Skip to main content

Shirikisho la Vyama vya magonjwa yasiyo ya Kuambukiza nchini lataja Sababu zinazosababisha ama kuchangia mtu kupata shinikizo la juu la damu

Shinikizo la juu la damu (presha)  ni kati ya magonjwa yasiyokuwa ya kuambukizwa  asilimia
ya wagonjwa  huo haioneshi kupungua tokea Shirika la Afya Duniani lilipo toa
ripoti yake 2012.
Shinikizo la damu inaelezwa, msukumo  wa damu unapozidi kiwango cha kawaida unaweza
kusababisha madhara mwilini wataaluma wasasema nipale moyo unapopiga husukuma
damu kwenye mishipa ya damu ili isambae mwilini kote.

Madaktari mbali mbali ulimwengini wamekuwa wakieleza mara kwa
mara juu ya shinikizo la damu ili jamii ipate kuelewa viashiria
dhidi ya ugonjwa huo.

Madhara ya shinikizo kubwa la damu,inaelezwa kuwa linaweza kuleta madhara mbali
mbali yakiwemo:Kupasuka kwa mishipa ya damu kichwani na kusababisha
kiharusiambapo kiharusi ni moja ya sababu kubwa za vifo vya watu
wazima, moyo upanuka na hatimaye kushindwa kufanya kazi yake ya
kusukuma damu.


UELIMISHAJI NA UPIMAJI MAGONJWA YASIYOYAKUAMBUKIZA CHUO CHA WALIMU SHINYANGA

Pia Kuharibika kwa mishipa ya damu kwenye figo na hatimaye figo kushindwa
kufanya kazi yake ya kusafirisha  damu ni moja ya madhara mengine .

Shinikizi la juu la damu  ni kati ya magonjwa yasiyokuwa ya kuambukizwa
ambapo asilimia ya wagonjwa wa ugonjwa huo haioneshi kupungua.

Hayo yalibainishwa na Mwenyekiti wa magonjwa yasiyo yakuambukizwa Profesa Andrew
Swai,wakati wa kampeni waliyoianzisha ya kupima kwa hiari magonjwa ya
kuambukizwa iliyofanyika katika viunga vya Chuo kikuu huria cha Tanzania jijini
Dar es Salaam hivi karibuni.

Mwandishi wa makala hii alitaka kufahamu zaidi nini sababu zaidi na nini kifanyike,
Profesa Swai anasema kuwa tatizo kubwa lipo katika ulaji usiofaa ,kwakuwa watu
wamekiuka misingi ya ulaji usiofaa na badala yake hujilia kwa kadri wawezavyo
hivyo ameitaka jamii kuzingatia ulaji unaofaa.

Profesa Swai anasema kuwa kwa mujibu wa takwimu za shirika la Afya duniani
za mwaka 2012 na tafiti zinazofanywa marakwamara na Shirikisho la Vyama vya Magonjwa yasiyo ya Kuambukiza, inaonesha shinikizo la juu la damu ni ugonjwa unaongoza kuliko magonjwa yote yasiyo
kuwa ya kuambukizwa.

Ripoti ya ya WHO ya 2012 inaonesha wagonjwa wanaougua plesha wanaongoza kwa
aslimia 26, sukari asilimia 9, na hata baada ya utafiti huo imeonekana ugonjwa
wa plesha umeongezeka mara tatu kuanzia 2012.


Imeelezwa kuwa watu 9 kwa kila 100 ya Watanzania wenye umri wa miaka 25
na kuendele wana ugonjwa wa kisukari,hata hivyo inatajwa kuwa kati ya
hao 9 ni wawili tu wanaojijua kuwa wanakisukari.

Profesa Swai anasema mishi mikubwa ya damu kuharibika kwa sababu ya kuvuja
kwa virutubishi vilivyo kwenye damu na kusababisha kiharusi.

Anasema ilikugundua kama unashinikizo kubwa la damu ni vyema kupima msukumo wa damu
kila unapoenda kwenye kituo cha tiba au kupima angalau mara moja kwa mwaka.

“Kwa mda mrefu tulikuwa tukielimisha ulaji unaofaa kila tunapopata fursa
yakuzungumza na watanzania lakini bado jamii haizingatii ulaji bora na salama
nakuwakumbusha umuhimu waulaji unaozingatia kiasi na si bora ulaji,”Alisema
Profesa Swai.

Hata hivyo Profesa huyo amewataka watanzania kufanya mazoezi kila siku walau
dk 30 za kuuweka mwili vizuri ili kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukizwa
kwakuwa magonjwa hayo ndiyo magonjwa yanayoongoza kwa vifo vingi barani Afrika.


Sababu  zinazosababisha ama kuchangia mtu kupata shinikizo kubwa la damu zimetajwa
kuwa ni matumizi ya chumvi kupita kiasi hasa ya kuongeza mezani,utumiaji wa pombe
kupitakiasi pamoja na utumiaji wa tumbaku na bidhaa zake pamoja na msongo wa mawazo
kutokana vitu kama vile majanga,unyanyasaji wa kijinsia huku mambo mengine yakitajwa
ni kuwa na umri mkubwa.
Moja ya visababishi vingine inatajwa kuwa ni kutojishughulisha mwili ugonjwa wa
kisukari ni moja ya kisababishi katika shinikizo la damu.

Katika makala hii pia tutadodosa  sukari mwilini hutokana na nini? ambapo Profesa Swai
amesema inatokana na vyakula pamoja na vinywaji tunavyotumia kila siku na hutumika
kuupa mwili nguvu.

Anasema ugonjwa wa sukari hutokana na kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu
kuliko inavyotakiwa,sukari ikizidi kwa muda mrefu husababisha madhara mengi
mwilini ambapo athari za ugonjwa wa kisukari, magonjwa ya moyo huwa mara mbili
zaidi ya watu wasio na kisukari,shinikizo la damu na kiharusi,kuharibika
mishipa ya damu na mishipa ya fahamu ambapo husababisha ganzi,vidonda  na
hata gangrini ya miguu na ugonjwa huo unatajwa kuwa ni sababu moja kubwa
ya watu kukatwa miguu.

Hali nyingine inatajwa ni kuharibika macho:duniani kote kisukari ni sababu
kubwa ya upofu kwa watu wazima,pia watu wanaokumbwa na tatizo la kisukari
upungua nguvu za kupambana na maambukizo:maambukizo ya fizi,ngozi,njia
ya mkojo na ukeni na kifua kikuu huwa zaidi ya mara mbili kuliko wasio
na kisukari.

Madhara mengine kwa mtu mwenye kisukari,hali ya ugonjwa wa kisukari
kwa anaye umwa inatajwa kuwa,uathiri uchumi kutokana na matibabu
ya muda mrefu :tiba ya kisukari ni ya maisha.


Ambapo maitaji ya dawa peke yake hayapungui shilingiza Tanzania
laki nne kwa mwaka kwa mgonjwa anaye hitaji nsulini.

Kwa upande wake  Meneja Mradi wa shirikisho la  Magonjwa hayo yasiyokuwa ya kuambukizwa
Happy Nchimbi,anasema kuwa lengo kubwa lakufanya kampeni hiyo chuoni hapo ni katika
kuhakikisha kuwa walimu na wanafunzi wanaosoma uwalimu wanaelewa umuhimu wakupima ma
gonjwa yasiyo yakuambukizwa ili watakapo kuwa mashuleni iwe rahisi kuwaelimisha wanafunzi
umuhimu wakupima afya zao.


Amesema Shirikisho hilo pia limeanza kwa sasa limeanza ziara ya kutoa elimu juu ya
ugonjwa huo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa

"Tumeanza kampeni hiyo katika mikoa ya kana ya ziwa ambapo
kuanzia septemba 20 na 21 tumetoa elimu juu ya magonjwa hayo
kwenye Chuo cha Walimu Shinyanga na kuwa zoezi la uelimishaji
limepokelewa vema,"amesema Happy.

Happy amesema kuwa zoezi hilo katika ukanda huo limeanza kufanyika
kuanzia Septemba mwaka huu ambapo Septemba 22 na 23 watakuwa Chuo
cha Walimu Butimba mkoani mwanza.

Amesema katika kuendelea na uelimishaji huo Kanda ya Ziwa Septemba
24 na 25 watakuwa Musoma Utalii Teachers and High School .

“Kampeni hii ina lengo la kuvifikia vyuo vya walimu  na shule za msingi na
sekondari kwakuwa serikali ina mpango wakurekebisha mitaala ya elimu nchini
nakupendekezwa magonjwa yasiyo yakuambukizwa kuingizwa katika mitaala ya elimu
nchini hivyo imetulazimu kuanza kampeni hii,”anasema Happy.

Happy aliwataka wananchi kwa ujumla kujitokeza kupima katika kampeni hiyo kwakuwa
hutolewa bure na  kampeni hiyo itaendeshwa katika mashule baada ya shule kufunguliwa.

Dunstan Mhilu ambaye ni miongoni mwa wananchi walijitokeza kupima afya kipindi kampeni hiyo
ilipofanyika Chuo Kikuu Huria Dar es Salaam,anasema kuwa
kampeni hiyo ilikuwa  nzuri na inawafaa watu wa uchumi wa chini kwakuwa hutolewa bure
lakini kikubwa amefahamu ana damu kiasi gani,plesha kiasi gani na sukari kiasi
gani na kusema kuwa atarekebisha mwenendo wake ya maisha ili asije athirika na
 moja ya magonjwa yasiyokuwa yakuambukizwa.

“Binafsi zoezi ni zuri kilichonigusa kwanza ni bure halafu ni vipimo vya uhakika
lakini nishafahamu afya yangu cha msingi nikuzingatia yale niliyoelekezwa na
Daktari,”anasema Dunstan.


Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.