Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2018

Wizara ya Afya:Yahimiza kuhamasisha na kuongeza uelewa wa jamii kuhusu humuhimu wa lishe bora kwa watoto

AZIRI wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy  Mwalimu amesema kesho Tanzania inaungangana na nchi zingine duniani kuadhimisha wiki ya unyonyeshaji wa maziwa ya mtoto. Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy  Mwalimu Akizungumza na  waandishi wa habari Dar es Salaam jana Ummy leo alisema Kila mwaka kuanzia Augosti mosi maadhimisho hayo yamekua yakifanyika na kupewa kaulimbiu maalum zinazolenga  kuhamasisha na kuongeza uelewa wa jamii kuhusu humuhimu wa lishe bora kwa watoto na taratibu sahihi za ulishaji. Alisema siku 100 za mwanzo wa uhai wa matoto ni kipindi muhimu cha kujenga msingi wa maisha ya mtoto hususani maendeleo ya ukuaji wake kimwili na kiakili. "Siku hizo mtoto huanza kuhesabiwa tangu pale mimba inapotungwa hadi mtoto anapotimiza umri wa miaka miwili nakuwa mtoto anapohitaji kunyonyeshwa anyonyeshwe wakati anapoitaji iwe usiku ama mchana,"alisema Ummy . Waziri Ummy alisema kuwa ka

Gabo Zigamba,Hashir Khalfan pamoja na Jennifer Temu wakutana na kutengeneza filamu kubwa

WADAU wa filamu nchini wameombwa kuupokea vyema ujio wa filamu ya 'Sumu' iliyoandaliwa kitaalam  ikiwa na lengo lake kuelimisha jamii . Ujio huo umeonekana kutengenezwa katika kiwango cha kimataifa na ni mojaya sinema zenye kuleta ushindani. Akizungumzia ujio huo jijini Dar es Salaam mtayarishaji mkuu wa filamu hiyo Hashir Khalfan  ‘Kalembo’ameliambia gazeti hili kuwa filamu hiyo ilionyeshwa  kwa mara ya kwanza Julay 21. mwaka huu Century Cinema, Mlimani City chini ya kampuni ya Third Eye Africa iliyoandaa uzinduzi huo. Hashir alisema umekuwa ni utambulisho wa filamu mkubwa kwani  filamu hiyo imetengenezwa Kimataifa imeonesha weledi wa hali ya juu katika utengenezaji wake lengo ikiwa kufikisha ujumbe kwa jamii husika. "Filamu ya Sumu imelenga kutoa hamasa kwa watanzania kuziona filamu za kitanzania na zile zinazotumia Lugha ya  Kiswahili pekee ili kutoa fursa  kwa vijana na jamii husika kwa ujumla kutumia njia rahisi na kurejea utamaduni

KBC Bank yaonesha mafanikio kwa wafanya biashara

Pichani  Mkurugenzi mtendaji wa benki ya KCB Cosmas Kimario. WAFANYA biashara waelezwa jinsi ya kupata mafanikio zaidi mara baada ya kupata mikopo katika mtazamo wa biashara zao. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi mtendaji wa benki ya KCB Cosmas Kimario Dar es Salaam jana katika mkunano na wafanya biashara hao,ulioitwa Biashara Club ukiwa na lengo la kuangalia changamoto wanazoku tana nazo wafanya biashara na kuweza kupata ufumbuzi.  Alisema benki hiyo imeandaa mkutano huo hili kuwakutanisha wafanya biashara wa ndani na wanje hilikuweza kukutana na kuongea mambo yao ya kibiashara ambapo imeimizwa pia wanaopata mikopo wasiiende kutumia kinyume na matakwa ya mikopo. "Wafanyabiashara wanaoweka pesa zao katika benki ya KCB tumeweza kuwakutanisha katika Biashara Club lengo ikiwa ni kuwakutanisha na kufanya mazungumzo na kuibua changa moto walizonazo na kuzizungumza hili kuleta maendeleao yenye tija,"alisema Kimario. Kimario alisema

Mng'ao Bandi waanza kusambaza kazi zao

KUNDI jipya katika muziki wa Bongoflava liitwalo 'Mng'ao Bandi',linalopatikana Jijini Dar es Salaamlimeanza kusambaza wimbo wake uitwao'Maya'ukiwa umelenga kuelimisha jamii juu ya mabinti wenye tabia mbaya kwenye mtazamo wa jamii. Hayo yamesemwa  jana na prodyza aliyehusika kutengeneza wimbo huo Jumanne Chewe ama maarufu kwa jina la Man Jay chini ya studio yake iitwayo Lady Records maeneo ya Kigogo jijini hapa. "Naamini kupitia muziki wao vijana hawa watapata mafanikio kwa kuwa jamii kwa sasa imekuwa ikiwapokea vizuri wasanii wanao ibukia  kivingine katika namna ya muziki mpya,"alisema Man Jay . Man Jay alisema kuwa kundi hilo la Mng'ao lilianza kusambaza wimbo wao huo uitwao Maya wiki iliyopita na tayari wamefanikiwa kufanya shoo ya kwanza katika mji wa Morogoro. Man Jay ametaja majina ya wasanii wengine wanao unda kundi hilo kuwa ni Frank Mzambwe pamoja na Seif Shabani ambapo alisema kuwa  wanataraji kushirikisha ny

Wizara ya Viwanda na Biashara imesema kuwepo kwa viwanda vidogo (SIDO) kutakuza wingi wa ajira

WIZARA ya Viwanda na Biashara imesema kuwa kuwepo kwa viwanda vidogo (SIDO) katika maeneo mengi nchini kutasababisha uzali shaji mkubwa wa ajira. Hayo yameelezwa jana na Naibu Waziri wa wizara ya Viwanda na Biashara Inginia Stellah Manyanya alipofanya ziara ya kushitukiza katika ofisi ya SIDO mkoa wa Dar es Salaam iliyopo eneo Vingunguti jijini Dar es Salaam. Amelitaka Shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO) kuanziasha kliniki ya viwanda na biashara katika Ofisi za shirika hilo kote nchini. Akizungumzia kuanzishwa kwa kliniki hiyo ambayo tayari Shirika hilo liliizinduwa wakati wa maonesho ya 42 ya kimataifa ya biashara yaliyofikia kilele chake hivi karibuni uwepo wake katika ofisi za SIDO  utaongeza ufanisi. “Hamna budi kuanzisha kliniki hapa SIDO na mikoani ambapo SIDO inafanya kazi kwakufanya hivyo mtakuwa mmeimarisha ubora wa bidhaa kabla ya kuingia sokoni.Alisema Ijinia Stellah. Ijinia Stellah alisema kuwepo kwa viwanda vidogo kunasababisha win

Dr Edmund Mndolwa :Wizi ama ubadhilifu wa mali za chama katika uongozi wake kwa sasa litabaki historia

MWENYEKITI  wa Jumuia ya Wazazi Tanzania wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Dr Edmund Mndolwa amesema  utekelezaji  wake katika majukumu ya uongozi suala la wizi ama ubadhilifu wa mali za chama katika uongozi wake kwa sasa litabaki historia.   Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Edmund Benard Mndolwa  Kamati  iliyoundwa na Rais Magufuli kukagua mali za chama hicho, hivi karibuni ilifanyia kazi   kwa miezi mitano  na kufanikiwa kukusanya taafa za kuhakiki na kuchambua taarifa  na nyaraka zenye maelezo kuhusu idadi, aina na hali ya mali zinazomilikiwa na kusimamiwa na chama hicho. Akizungumza Dar es Salaam mwenyekiti huyo msomi Dk.Mdolwa katika kikao cha utekelezaji cha jumuiya ya wazazi ambacho kinadaiwa  kuwa cha dharula alisema kuwa anazifahamu changamoto zilizopo na kuwa uongozi wake huko imara. "Kuhusiana na usimamizi wa mali za CCM  mali za chama zitasimamiwa barabara kwa maslahi ya chama yaye mambo ya ukosefu wa maadili au matum

zamu ya Messi na Ronaldo kumpokeza Mbappe taji

Sambaza habari hii Facebook   Sambaza habari hii Messenger Sambaza habari hii Twitter   Sambaza habari hii Ema Mshirikishe mwenzako Haki miliki ya picha EPA Beki wa zamani wa England na Manchester United Rio Ferdinand anaamini Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wanakabidhi usukani 'taji lao la mchezaji bora zaidi duniani' kwa mfungaji chipukizi wa Ufaransa Kylian Mbappe. Mbappe mwenye miaka 19 alifunga goli la nne la Ufaransa walipoichapa Croatia 4-2 fanali ya Kombe la Dunia Moscow, pamoja na kutunukiwa tuzo ya mchezaji bora mwenye umri mdogo katika michuano hiyo. "Ni mtu atakuwa akisimama kwenye jukwaa la kupokea Ballon d'Or miaka michache ijayo," alisema Rio Ferdinand, beki mstaafu wa Manchester United. "Natumai klabu yangu ya zamani (Manchester United) itamkimbiza kumsajili. Ana ushirikiano mzuri na Paul Pogba." Kylian Mbappe ahamia Paris St-Germain Kylian Mbappe ana uhusiano na Tanzania? Ufaransa washinda Kombe la Dunia kw

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa Agosti 12 mwaka huu itakuwa ni siku ya uchaguzi mdogo

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa Agosti 12 mwaka huu itakuwa ni siku ya uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Buyungu na wa madiwani katika kata 79 Tanzania Bara. Mwenyekiti wa Tume hiyo,Jaji Semistocles Kaijage ameeleza hayo hivi karibuni  jijini Dar es salaam wakati akizungumza na wajumbe wa tume hiyo pamoja na viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa nchini ambapo amesema wameshaandaa ratiba ya uchaguzi huo na wanatarajia form kuanza kuchukuliwa Julai 8 hadi 14 mwaka huu.

CCM Dar Kukutana Tamashani Viwanja leaders Club Julai 21

WAKATI tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC)Agosti 12 ikiwa imetangaza kuwa   mwaka huu itakuwa ni siku ya uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la  Buyungu na wa madiwani katika kata 79 Tanzania Bara. Jijini Dar es Slaam Katibu mwenezi wa Chama Cha MapinduziSimon  Mwakifwamba amesema jana kuwa (CCM)Mkoa wa Dar es Salaam hupo katika maandalizi ya onesho kubwa litakarofanyika kwenye viwanja vya jijini hapa. Mwakifwamba alisema kuwa hali ya maandali hayo inaendelea vizuri na  tayari onesho hilo limepangwa kufanyika Julai 21 mwaka huu katika  viwanja hivyo na kikubwa ni kuwa bendi mbali mbali pamoja na wasanii  nyota akiwemo Nguza Viking 'Babu Seya' na Papii Kocha watatumbuiza. "Lengo la siku hiyo ni kuwa wadau wote wa CCM watapata kukutana kwa pamoja na kufahamiana kwa ukaribu hali itakayofanya waweze kubadilishana mawazo kisiasa,"alisema Mwakifwamba . Mwakifwamba alisema kuwa kumekuwa na namna nyingi za kufikishiana ujumbe

Soma hapa kongamano lililo andaliwa na UONGOZI Institute

SERIKALI ya awamu ya Tano imedhamiria kwa dhati kuhakikisha kuwa hadi kufikia mwaka 2025 Tanzania inakuwa nchi ya uchumi wa kati kupitia maendeleo ya viwanda, dhamira hiyo imeelezwa inasimamiwa kwa dhati na kwa vitendo na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hivyo imesisitizwa kuwa watanzania wanapaswa kumuunga mkono na kumsaidia katika kutimiza dhamira hiyo njema kwa Taifa ambapo Tanzania imepitia hatua mbalimbali za ujenzi wa viwanda, kabla na baada ya uhuru,kila awamu katika mchakato huo ilipitia changamoto mbalimbali na kupiga hatua kwa kiasi fulani. Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam jana katika ukumbi wa MWL.Julius Nyerere  wakati wa Kongamano la “Wajibu wa Mashirika ya Umma katika Utekelezaji wa Ajenda ya Tanzania ya Viwanda” lililoandaliwa na taasisi ya UONGOZI Institute mbapo hotuba ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dkt.Philip Mpango akimwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Majaliwa Kassim Majaliwa kweny

TRA:Kuwasamehe wafanya biashara wenye malimbikizo makubwa

MAMLAKA ya Mapato nchini(TRA) imesema kuwa imewasamee  kodi wafanya biashara  wenye malimbikizo makubwa ya madeni ya kodi za nyuma yakijumuisha riba na adhabu . Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limefanya marekebisho  kupitia sheria yafedha  ya mwaka 2018 na sheria ya usimamizi wa Kodi ya  MWAKA 2015. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Kamishna Mkuu Mamlaka ya Mapato Tanzanai Charles Kichere alisema katika marekebisho  hayo Waziri mwenyedhamana  ya fedha na mipango  amepewa mamlaka ya kutoa utaratibu maalum wa kuwezesha Kamisna Mkuu kutoa msamaha riba  na adhabu  wa  hadi asilimia mia moja riba na adhabu kwenye malimbikizo ya madeni ya kodi kwa asilimia mia moja tofauti  na aslimia  moja tofauti na asilimia 50 ya hapo awali. Alisema lengo kuu la msamaha huo ni kutoa unafuu kwa walipapa kodi wenye malimbikizo ya madeni ya riba na adhabu kwa kuwapa  fursa ya kulipa malimbikizo ya madeni  ya msingi  kwa awamu  ndani ya mwaka wa fedha 2018 hadi mwakani 2019 ili k

Shirika la Posta nchini lawataka wafanyabiashara nchini kutangaza bidhaa zao kiteknolojia

WAFANYABIASHARA wa Kilimo nchini wametakiwa Shirika la Posta nchiniya Shirika la Posta nchini katika kutangaza bidhaa zao pamoja  na kuuza. Hayo yamesemwa na  Dar es Salaam jana na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi  Atashasta Nditiye  alipofungua mkutano wa 16 wa  Mashirika ya Posta yaliyopo Nchi zilizo kusini mwa Afrika (SADEC), huku  akisisitiza kwa kufanya hivyo wafanyabiashara hao wataweza kuuza bidhaa  zao Dunia nzima. ''Unajua Shirika la Posta sasa hivi, linajulikana Dunia nzima, hivyo  wafanyabiashara kama watatumia website hii watapata fulsa ya kuonekana  dunia nzima, hali itakayopelekea kupata masoko makubwa ya Kimataifa'', alisema. Alisema alisema kuwa, Shirika la Posta hivi sasa limehimarika linajiaendesha  kwa faida, hivyo lina uwezo wa kusafirisha vifurushi popote Duniani  na mzigo  wako ukafika salama na pesa yako ukaipata bila matatizo.  Naibu huyo amezitaka taasisi zote za Serikali kulitumia Shirika hi

Kesi ya Viongozi Chadema yasogezwa mbele

Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri anatarajia kutoa uamuzi katika kesi inayowakabili viongozi 9 wa Chadema, July  10,2018 kama ajitoe kusikiliza kesi hiyo ama lah. Hatua hiyo inatokana na viongozi akiwemo Mwenyekiti Freeman Mbowe kuwasilisha hoja za kutaka Hakimu huyo ajitoe kwa sababu hawana imani naye. Miongini mwa hoja ya Mbowe amedai ni adhabu tosha kwa upande wao kuripoti kituo cha Polisi cha Kati kila Ijumaa. "Kwa miezi 3 kila siku ya Ijumaa tunakwenda kuripoti hiyo ni adhabu tosha ukizingatia sisi ni viongozi wa umma,"amedai. Amedai kuwa kundi lao wote ni viongozi na wanatokea sehemu mbalimbali na wanamajukumu katika maeneo wanayitokea. Pia amedai kuwa wanakosa haki za msingi kwa sababu mawakili wao wamekuwa wakipingwa wazi wazi pindi wanapowasilisha pingamizi zao. Akifafanua zaidi, Mbowe alidai mwenendo wa hakimu wa kutokuthamini haki za msingi za watuhumiwa, kwamba aliuguliwa na kufiwa lakini hakuruhusiwa ombi la kumaliza msiba aliamriwa kurudi kusiki

TMRC: imefanikiwa kuorodheshwa hatifungani yenye thamani ya bilioni I20

Kampuni ya mikopo ya nyumba (TMRC) imefanikiwa kuorodheshwa hatifungani yenye thamani ya bilioni I20 katika soko la hisa la Dar es Salaam (DSE) jambo ambalo litasaidia kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kutumia fursa zilizopo katika sekta ya masoko katika mitaji. Akizungumza leo jijini Dar es Salaam katika hafla ya kuorodhesha hatifungani za kampuni ya TMRC soko la hisa (DSE) Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe Dkt. Ashatu Kijaji, amesema kuwa hatua ya TMRC ni mkakati wa maksudi wa kutekeleza jukumu lake la msingi la kutafuta na kukuza mtaji kwa ajili ya kuinua sekta ya mikopo ya nyumba pamoja na mitaji. "Hatifungani ya TMRC ni ya muda wa miaka mitano ambayo kitaalamu itaipatia kampuni fedha za kukopesha mabenki kwa ajili ya mikopo ya nyumba kwenye soko la fedha za ndani" amesema Dkt. Kijaji. Amesema hatua hiyo itachangia kukua kwa masoko ya mitaji hapa nchini, kwani ni wakati mwafaka sekta ya fedha kuwa imara kwa kuendelea kuchachua ukuaji wa uchumi. Dkt.