Skip to main content

Posts

Showing posts from September, 2018

China yafungua milango ya biashara ya mazao ya kilimo nchini

CHINA imefungua milango ya biashara ya mazao ya kilimo, ambapo Tanzania  imeombwa kupeleka bidhaa za kilimo zilizoongezwa thamani. Pichani Mkurugenzi Mkuu wa  Mamlaka ya Biashara ya Maendeleo ya Biashara Tanzania(TANTRADE)Edwin Rutagenika . Katika hali hiyo zinahitajika tani 200,000 za mbaazi zilizokobolewa na zisizoko bolewa natena wakati huo, zikihitajika tani 138,000 za tangawizi zilizoongezwa thamani. Hayo yamesemwa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita wakati Mkurugenzi Mkuu wa  Mamlaka ya Biashara ya Maendeleo ya Biashara Tanzania(TANTRADE)Edwin Rutagenika  alipo rejea kutoka nchini China. “Nilikuwa nchini China hivi karibuni,China imeridhishwa na bidhaa za kilimo  ambapo zinahitajika tani nyingi za mazao mbalimbali ya kilimo,”Alisema Bidhaa za kilimo zilizooledheshwa ni pamoja na korosho,mbaazi,kahawa,  tangawizi, mhogo, choroko na kunde. Rutagenika alisema kuwa wana jukumu la kukuhakikisha bidhaa na mazao yanayozalishwa Tanzania yanapa

Anthony Joshua kupanda ulingoni tena

  re via Email Bondia aliyetajwa na Mtanzania, Hassan Mwakinyo kuwa ndiyo tageti yake katika mapambano yajayo, Amir Khan amemshauri bingwa wa Dunia wa IBF, WBA na WBO, Anthony Joshua kuhakikisha mapambano yake anafanyia Marekani ili kuwa nyota wa ulimwenguKhan amesema kuwa yeye kwa hivi sasa anafahamika ulimwengu mzima kwa sababu ya mafanikio aliyopata katika mapambano yake ya Marekani, wakati bingwa huyo wazamani wa dunia uzito wa light-welterweight akiwa amepambana zaidi ya mapambano 10 huko Las Vegas na New York Madison Square Garden. Bondia wa Tanzania, Hassan Mwakinyo Mwanamasumbwi huyo amesema King Joshua ambaye anatarajia kushuka ulingoni hapo kesho siku ya Jumamosi kutetea mkanda wake dhidi ya Alexander Povetkin kwenye uwanja wa Wembley ulimwengu mzima ungemfahamu kama angezipiga Mmarekani na kuachana na tamaduni za kupigana mapambano yake England. Bondia wa England, Anthony Joshua “Ndiyo, kama unahitaji kuwa nyota wa ulimwengu mzima ni lazima uwende ukapigan

Shirikisho la magonjwa yasio ya kuambukiza lafanya ziara mikoa ya Kanda ya Ziwa

Shirikisho la magonjwa yasio ya kuambukiza limeanza dhiara ya kutoa elimu juu ya ugonjwa huo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.  Chuo cha Walimu Shinyanga    Hayo yamesemwa jana na  Meneja Mradi wa Shirikisho hilo Happy Nchimbi,ambapo amebainisha kuwa tayari wameanza kampeni inayolengo kuvifikia vyuovya mbali mbali nchini  na shule za msingi na sekondari kuelimisha juu ya ugonjwa huo. Amesema  kuwa shinikizo la juu la damu ni kati ya magonjwa yasiyokuwa ya kuambukizwa ambapo asilimia ya wagonjwa wa ugonjwa huo haioneshi kupungua. "Tumeanza kampeni hiyo katika mikoa ya kana ya ziwa ambapo kuanzia septemba 20 na 21 tumetoa elimu juu ya magonjwa hayo kwenye Chuo cha Walimu Shinyanga na kuwa zoezi la uelimishaji limepokelewa vema,"amesema Happy. Happy alisema kuwa zoezi hilo linaendelea septemba ambapo Septemba 22 na 23 watakuwa Chuo cha Walimu Butimba mkoani mwanza. Amesema katika kuendelea na uelimishaji huo Kanda ya Ziwa Septemba 24 na 25 watakuwa Musoma Utalii Teachers a

Lukuvi :Hakuna Kampuni binafsi kuingia moja kwa moja makubaliano kuwapimia maeneo wananchi

Serikali kupitia kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi imepiga marufuku kampuni binafisi za upimaji ardhi ambazo zimekuwa zikiingia makubaliano ya upimaji ardhi za wananachi bila hata uongozi wa Wilaya husika kuwa na taarifa. Waziri wa Ardhi,William Lukuvi  Lukuvi amesema kuwa kuanzia sasa nchini kote hakuna Kampuni binafsi ya aina yoyote inaruhusiwa kwenda na kuingia moja kwa moja makubaliano na wananchi ya kuwapimia maeneo yao bila hata kutoa taarifa kwa uongozi wa Wilaya husika. Hayo yamejiri kufuatia wakazi wa baadhi ya maeneo ya Manispaa ya Tabora kuilalamikia Kampuni ya Ardhi Plan kuwachangisha fedha zao bila ya kupimia ardhi yao. Aidha, amesema haiwezekani upimaji wa ardhi za wanyonge ukageuza uchochoro wa kuwaibia na kuwadhulumu wananachi haki zao na kuongeza kuwa lazima sheria na taratibu zifuatwe katika upimaji wa ardhi za wananchi na taarifa ziwe kwa Wakuu wa Wilaya. Huku Waziri Lukuvi akiongeza kuwa Kampuni za aina hiyo zimekuwa

Kivuko cha Mv. Nyerere miili yaendelea kutambuliwa na ndugu zao

 Sehemu ya waokoaji wakiwa katika pemezoni mwa kivuko cha Mv. Nyerere kilichopinduka na kupelekea idadi kubwa ya watu kupoteza maisha na wengine kujerukiwa, katika eneo la Ukara, Kisiwa cha Ukerewe jijini Mwanza, wakiangalia maeneo mbalimbali kutafuta miili au watu waliohai waliozama kwenye maji.  ajali ya Kivuko cha MV. Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Bugorora na Ukara katika wilayani ya  Ukerewe mkoani Mwanza kilipinduka juzi Alhamisi (Septemba 20, 2018) kikikadiriwa kubeba idadi kubwa ya abiria kuzidi uwezo wake. Kwa Mujibu wa taarifa iliyotolewa na  Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isack Kamwelwe,  Mpaka wahati huu miili ya waliopolewa majini imefikia 163, huku kati yao miili 116 imetambuliwa na ndugu zao. Picha zote na Kasampaida.  Vivuko vya Mv. Clarias na Mv. Nyehunge vikiwa tayari kwa msaada wowote wa hata. Zoezi la Ukoaji likiendelea.   Baadhi ya vijana wa Skaut wakiwa wamebeba moja ya miili iliyoopolewa kwenye maji baada ya  Kivuko cha MV. Ny

Shirikisho la Vyama vya magonjwa yasiyo ya Kuambukiza nchini lataja Sababu zinazosababisha ama kuchangia mtu kupata shinikizo la juu la damu

Shinikizo la juu la damu (presha)  ni kati ya magonjwa yasiyokuwa ya kuambukizwa  asilimia ya wagonjwa  huo haioneshi kupungua tokea Shirika la Afya Duniani lilipo toa ripoti yake 2012. Shinikizo la damu inaelezwa, msukumo  wa damu unapozidi kiwango cha kawaida unaweza kusababisha madhara mwilini wataaluma wasasema nipale moyo unapopiga husukuma damu kwenye mishipa ya damu ili isambae mwilini kote. Madaktari mbali mbali ulimwengini wamekuwa wakieleza mara kwa mara juu ya shinikizo la damu ili jamii ipate kuelewa viashiria dhidi ya ugonjwa huo. Madhara ya shinikizo kubwa la damu,inaelezwa kuwa linaweza kuleta madhara mbali mbali yakiwemo:Kupasuka kwa mishipa ya damu kichwani na kusababisha kiharusiambapo kiharusi ni moja ya sababu kubwa za vifo vya watu wazima, moyo upanuka na hatimaye kushindwa kufanya kazi yake ya kusukuma damu. UELIMISHAJI NA UPIMAJI MAGONJWA YASIYOYAKUAMBUKIZA CHUO CHA WALIMU SHINYANGA Pia Kuharibika kwa mishipa ya damu kwenye figo na hatimay

Serikali yalizishwa na mradi sekta za kilimo na mifugo

SERIKALI imeridhishwa na mradi wa mapinduzi katika sekta za kilimo na mifugo baada ya mradi huo unaotekelezwa katika halmashauri nne za Mkoa wa Mwanza kuonyesha mafanikio na tija kwa wakulima na wafugaji. Akizungumza katika mahojiano na waandishi wa habari wilayani Misungwi hivi karibuni Mkurugenzi wa Sera na Mipango Ofisi ya Rais(TAMISEMI) John Cheyo alisema baada ya kukutana na wakulima walikiri kuwa mradi huo una tija. “Tulipokutana na wakulima maeneo mbalimbali ya mradi walikiri una tija na hivyo tukiuhamisha na kuupeleka katika mikoa mingine kunaweza kuwa mabadiliko makubwa zaidi kwenye kilimo. Ili kuongeza uzalishaji wakulima wanatakiwa kusaidiwa utaalamu na ushauri wa kupanda mbegu kwa nafasi na matumizi bora ya pembejeo,” alisema Cheyo. Alifafanua kuwa mradi huo unafanya kazi kwa kushirikiana na serikali ya Mkoa wa Mwanza kwenye maeneo manne kujaribu zao la alizeti huko Buchosa na Sengerema ambako lilikuwa halijaanza ili wawasaidie wakulima walime kibiashara na

Tanznaia yazikaribisha Asia na nchi za Afrika kuja kuwekeza nchini

TANZANIA imezikaribisha nchi za Bara la Asia na nchi za Afrika kuja kuwekeza nchini kutokana na rasilimali nyingi zilizopo nchini. Hayo yalisemwa jana na Balozi Hassan Yahya, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kimataifa wa mahusiano kati ya Afrika na Asia, uliofanyika jijini Dar es Salaam ambapo wataalamu kutoka nchi za bara la Asia na Afrika wemeshiriki. Ukumbi wa Nkrumah ,  Chuo Kikuu  cha Dar es Salaam “Tunazo fursa nyingi za uwekezaji hapa nchini,tumieni fursa za mkutano huu kubaini maeneo ya uwekezaji,nchi yetu ina mazingira mazuri ya uwekezaji lakini utengamano na utulivu wakisiasa ni kichocheo cha uwekezaji nchini ,”Amesema Balozi Yahya, aliuambia ujumbe wa wawashiriki wa mkutano huo kutoka mataifa mbalimbali duniani kuwa miongoni mwa maeneo watakayo wekeza ni katika,   madini, elimu, afya, kilimo,utalii,biashara na uchumi na sekta ya mawasiliano na uchukuzi. Hata hivyo Balozi Yahya aliwataka washiriki hao kuwakaribisha watanzania kuwekeza katika nchi za Asia kutok

TOKA JANUARI HADI SASA TABORA WANAWAKE 46,158 WAMEJIFUNGUA

TIGANYA VINCENT RS TABORA JUMLA ya wanawake 46,158 mkoani Tabora wamejifungua katika kipindi cha kuanzia Januari hadi kufikia Septemba mwaka huu. Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Kaimu Katibu wa Afya wa Mkoa wa Tabora Tausi Yunge wakati wa mkutano wa wadau wa faya wa Mkoa huo. Alisema walijifungua chini ya umri wa miaka 20 walikuwa 11,332 ambao ni sawa na asilimia 24.5 na wanawake wenye umri wa miaka zaidi ya ishirini waliojifungua walikuwa 34,826 sawa na asilimia 75.4. Tausi alisema watoto waliozaliwa wakiwa hai walikuwa 45,336 sawa na asilimia 98.7 na wasio hai walikuwa 563 sawa na asilimia 1.2. Kaimu Katibu Afya Mkoa huyo alisema jumla ya wanawake waliojifungulia katika vituo vya kutolea huduma walikuwa ni 43,991 sawa na asilimia 95.3. Wakati huo huo Kaimu Katibu huyo wa  Afya Mkoa amesema kuwa hadi hivi sasa ni Wazee 32,470 sawa na asilima 50 ya wazee 71,116 ya waliotambuliwa ndio wameshapewa vitambulisho kwa ajili ya matibabu mkoani humo.

Mhandisi Isack Kamwelwe akagua kipande kilichotandikwa reli ya kisasa ya SGR

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe (katikati) akikagua kipande kilichotandikwa reli ya kisasa ya SGR, Soga mkoani Pwani. Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye na kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania,Masanja Kadogosa. MRADI mkubwa wa ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge unaendelea nchini, Reli hiyo itakayoanzia bandari ya Dar es Salaam hadi mji mkuu wa Dodoma na baadaye hadi nchi za jirani za Rwanda Burundi na DR Congo umeanza kutandazwa reli katika eneo la soga mkoani Pwani. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amezindua rasmi kazi ya utandikaji wa reli ya kisasa ya SGR kwenye eneo la Soga lililopo mkoani Pwani ambapo reli hiyo inajengwa kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kwa  umbali wa kilomita 300 na  kushuhudiwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli  Tanzania Mas

Ireland yatoa Sh 2.6 bilion kukuza sekta ya kilimo nchini

KATIKA kuhakikisha sekta ya kilimo inapewa kipaumbele katika kujenga uchumi ambapo ubalozi wa Ireland umetoa msaada wa shilingi 2.6 bilion ili kuweza kukuza sekta hiyo hapa nchini. Akizungumza nawaandishiwa habari Dares Salaam mwakilishi wa (WFP) nchini Tanzania Michael Dunford alisema msaada huo unafuatiwana juhudi za ubalozi huo kwakushirikiana na mradi wa kupboresha  sektaya kilimo awamu yapili Agriculture Sector Development(ASDP11) "Mradi huo wa ASDP awammu ya pili unaelenga kukuza sekta binafsi na viwanda ili kuleta tija katika kukuza sekta ya uzalishaji na kukuza ajira,"alisema Dunford. Dunford alisema mradi huo unalenga kukuza uzalihaji wa chakula na kupeleka chakula katika meeneo ya karibu na kambi za wakimbizi kama vile Burundi,Congo pamoja na kambi zilizopo mjini Kigoma. Alisema mradi huo unawalenga wakulima takribani 6000, na kuwa utajumisha kukuza uzalishaji wa bidhaa za wakulima na kutafuta masoko. "Sambamba na mradi wa Agriculture Deve