mikoa ya Pwani, Lindi, Mtwara, Tanga, Iringa, Shinyanga na Tabora. Katika Ziara hiyo kamati ya Bunge imejionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na kiwanda hicho na kupongeza uongozi wa kiwanda kwa uwekezaji mkubwa uliofanyika ambao umesaidia nchi kupata kodi pia ajira kwa watanzania. Aidha uongozi wa Kiwanda umeeleza changamoto mbalimbali wanazokutana nazo zikiwemo wingi wa taasisi za udhibiti ubora, kodi kubwa inayotozwa wakati wa uingizaji wa makasha maalumu ya kuhifandhia matunda, Stika za kodi za kielet

Soma yaliyojili baada ya Yanga kutua Dar

Mwanachama na aliyekuwa Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusuph Manji, ameshindwa kuungana na wachezaji wa klabu hiyo kwa ajili ya kujumuika nao kula mlo wa usiku baada ya kufikia kwenye hoteli ya Protea iliyopo maeneo ya Posta, jijini Dar es Salaam. Yanga iliwasili hotelini hapo ikitokea Morogoro ambako ilikwenda kuweka kambi ya wiki mbili kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger kutoka Algeria. Awali uongozi ulieleza angeweza kufika hotelini hapo kwa ajili ya kujumuika nao lakini imekuwa sivyo na haijajulikana sababu za kushindwa kuwasili kwa Manji ni zipi. Mbali na kushindwa kuwasili hotelini hapo, Manji anategemewa kuhudhuria mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika ambapo Yanga itacheza dhidi ya USM Alger majira ya saa 1 jioni leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Yanga itashuka dimbani kukipi

CRDB tawi la Temeke yatoa mafunzo ya maboresho kwa wafanyabiashara wadogo na wakati

CRDB tawi la Temeke , i meanza kutoa mafunzo ya maboresho kwa wafanyabiashara wadogo na wakati katika Manispaa ya Temeke, kwa lengo la kuwajengea uwezo ili waweze kufanya biashara zenye tija na faida zaidi. Akifungua mafunzo hayo yaliyotolewa kwa   siku tatu mfululizo na kufikia kilele chake siku ya alhamis wiki hii, Meneja wa CRDB tawi la Temeke Andrew Augastine aliwataka wafanyabiashara hao kuhudhuria kikamilifu na kuwaalika wengine kwakuwa hutolewa bure. “Wafanyabiashara wengi wanashindwa kuendelea na kukuza biashara zao, kwa sababu mbalimbali,tutawapa mafunzo yatakayo wajenga upya na kufahamu mazao ya tolewayo na Benki ya CRDB”Alisema. Lengo la mafunzo hayo nikuwajengea uwezo wafanyabiashara hao ,ili waweze kufanya biashara zinazo kidhi vigezo vya ubora na zenye kuleta faida kubwa. Hata hivyo Augastine ali waahidi wafanyabiashara hao kuwafungulia akaunti bure na baada ya mafunzo hayo watatunikiwa vyeti vitakavyo watambulisha kama wafanyabishara waliosoma biashar

Balozi wa China Wang Ke msaada wa cherehani azungumzia jinsi msaada wa cherehani zitakazo saidia wakina mama kuwainia kiuchumi

Agos Balozi wa China hapa nchini Wang Ke akizungumza na wanahabari jijini Dar es salaam. Serikali ya China imetoa msaada wa cherehani zitakazo saidia wakina mama kuwainua kiuchumi hasa katika kutekeleza dira ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa kati wa viwanda kufikia 2020. Akizungumza jijini Dar es salaam  siku chache zilizopita wakati wa hafla ya kukabidhi cherehani hizo kwa wanawake wa mikoa ya Simiyu,Mbeya na Kagera,Balozi wa China hapa nchini Wang Ke amesema kwamba msaada huo unatokana na ushirikiano mzuri wa muda mrefu kati ya Serikali yake na Tanzania. China imetoa cherehani 73 mkoani Simiyu,cherehani 40 mkoani kagera pamoja na Cherehani 80 mkoani Mbeya kwa ajili ya kuwafanya wanawake wainuke kiuchumi. Akizungumza wakati akipokea msaada huo ,Mbunge wa Busega mkoani Simiyu Dr.Raphael Chegeni amemshukuru balozi huyo nakusema kuwa uchumi wa kati wa viwanda hauwezi kufanikiwa endapo jamii kuanzia ngazi za chini haitawezeshwa,hivyo msaada huo utasaidia k