Skip to main content

Metropolitan yawapatia ufadhiri wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya bima Chuo cha IFM

Kampuni ya Bima ya Metropolitan imewapatia ufadhiri wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya bima na udhibiti wa majanga katika Chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) kwakuwalipia ada wanafunzi watatu wa mwaka watatu wanaosoma shahada ya kwanza ya bima na udhibiti wa majanga.
Makamu Mkuu wa Chuo cha IFM Dk. Emanuel Mzava aliwataja wanafunzi hao kuwa ni Rhoda Carol, Leonard Mahimbo, na Paschalina Msofe wote wakiwa mwaka watatu.

Akizungumza katika hafla ndogo ya kuwakabidhi wanafunzi hundi ya shilingi milioni 4,500,000 iliyofanyika chuoni hapo Dk. Mzava alisema kuwa Wakala wa Bima nchini (TIBA) wamekua wakiwatafuta wadau kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wanaosoma masomo ya bima na masomo mengine.

“Tunao mkataba wa kudumu na TIBA ambapo huwasaidia wanafunzi wetu kuwaunganisha na makampuni ya bima kwakupatiwa mafunzo kwa vitendo, kupatiwa kazi pamoja na ufadhiri wa kitaaluma,”amesema.

Dk Mzava aliongeza kuwa hata ufahiri uliotolewa jana na kampuni ya Metropolitani ni matunda ya mahusiano mazuri na TIBA, IFM na Metropolitan wana mkataba wa mda mrefu wakuwasaidia wanafunzi ambapo baadhi wamenufaika na mpango huo.

Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Metropolitan Suresh Kumar, alisema tokea kuanzishwa kwa ushirikiano baina yao na IFM wanafunzi 11 wamenufaika na mpango huo na kuongeza kuwa baadhi ya wahitimu wa bima chuoni hapo wameunganishwa na makampuni ya bima.

“Hatuishii kudhamini tu,vilevile tunaajili,na tunawaunganisha na makampuni rafiki ya bima nchini lakini hatuwazuii kufanya kazi katika sekta mbalimbali, wapo wanaofanya katika sekta za fedha yakiwemo mabenki,”amesema.

Kumar aliwasisitiza wanufaika wa ufadhiri huo kusoma kwa bidii nakufanya vyema kwenye masomo yao hususani katika kipindi cha mwaka wa mwisho kwakuwa soko la ajira hulenga zaidi waliofanya vizuri katika masomo.

Rhoda Caroli akizungumza kwa niaba ya wanafunzi walionufaika na ufadhiri huo, aliuhakikisha uongozi wa IFM,TIBA na Metropolitani kuwa watasoma kwa bidii na hawata waangusha kitaaluma.

“Kwa niaba ya wenzangu ,tunashukuru kwa ufadhiri huu tunaahidi kuutendea haki na hatuta waangusha tutasoma kwa bidii ili kutimiza malengo yetu ili tuweze kutoa mchango katika sekta ya bima na nchi yetu,”amesema

Comments