Skip to main content

Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wamlilia Monica Magufuli


 IDADI kubwa ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana walijitokeza kwenye Mazishi ya Dada wa Rais John Joseph Magufuli, Bi Monica Magufuli aliyefariki dunia asubuhi ya tarehe 19 Agosti, 2018 katika hospitali ya Bugando Jijini Mwanza alipokuwa amelazwa kwa matibabu.

Wabunge na viongozi mbalimbali wakiongozwa na Marais wastaafu walianza kuingia Mkoani Geita kuanzia juzi tarehe 20 Agosti 2018 ili kuwahi mazishi hayo.

Katika ibada ya mazishi iliyoongozwa na Askofu mkuu Mwandamizi Yuda Thaddeus Ruwaichi, Wabunge waliwakilishwa na Mheshimiwa Mwigulu Nchemba Mbunge wa jimbo la Iramba Mashariki pamoja na wabunge wengine wakiongozwa na Mbunge wa Manonga Seif Gulamali,  Mbunge wa Bukoba vijijini Jason Rweikaza, Mbunge wa Namanyele Ally Kessy, Medard Kalemani Mbunge na Waziri wa Nishati na Mbunge wa Karagwe Innocent Bashungwa.

Aidha mazishi hayo yalihudhuriwa na kiongozi mkuu wa upinzani nchini Kenya na Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga ambaye alivutiwa na idadi kubwa ya wabunge vijana waliofika kumzika Monica Magufuli.

Akizungumza na mwandishi wetu Mbunge wa Jimbo la Manonga, Mheshimiwa Seif Gulamali alisema: "Mwenyezi Mungu anatufundisha kuthamini zawadi ya Uhai na kuitumia vizuri, maisha ya bi. Monica yametuachia funzo kubwa la Upendo na Kujali wengine" ameeleza  Gulamali

"Kama tulivyomsikia Mheshimiwa Rais akielezea jinsi dada yake  alivyojitoa kuja kumuhudumia mama yake Bi  Suzana Magufuli ambaye ni mzee. Huu ni upendo usio kifani ambao sisi tuliobaki inatupasa kuiga" Aliongeza.

Aidha Mbunge wa Namanyele Ally Kessy aliyehudhuria msiba huo amewaasa viongozi hasa wabunge kushirikiana zaidi wakat wa misiba bila kujali itikadi zao za vyama.

Msiba huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo Marais wastaafu, Makamu wa Rais Waziri Mkuu, Wabunge na viongozi wengine wa dini na Serikali.

Mwili wa Monica Magufuli (Dada wa Rais Magufuli ) ulizikwa  hapo jana katika makaburi ya familia yaliyopo ndani ya makazi ya Rais katika Kijiji cha Mlimani, Kata ya Muungano Wilaya ya Chato mkoani Geita. Monica Magufuli ameacha Mume, Watoto tisa na wajukuu 25.
WhatsApp%2BImage%2B2018-08-22%2Bat%2B9.37.02%2BPM
Mbunge wa Manonga, Seif Gulamali  akisaini kitabu cha maombolezo cha Dada wa Rais John Joseph Magufuli, Bi Monica Magufuli aliyefariki dunia asubuhi ya tarehe 19 Agosti, 2018 katika hospitali ya Bugando Jijini Mwanza.
WhatsApp%2BImage%2B2018-08-21%2Bat%2B11.45.15%2BPM
 Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Odinga akisalimiana na Mbunge wa Manonga, Seif Gulamali

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...