Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2017

WAZIRI MHAGAMA AZITAKA HIFADHI ZA TAIFA KUTUMIA WASANII KATIKA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII

WAZIRI wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama akiwa anamsikiliza Balozi wa Mamlaka ya hifadhi Ngorongoro Mrisho Mpoto mara baada ya kuwasili katika banda hilo hivi karibuni jijini Arusha katika maadhimisho ya sikukuu ya nane nane Ofisa Utalii wa Mamlaka ya hifadhi Ngorongoro Peter Makutian aliwashukuru watanzania kuendelea kuhamasika kutembelea hifadhi hiyo tofauti na awali na kusema kuwa idadi ya wageni toka nje ya nchi wanaotembelea hifadhi hiyo kwasasa ipo sawa na watanzania. Na Pamela Mollel,Arusha WAZIRI wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama amezitaka hifadhi za taifa nchini kuendelea kuwatumia wasanii nchini katika kutangaza vivutio mbalimbali vinavyopatikana huku akiipongeza Mamlaka ya hifadhi za taifa Ngorongoro inavyotangaza vivutio vyake kupitia msanii Mrisho Mpoto. Kauli hiyo aliitoa hivi karibuni  jijini Arusha alipotembelea banda la Mamlaka ya hifadhi Ngorongoro katika maonesho ya Nanenane. Alisema kuwa

Waasi wa LRA wawateka watu 40 DR Congo

Mkuu wa LRA Joseph Kony Waasi wa kundi la LRA wamewateka takriban watu 10 na hadi 40 kutoka kijiji cha Kunu katika jimbo la kaskazini mashariki mwa DR Congo kulingana na kitengo cha habari cha AFP . Kitengo hicho kilimnukuu afisa Dungu Christophe Ikando akisema walijitambulisha kuwa wale wa LRA. ''Tunashutumu utekaji wa watu 10 kutoka kijiji cha Kunu na watu waliojihami kwa bunduki ambao walijitambulisha kuwa waasi wa LRA'' Idhaa ya redio ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa takriban watu 40 walitekwa ikiwemo maafisa wawili wa tume ya uchaguzi nchini humo. Ettiene Akangiambe ambaye ni afisa mkuu wa tume hiyo ya CENI alitibitisha habari hizo. ''Maajenti wetu wawili ambao walikuwa wakirudi kutoka katika kituo cha kusajili wapiga kura walivamiwa na watu hao waliojihami''. Amesema kuwa ajenti mmoja alifanikiwa kutoroka. Waasi wa LRA wanekuwa wakifanya operesheni zao nchini Uganda, DR Congo na Jamhuri ya Afrika ya kati CAR na Sudan kwa mion

MTANZANIA ALPHONCE SIMBU ASHIKA NAFASI YA TATU MBIO ZA DUNIA JANA

MICHEZO MTANZANIA Alphonce Felix Simbu jana amefanikiwa kushika nafasi ya tatu katika mbio za dunia za IAAF zinazoendelea kufanyika nchini Uingereza katika Jiji la London. Simbu ameshika nafasi ya tatu nyuma ya Mkenya aliyeshika nafasi ya kwanza akifuatiw ana Muethiopia aliyeshika nafasi ya pili. Akitumia masaa 2 na dakika 10 Simbu aliweza kushiuka nafasi ya tatu baada ya kumpita Mkenya mwingine aliyejua kushika nafasi ya tano. Hii inakuwa ni kwa mara ya kwanza kwa Simbu kushika nafasi ya tatu baaada ya mwaka jana katika mbio ndefu za  London Marathon aliweza kushika nafasi ya tano.

Serilikali kununua mtambo wa kutibu kansa ya mionzi wenye thamani ya Shilingi billion 14.5

SERIKALI kununua mtambo wa kutibu kansa ya mionzi wenye thamani ya Shilingi billion 14.5, hayo yamesemwa jana na Naibu waziri wa Afya Dakt Khamis Kigwangala  alipokuwa akifungua mafunzo ya kansa ya mionzi katika Taasis ya Saratani  (Ocean Road Hospital) jijini Dar es Salaam. Kigwangala amezungumza hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari mara  baada ya kufunguliwa mafunzo hayo ya wiki moja yanayofanyika nchini. “Kutokana na idadi kubwa ya wagonjwa wa saratani nchini kuzidi kuongezeka,serikali katika bajeti yake yamwaka 2017/18 imetenga kiasi hicho cha fedha katika kukabiliana na magonjwa ya kansa. Mtambo huo wenye uwezo wakugundua kila aina ya kansa ,kwasasa upo Afrika ya Kusini pekee katika bara la Afrika hivyo endapo Tanzania itanunua mtambo huo  itaokoa maisha ya watu wengi sana. Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Ocean Road Dakt Julius  Mwaiselage amesema miongoni mwa kansa inayongoza Tanzania ni ile saratani  ya mfuko wa uzazi kw

Basi la Sharon Lapinduka.....Wawili Wafariki Dunia

Basi la kampuni ya Sharon lililokuwa litatoka Dodoma kwenda Arusha, limepinduka eneo la mabanzini mjini Babati na kusababisha vifo vya watu wawili huku wengine wakijeruhiwa. Majeruhi wa ajarili hiyo wamepelekwa hospitali ya Mrara mjini Babati. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara  akizungumza juu ya ajali hiyo alisema kondakta na mtoto mdogo ndiyo walifariki.Source  http://www.mpekuzihuru.com

WAZIRI UMMY ATOA NENO KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WATOTO

Waziri  wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh.  Ummy Mwalimu  akikabidhi kadi kwa mmoja wa watoto waliojiunga na bima ya afya ya watoto (TotoAfyaCard) katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam leo kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Bima ya Taifa ya Afya  (NHIF) Spika Mstaafu Mama Anne Makinda na kushoto ni Benarld Konga Kaimu Mkurugenzi wa Mkuu wa (NHIF).  Waziri  wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh.  Ummy Mwalimu  amezindua (TotoAfyaKadi) Bima ya Afya kwa watoto. katika uzinduzi uliofanyika leo kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam aki, Kwa mujibu wa Taasisi ya Takwimu ya Taifa (NBS), kati ya Watanzania 52m waliopo sasa (2017) watoto ni 26.7m (sawa na 51%). Mtoto ni mtu mwenye umri wa chini ya miaka 18. Ummy Mwalimu anasema (TotoAfyaKadi) ni njia sahihi ya kuelekea Bima ya Afya kwa Wote nchini. Mpango huu unatoa Uhakika wa Matibabu kwa mtoto kwa Tshs 50,400/= kugharamia matibabu yake kwa mwaka mzima

Barcelona wapiga hodi Arsenal

Klabu ya Barcelona inamuona Mesut Ozil kama mrithi wa Andre Iniesta na wanaweza kujaribu kumsajili kwa £53m endapo watashindwa kumsajili Phellipe Coutinho kutoka Liverpool. Kelechi Iheanacho tayari anafanyiwa vipimo vya afya katika timu ya Leicester tayari kwa kujiunga nao, usajili wa Iheanacho umeigharimu Leicester City kiasi cha £25m na atatambulishwa rasmi ndani ya saa 24 zijazo. Wakati Iheanacho anajiunga na klabu ya Leicester City, kiungo wa Manchester City Fernando naye yuko njiani kuondoka City huku yeye akielekea nchini Uturuki kukipiga katika klabu ya Galatasaray. Kiungo wa klabu ya Everton Ross Barkley itambidi kukubali kupunguziwa kiasi cha mshahara kama yuko tayari kwenda Tottenham, Tot hawako tayari kumlipa Barkley £120,000 kwa wiki kama anavyotaka. Pamoja na Carlo Ancelotti kusisitiza Renato Sanchez hauzwi lakini kocha wa Liverpool Jurgen Klopp atajaribu kuishawishi Bayern kuwauzia kinda huyo endapo Coutinho atahamia Barcelona. Kiungo wa Manchester Unit

MSUVA MATUMAINI KIBAO MOROCCO

Kiungo mshambuliaji wa Tanzania Simon Msuva ndio ameisha tambulishwa hivyo , rasmi na klabu yake mpya Difaa Hassani El Jadidi ya Morocco baada ya kusaini mkataba wa miaka mitatu kuitumikia klabu hiyo. Msuva aliondoka nchini mwanzoni mwa wiki hiliyopita , kwenda Morocco ambako atakuwa na mtanzania mwingine Ramadhani Singano ‘Messi’, ambaye alifika Morocco mapema kuliko Msuva aliyekuwa na majukumu kwenye timu ya taifa.

MALINZI AWATAKIA HERI WAJUMBE WA MKUTANO MKUU TFF