Skip to main content

Gabo Zigamba,Hashir Khalfan pamoja na Jennifer Temu wakutana na kutengeneza filamu kubwa


WADAU wa filamu nchini wameombwa kuupokea vyema ujio wa filamu ya
'Sumu' iliyoandaliwa kitaalam  ikiwa na lengo lake kuelimisha jamii .
Image result for Gabo Zigamba,
Ujio huo umeonekana kutengenezwa katika kiwango cha kimataifa na ni
mojaya sinema zenye kuleta ushindani.

Akizungumzia ujio huo jijini Dar es Salaam mtayarishaji mkuu wa filamu hiyo Hashir Khalfan
 ‘Kalembo’ameliambia gazeti hili kuwa filamu hiyo ilionyeshwa  kwa mara ya kwanza Julay 21.
mwaka huu Century Cinema, Mlimani City chini ya kampuni ya Third Eye Africa iliyoandaa uzinduzi huo.

Hashir alisema umekuwa ni utambulisho wa filamu mkubwa kwani  filamu hiyo imetengenezwa
Kimataifa imeonesha weledi wa hali ya juu katika utengenezaji wake lengo ikiwa kufikisha
ujumbe kwa jamii husika.

"Filamu ya Sumu imelenga kutoa hamasa kwa watanzania kuziona filamu
za kitanzania na zile zinazotumia Lugha ya  Kiswahili pekee ili kutoa fursa
 kwa vijana na jamii husika kwa ujumla kutumia njia rahisi na kurejea utamaduni
 wa kuangalia filamu katika majumba ya sinema (Theatre.) alisema Hashir .


Alisema baada ya kutapata hadithi ya filamu hiyo ilinichukua mudu sana kufanya
utafiti katika kupata Location sahihi kwa kazi husika,mavazi ubunifu
wa vitu mbalimbali umeifanya filamu kuwa ya kipekee na kuwa huo ni mwanzo tu
atafanya makubwa zaidi katika tasnia ya filamu

Aidha alisema kuwa  filamu hiyo imelenga ushindani katika fani ya uigizaji  inayotoa
nafasi kwa wasanii chipukizi kuonyesha uwezo katika sinema ya Sumu iliyotawaliwa na
Uhalisia kulingana na Hadithi.

Ujio huO umefanyika kwabajeti  kubwa kulingana na kila kilichotakiwa
kilitafutwa  kuanziz mavazi maalum,katika kuhakikisha sinema hiyo inaendana na
 uhalisia kwani pia ni njia mojawapo katika kuleta ushindani nje ya mipaka ya Tanzania kwa watengenezaji washindani na Bongo movie.

Pia filamu imeelezwa itatengeneza njia mpya ya usambazaji kupitia Runinga ya Azam Tv kwa malipo ya Tshs. 1,000/ (Pay per View) na baadae kampuni hiyo itaangalia njia sahihi ya usambazaji ambao kila mtu ataweza kufikiwa na huduma hiyo ili aweze kufaidi kazi bora yenye
viwango vya kimataifa.


“Filamu ya Sumu ina upekee wa aina yake kwani kuna Lugha nyingi zimetumika 
kama Lugha Mama ya Kiswahili na Kiarabu, ikiwa sambamba na kurekodiwa katika 
nchi mbalimbali kama Sudan, Tanzania na wasanii wakali ,” alisema Hashir.


Filamu ya Sumu imerekodiwa  katika nchi zifuatazo  Sudan, Mombasa,
Lamu nchini Kenya, kwa Tanzania ,sinema imererkodiwa Kisiwa cha Mafia, 
Arusha, Morogoro, Tanga na Dar es salaam.

Mkurugenzi wa Third Eye africa Hashir ameeleza kuwa katika kuzingatia
maendeleo ya tasnia ya filamu ni lazima kuwe na njia rahisi kwa mtazamaji kufikiwa
alipo, mtu ataweza kuangalia sinema ya Sumu popote alipo kwa kutumia Azamtv
 kuangalia filamu ya Sumu na kuchangia kwa gharama ndogo tu Tshs. 1,000/ na 
kuona filamu yote.

Filamu ya  Sumu imeshirikisha wasanii wengi hasa wachanga wapatao mia
moja ambao wana vipaji wakiwa na wasanii nguli Salim Ahmed (Gabo Zigamba), 
Jennifer Temu, Hashir Khalfan na kuifanya sinema kuwa bora zaidi na imeongozwa 
na Patrick Komba ambaye pia ndio mwandishi wa filamu.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...