Skip to main content

Agnes Kijo: Ni muhimu watoa huduma ya chakula kuzingatia sheria

Watoa huduma ya chakula kwenye mikusanyiko ya watu wametakiwa kuzingatia sheria na kanuni bora za usafi ili kuhakikisha chakula kinachoandaliwa kinakuwa salama jambo ambalo litasaidia kulinda afya ya jamii.
Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa mkutano wa watoa huduma ya chakula, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Agnes Kijo,  amesema kuwa ni muhimu watoa huduma ya chakula kuzingatia sheria katika utendaji wao.
Kijo amesema kuwa uandaaji wa chakula pasipo kuzingatia matakwa ya sheria na kanuni usababisha uchafuzi wa vimelea vya maradhi kwa watumiaji wa chakula hicho.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chukula na Dawa (TFDA) Agnes Kijo akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wadau mbalimbali wanaotoa huduma ya chakula kwenye mikusanyiko ya Watu.

"Kama mtoa huduma wa chakuka hajazingatia usafi anaweza akasababisha madhara ya kiafya kama vile kuhara, kuhara damu, homa ya matumbo, minyoo pamoja na kipindupindu" amesema Kijo.

Amesema kuwa wakati umefika watoa huduma ya chakula wakatambua madhara yanayosababishwa na uchafuzi wa vimelea katika chakula kwani yameendelea kuwa tatizo kwa watumiaji wa chakula hicho.

Ameeleza kuwa uwepo wa magonjwa yanayotokana na kula chakula kisicho salama inatoa picha juu ya umuhimu wa kutoa kipaombele katika masuala ya usalama wa chakula.

Kijo amefafanua kuwa sasa kuna ongezeko la watu wanatoa huduma ya chakula katika mikusanyiko ikiwemo misiba, mikutano, maofisini pamoja na sherehe mbalimbali hivyo vema kila mmoja akafata sheria.

"Kupitia mkutano huu watoa huduma wa chakula watapa fursa ya kufahamu taratibu za kupata kibali pamoja na kutoa mapendekezo yao ili kuimarisha usalama wa chakula wanachoandaa" amesema Kijo.



Katika hatua nyengine amebainisha kuwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto kupitia TFDA inaendelea kushirikiana na watoa huduma ya chakula ili kulinda afya ya jamii.

Kwa upande wa watoa huduma ya Chakula kwenye mikusanyiko wemeonesha nia ya kushirikiana na TFDA katika kuboresha huduma zao kwa kuzingatia sheria.
Mkurungenzi wa Kampuni ya Love Catering Services inayotoa huduma ya chakula kwenye mikusanyiko ya watu Michael Lee, amesema kuwa ni vizuri watu wakatoa huduma ya chakula kwa kufata utaratibu.




Amesema ni jambo njema ambalo TFDA wamelifanya kwa kutukutanisha leokatika mikutano huu ambao ni rafiki kwetu katika kutoa mapendekezo yetu kwa lengo la kujenga.
Hata hivyo Lee amebainisha kuwa watanzania wanapaswa kuheshimu kazi ya kupika chakula kwani ni taaluma kama zilivyo taaluma nyengine kwani baadhi ya watu wamekuwa wakitoa huduma ya chakula pasipo kufata utaratibu.
"Wapo ambao wanasoma taaluma ya mapishi kwa muda wa miaka minne ambapo sawa na taalamu nyengine ambazo zinatumia muda wa miaka hiyo hadi kumaliza Masomo" amesema Lee.
Kwa mujibu wa taarifa za Shirika la Afya Duniani (WHO) mwaka 20I5 zinabainisha inakadiriwa watu milioni 600 kila mwaka  huugua kutokana na kula chakula kisicho salama.




Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula Mamlaka ya Chakula Na Dawa (TFDA) Justin Makisi akizungmzia madhumuni ya mkutano wa wadau wanaotoa huduma ya Chakula uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Taarifa ya WHO inaeeleza kuwa kati ya watu milioni 600 wanaougua huku 420, 000 hufariki dunia kutokana na kula chakula kisichokuwa salama.

Tatizo la chakula kisicho salama barani afrika ni kubwa, kwani watu zaidi ya milioni 9I wanakadiriwa kuugua na I37,000 hufariki kila mwaka kutokana na kula chakula kisicho salama.

Magonjwa ya kuhara uchangia asilimia asilimia 70 ya magonjwa yote yatokanayo na chakula katika bara la afrika.

Hapa Tanzania tumekuwa tukishuhudia watu wakiugua magonjwa mbalimbali kama vile homa ya matumbo (typhoid), minyoo, kuhara damu, kipindupindu huku wengine wakipoteza maisha.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.