Skip to main content

CRDB tawi la Temeke yatoa mafunzo ya maboresho kwa wafanyabiashara wadogo na wakati


CRDB tawi la Temeke , imeanza kutoa mafunzo ya maboresho kwa wafanyabiashara wadogo na wakati katika Manispaa ya Temeke, kwa lengo la kuwajengea uwezo ili waweze kufanya biashara zenye tija na faida zaidi.
Tokeo la picha la CRDB
Akifungua mafunzo hayo yaliyotolewa kwa  siku tatu mfululizo na kufikia kilele chake siku ya alhamis wiki hii, Meneja wa CRDB tawi la Temeke Andrew Augastine aliwataka wafanyabiashara hao kuhudhuria kikamilifu na kuwaalika wengine kwakuwa hutolewa bure.

“Wafanyabiashara wengi wanashindwa kuendelea na kukuza biashara zao, kwa sababu mbalimbali,tutawapa mafunzo yatakayo wajenga upya na kufahamu mazao ya tolewayo na Benki ya CRDB”Alisema.

Lengo la mafunzo hayo nikuwajengea uwezo wafanyabiashara hao ,ili waweze kufanya biashara zinazo kidhi vigezo vya ubora na zenye kuleta faida kubwa.

Hata hivyo Augastine ali waahidi wafanyabiashara hao kuwafungulia akaunti bure na baada ya mafunzo hayo watatunikiwa vyeti vitakavyo watambulisha kama wafanyabishara waliosoma biashara kwa kiasi fulani.

Naye mhamasishaji wa mafunzo hayo ambaye pia ni Meneja wa wa kitengo cha biashara ndogo na za kati Claudina William ,aliwataka washiriki kufuatilia mafunzo hayo kwa umakini ili watakapo maliza mafunzo hayo wawe wameelewa barabara.

“ Nawaombeni muwe mnafuatilia mafunzo haya kwa umakini wa hali ya juu ili mtokapo hapa muwe mmetoka na kitu kitakacho badirisha biashara zenu kutoka hapo zilipo na kupaa zaidi.”Alisema Claudina.

Mafunzo yatakayotolewa na ambayo tayari yalianza kutolewa jana ni yale ya kufahamu misingi ya uwendeshaji bora wa biashara,jinsi ya kukuza mtaji,manunuzi ,kutunza kumbukumbu, udhibiti wa mali ,na na jinsi ya kuandaa mpango wa biashara.

Comments