Skip to main content

Posts

Showing posts from November, 2014

BATULI AANZA HARAKATI ZAKUOLEWA

Stori: Gladness Mallya GOOD news kwa mtoto mzuri Bongo Movies, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’ ni kwamba anatarajia kuolewa hivi karibuni baada ya kuishi maisha ya upweke kwa muda mrefu, Risasi Jumamosi linakujuza. Msanii wa Bongo Movies, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’. Batuli ambaye ni mama wa watoto wawili, ameliambia Risasi Jumamosi kuwa kwa umri alionao, amejifunza vitu vingi katika maisha hivyo kwa kuwa ameshampata mtu sahihi kwake, ameona bora aolewe. GPL(P.T) Alisema katika safari ya maisha, vikwazo ni vingi ikiwemo masuala ya skendo za wasanii lakini ameshavuka vikwazo hivyo na hahitaji tena kuyumbishwa na mtu kwani anaingia kwenye ndoa akiwa ameshajifunza mengi. “Ndoa siyo kitu cha mchezo tena kwa sisi wasanii mambo ni mengi. Kazi yetu tunakutana katika mazingira mbalimbali hatarishi na wadau tofauti, vikwazo ni vingi na mtu akivuka salama basi ni jambo la kumshukuru Mungu,” alisema Batuli. Yobnesh Yusuf ‘Batuli’ aki

Diamond na mchumba wake Zari wazua gumzo Airport…

BAADA  ya kula bata za kutosha Bongo, wakati wakisindikizana kimahaba, staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na mrembo mkali kutoka Uganda, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady, wamezua gumzo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar, Ijumaa lina mchapo kamili. Mrembo mkali kutoka Uganda, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady (mwenye gauni jekundu) akishuka kutoka gari la ‘Diamond Platnumz’. HABARI KAMILI Tukio hilo lililoshuhudiwa na wanahabari wetu lilijiri mishale ya mchana, Jumanne iliyopita katika maegesho ya airport (uwanja wa ndege) ambapo Diamond alikuwa akimsindikiza Zari aliyekuwa akitimua Bongo baada ya kufanya yao kwa siku kadhaa. KABLA YA TUKIO Awali kabla ya tukio hilo, gazeti hili lilipokea ‘ubuyu’ kutoka kwa chanzo chake cha kuaminika kwamba, wawili hao walikuwa wakijiandaa katika hoteli waliyokuwa kwa siku kadhaa iliyopo kwenye Ufukwe wa Bahari ya Hindi, tayari kuelekea uwanja wa ndege. Zari

Dewji Bilionea Namba Moja, Rostam Aziz Anamfuatia

Mfanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Dewji (39), ametajwa kuwa ndiyo bilionea namba moja nchini kwa sasa, akifuatiwa na Rostam Aziz (49). Kwa mujibu wa ripoti ya Jarida la Ventures Afrika lililotolewa jana, wafanyabiashara hao ndiyo Watanzania pekee waliongia kwenye orodha ya mabilionea 55 barani Afrika. Dewji, ambaye pia ni mbunge wa Singida Mjini kwa tiketi ya CCM, ni mfanyabishara kijana aliyekamata nafasi ya 24 katika orodha hiyo akiwa na utajiri wa Dola 2 bilioni Marekani (Sh3 trilioni). Nafasi hiyo inamfanya kijana huyo kutambulika kama tajiri namba moja nchini kwa sasa na siyo tena Rostam. Katika orodha hiyo Dewji amemwacha Rostam kwa nafasi 16. Rostam anashika nafasi ya 40 akiwa na utajiri wa Dola 1.2 bilioni za Marekani. Mwaka jana, Rostam alitajwa kuwa ndiye tajiri namba moja Tanzania. Hiyo ilikuwa kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na jarida la Marekani la Forbes. Rostam alikamata nafasi hiyo na ya 27 katika Afrika akiwa na utajiri wa Dola 1 bili

Lady Jay Dee' Afanya kichupa kipya' South Africa,Dabo Yupo,Uzinduzi Nov 28 M.O.G Bar & Restaurant.

  Shabiki wa Lady Jay Dee kaa tayari kwa wimbo na video mpya kutoka kwa msanii wako, Mpaka sasa taarifa tulizopata wimbo unatoka tarehe 24 na video itatoka tarehe 28 mwezi huu. Video itazinduliwa M.O.G Bar & Restaurant.#DressToImpress #LifeIsAToast              

Waziri ajiuzulu Ureno kupisha uchunguzi

Miguel Macedo waziri wa mambo ya ndani wa Ureno aliyejiuzulu Waziri wa mambo ya ndani wa Ureno amejiuzulu kupisha uchunguzi kuhusu tuhuma za rushwa inayohusishwa na utoaji vibali vya mgawo wa makazi. Miguel Macedo amesema hahusiki na kashfa hiyo lakini anajiuzulu kulinda heshima ya taasisi za serikali. Polisi wamewakamata watu 11, akiwemo mkuu wa idara ya uhamiaji nchini humo, siku ya Alhamisi. Ureno inatoa visa za daraja la kwanza kwa wageni wanaotaka kuwekeza nchini humo. Mnufaika mkuu wa uharakishaji wa vibali ni raia wa China ambao wamekuwa wakiwekeza kiasi kikubwa nchini Ureno. Polisi wamesema watu 11 waliokamatwa wanatuhumiwa kwa vitendo vya rushwa, fedha haramu, upendeleo na uhujumu uchumi. Visa za daraja la kwanza au kwa tafsiri isiyo rasmi "visa za dhahabu" mpango huu uko wazi kwa wageni wanaowekeza kiasi kikubwa katika majengo na ardhi. Bwana Macedo ameiambia serikali ya serikali kuwa "binafsi hahus

Matokeo ya michuano ya dimba la Afrika

Mabingwa watetezi wa kombe la Afrika Nigeria wameicharaza Congo Brazaville 2-0 siku ya jumamosi ili kuimarisha matumaini yake ya kufuzu katika dimba la Afrika mwaka 2015 huku Afrika kusini na Cameroon zikifuzu katika kinya'nganyiro hicho. Afrika kusini iliichapa Sudan 2-1 katika mechi yao ya kwanza tangu kuuawa kwa mlinda lango wake Senzo Meyiwa ili kuongoza kundi la Da. Zambia nayo iliinyamazisha Mozambique 1-0 mjini Moputo kufuzu na katika kundi Fa pamoja na viongozi wa kundi hilo Cape Verde. Burkina Faso na Gabon pia zilifuzu katika kundi Cha baada ya Kuishinda Lesotho 1-0 mjini Maseru huku Angola ikipata sare ya bila kwa bila dhidi ya wenyeji wake mjini Luanda.     Mechi ya kufuzu kwa dimba la Afrika    Siku ya Ijumaa Tunisia ilitoka sare ya bila kwa bila na Botswana na hivyobasi kufuzu katika fainali hizo. Kwengineko mabao mawili ya kipindi cha pili ya Ikechukwu Uche na Aaron Samuel dhidi

GHARAMA MPYA ZA MUHIMBILI ZASITISHWA

SERIKALI imesitisha ongezeko la tozo zilizoanza kutumika hivi karibuni katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), ambayo ndiyo yenye vifaatiba na madaktari wenye uwezo mkubwa kuliko hospitali yoyote nchini. Hatua hiyo ya Serikali, ipo katika kauli ya Serikali bungeni, iliyotolewa jana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid, ambapo pia Bohari ya Dawa (MSD) iliagizwa kupeleka dawa muhimu zenye thamani ya Sh milioni 200 katika hospitali hiyo. Hivi karibuni hospitali hiyo ilipandisha gharama za huduma hospitalini hapo, ambapo mgonjwa aliyetakiwa kulazwa baada ya kupatiwa rufaa kutibiwa katika hospitali hiyo, alipaswa kulipa Sh 5,000 kwa siku na Sh 2,000 za chakula, ambazo hazikuwepo hapo awali. Taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, , ilikaririwa na vyombo vya habari, ikieleza kuwa gharama mpya zilianza kutumika Oktoba 17, mwaka huu. Kutokana na gharama hizo, baad

GHARAMA MPYA ZA MUHIMBILI ZASITISHWA

SERIKALI imesitisha ongezeko la tozo zilizoanza kutumika hivi karibuni katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), ambayo ndiyo yenye vifaatiba na madaktari wenye uwezo mkubwa kuliko hospitali yoyote nchini. Hatua hiyo ya Serikali, ipo katika kauli ya Serikali bungeni, iliyotolewa jana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid, ambapo pia Bohari ya Dawa (MSD) iliagizwa kupeleka dawa muhimu zenye thamani ya Sh milioni 200 katika hospitali hiyo. Hivi karibuni hospitali hiyo ilipandisha gharama za huduma hospitalini hapo, ambapo mgonjwa aliyetakiwa kulazwa baada ya kupatiwa rufaa kutibiwa katika hospitali hiyo, alipaswa kulipa Sh 5,000 kwa siku na Sh 2,000 za chakula, ambazo hazikuwepo hapo awali. Taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, , ilikaririwa na vyombo vya habari, ikieleza kuwa gharama mpya zilianza kutumika Oktoba 17, mwaka huu. Kutokana na gharama hizo, baad

GHARAMA MPYA ZA MUHIMBILI ZASITISHWA

SERIKALI imesitisha ongezeko la tozo zilizoanza kutumika hivi karibuni katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), ambayo ndiyo yenye vifaatiba na madaktari wenye uwezo mkubwa kuliko hospitali yoyote nchini. Hatua hiyo ya Serikali, ipo katika kauli ya Serikali bungeni, iliyotolewa jana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid, ambapo pia Bohari ya Dawa (MSD) iliagizwa kupeleka dawa muhimu zenye thamani ya Sh milioni 200 katika hospitali hiyo. Hivi karibuni hospitali hiyo ilipandisha gharama za huduma hospitalini hapo, ambapo mgonjwa aliyetakiwa kulazwa baada ya kupatiwa rufaa kutibiwa katika hospitali hiyo, alipaswa kulipa Sh 5,000 kwa siku na Sh 2,000 za chakula, ambazo hazikuwepo hapo awali. Taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, , ilikaririwa na vyombo vya habari, ikieleza kuwa gharama mpya zilianza kutumika Oktoba 17, mwaka huu. Kutokana na gharama hizo, baad

GHARAMA MPYA ZA MUHIMBILI ZASITISHWA

SERIKALI imesitisha ongezeko la tozo zilizoanza kutumika hivi karibuni katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), ambayo ndiyo yenye vifaatiba na madaktari wenye uwezo mkubwa kuliko hospitali yoyote nchini. Hatua hiyo ya Serikali, ipo katika kauli ya Serikali bungeni, iliyotolewa jana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid, ambapo pia Bohari ya Dawa (MSD) iliagizwa kupeleka dawa muhimu zenye thamani ya Sh milioni 200 katika hospitali hiyo. Hivi karibuni hospitali hiyo ilipandisha gharama za huduma hospitalini hapo, ambapo mgonjwa aliyetakiwa kulazwa baada ya kupatiwa rufaa kutibiwa katika hospitali hiyo, alipaswa kulipa Sh 5,000 kwa siku na Sh 2,000 za chakula, ambazo hazikuwepo hapo awali. Taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, , ilikaririwa na vyombo vya habari, ikieleza kuwa gharama mpya zilianza kutumika Oktoba 17, mwaka huu. Kutokana na gharama hizo, baad

GHARAMA MPYA ZA MUHIMBILI ZASITISHWA

SERIKALI imesitisha ongezeko la tozo zilizoanza kutumika hivi karibuni katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), ambayo ndiyo yenye vifaatiba na madaktari wenye uwezo mkubwa kuliko hospitali yoyote nchini. Hatua hiyo ya Serikali, ipo katika kauli ya Serikali bungeni, iliyotolewa jana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid, ambapo pia Bohari ya Dawa (MSD) iliagizwa kupeleka dawa muhimu zenye thamani ya Sh milioni 200 katika hospitali hiyo. Hivi karibuni hospitali hiyo ilipandisha gharama za huduma hospitalini hapo, ambapo mgonjwa aliyetakiwa kulazwa baada ya kupatiwa rufaa kutibiwa katika hospitali hiyo, alipaswa kulipa Sh 5,000 kwa siku na Sh 2,000 za chakula, ambazo hazikuwepo hapo awali. Taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, , ilikaririwa na vyombo vya habari, ikieleza kuwa gharama mpya zilianza kutumika Oktoba 17, mwaka huu. Kutokana na gharama hizo, baad

Soma hapa inshu ya Ramsey

Ramsey Nouah ameoa na ana watoto watatu ila mtoto wake wa kwanza alizaa kabla ya kuoa na anaishi Marekani, mkewe anaitwa Emily na amezaa nae watoto wawili yaani Quency na Camili. Muigizaji mashuhuri wa Nollywood, Ramsey Nouah, ametekeleza alichoambiwa na mashabiki wake kwa kujiunga na masuala ya siasa. Katika mazungumzo yake na Nigeriafilms, Ramsey alisema kazi ya siasa angeweza kuikataa ila mashabiki wake wanataka awe mwanasiasa. .

Kolo na Zakora wajumuishwa kikosini

  Kolo Toure Mkufunzi wa timu ya Ivory Coast Herve Renard amewajumuisha wachezaji wa miaka mingi Kolo Toure na Didier Zakora katika kikosi chake cha mechi za kufuzu kwa dimba la bara Afrika mwaka 2015. Wawili hao hawajashiriki katika mechi za kufuzu kwa dimba hilo kufikia sasa. Timu ya Ivory Coast ni ya tatu katika kundi D huku wakitarajiwa kuchuana na Sierra Leone tarehe 14 mwezi Novemba na Cameroon siku tano baadaye. Mechi zote mbili zitachezwa mjini Abidjan kwa kuwa Sierra Leone haiwezi kuandaa mchuano wao kutokana na mzozo wa ugonjwa wa ebola nchini mwao. Hatahivyo hakuna nafasi ya mchezaji wa CSKA Moscow,Seydou Doumbia katika kikosi hicho cha wachezaji 24. Mshambuliaji huyo amefunga mabao sita katika ligi ya Urusi msimu huu ili kuisaidia timu yake kukaa katika nafasi ya pili baada ya mechi 12.BBC

USA:Mwanamke mweusi ateuliwa mwanasheria

Ikulu ya white house nchini Marekani inasema kuwa rais Brack Obama amemteua mwendesha mashtaka wa mji wa New York Loretta Lynch kuwa mkuu wa sheria nchini humo. Msemaji wa ikulu ya white house alisema kuwa mkuu huyo mpya wa sheria atateuliwa rasmi leo Jumamosi. Ikiwa uteuzi wake utaidhinishwa na bunge la seneti Loretta Lynch atakuwa mwanamke wa kwanza mwenye asili ya afrika kuwa mkuu wa sheria nchini marekani . Uteuzi huo unafanyika wiki sita baada ya kujiuzulu kwa Eric Holder ambaye ndiye M'marekani wa kwanza mweusi kuteuliwa kuwa mkuu wa sheria nchini humo. BBC (V.S)

Chelsea yaisambaratisha Liverpool 2 - 1

Mlinda mlango wa Liverpool Simon Mignolet aliingia na mpira wavuni na kuwa goli dhidi ya Chelsea Kwa mara nyingine Chelsea imeonyesha ni moto wa kuotea mbali baada ya kuifunga Liverpool 2 - 1 mbele ya mashabiki wao katika uwanja wa Anfield. Liverpool ndio waliokuwa wa kwanza kufunga goli lililotiwa wavuni na Emre Can baada ya kupiga shuti na kumgonga beki mmoja wa Chelsea na kujaa wavuni. Baadae Chelsea wakaja juu na kusawazisha goli kupitia kwa Gary Cahill baada ya mlinda mlango wa Liverpool Simon Mignolet kuingia na mpira wavuni wakati alipokuwa ameudaka. Goli la pili la Chelsea lilifungwa na Diego Costa kwa shuti kali umbali wa takribani meta 15 ndani kisanduku cha 18. Mechi hiyo ya Chelsea na Liverpool katika uwanja Anfiled kunarejesha kumbukumbu zisizofurahisha kwa upande wa Liverpool pamoja na hali yao ya baadaye ambayo si nzuri sa

Sitti Mtemvu amejivua taji lake jana

Miss Tanzania Sitti Mtemvu, amejivua taji lake jana Jiji Dar es Salaam, kwa kuuandikia barua uongozi wa uandaaji wa mashindano hayo kampuni ya Lino International Agency, baada ya uvumi uliodai kuwa alidanganya umri wa kuzaliwa kwa kupeleka cheti kisicho sahihi na kudaiwa kuwa na mtoto. Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ukumbi wa Jb Belmont, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Hashimu Lundenga, alisema kuwa uwamuzi huo umefanywa baada ya Miss huyo kuwaandikia barua ya kujivua taji hilo kwa madai kuwa analinda heshima yake. "Sitty ameamua kujivua taji hilo mwenyewe kwa madai kuwa analinda heshima yake kutokana na yale yaliyoongelewa siku mbili tatu za nyuma, na sisi hatuna budi kukubaliana na maamuzi yake kwani yeye ndiye muamuzi wa mwisho" alisema Lundenga. Lundenga, alisema kuwa katika barua hiyo Sitty amewashukuru watu wote waliokuwa pamoja nae tangu hatua za awali hadi kufikia kuchukua taji la Miss Tanzani 2014. "Sitty katika barua yake kawashukuru wale

Tiketi za elektroniki kutouzwa kwenye magari

Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea wikiendi hii ambapo tiketi za elektroniki hazitauzwa tena kwenye magari, hivyo washabiki wanunue tiketi hizo kwenye mtandao au kwenye maduka ya CRDB Fahari Huduma. Kesho (Novemba 8, 2014) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kutakuwa na mechi kati ya Yanga na Mgambo Shooting wakati Uwanja wa Chamazi kutakuwa na mechi kati ya Azam na Coastal Union. Jumapili ni mechi kati ya Simba na Ruvu Shooting. Viingilio kwenye mechi za Uwanja wa Taifa ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani na bluu, sh. 8,000 (viti vya rangi ya chungwa), sh. 15,000 (VIP B na C) wakati VIP A itakuwa sh. 20,000. Mechi za Uwanja wa Chamazi kiingilio ni sh. 3,000 kwa sh. 10,000. Mechi nyingine za VPL kesho ni kati ya Stand United na Mbeya City (Uwanja wa Kambarage, Shinyanga), Mtibwa Sugar na Kagera Sugar (Uwanja wa Manungu, Morogoro). Raundi hiyo ya saba itakamilika Jumapili

Yule Bilionea Dangote akagua ujenzi wa kiwanda chake cha saruji Mtwara

Bilionea mwenye dola nyingi kuliko wote barani Afrika, Alhaj Aliko Dangote kutoka Nigeria amefanya ziara mkoani Mtwara kukagua hatua zinazopigwa katika ujenzi wa kiwanda chake kikubwa cha saruji mjini Mtwara. Kasi ya kazi hiyo ni kubwa na kitapomalizika kitaongeza kiwango cha saruji inayozalishwa nchini kwa kiasi cha tani milioni tatu kwa mwaka. Bilionea kutoka Nigeria ambaye ni Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dangote Group of Industries, Alhaj Aliko Dangote (kulia) akiteremka kwenye ndege alipowasili Mtwara, kwenda kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda chake kikubwa cha saruji kinachojengwa mkoani humo. Msafara wa Alhaj Dangote ukipita eneo la kiwanda kukagua shughuli inavyopiga hatua. Kiwanda hicho kinatarajiwa kuchangia kukuza upatikanaji wa ajira mkoani Mtwara na kukuza uchumi. Vile vile kupunguza gharama za upatikanaji wa saruji maeneo ya kusini mwa Tanzania na nchi jirani.

Kutoka Facebook Profesa Jay akifungua matawi mapya ya Chadema

Jana kupitia ukurasa wake wa Facebook Profesa Jay aliweka picha zikimuonyesha akifungua matawi mapya ya Chadema na kuandika haya ” JANA; Kufungua matawi mapya na kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwenye daftari la makazi na kisha kuitumia vema HAKI yao ya kupiga KURA na kuwachagua viongozi wao kwa maendeleo yao! !! Hamasisha na watu wako ili wajitambue na kujiandikisha! !! ”

Rais Uhuru Kenyata wa kenya atumia Daladala kwenda Ofisini

Rais uhuru Kenyata ameendelea kujizolea umaarufu mkubwa nchini Kenya kutokana na matukio mengi anayoyafanya, mengi yakiwa yale ambay ni mara chache sana kumuona rais akifanya. Mfano ni kama lile tukio la kutoka ikulu akiwa hana bila ya walinzi, kucheza mziki katika matamasha mbalimbali na lile la kusimamisha msafara wake kisa tu anunue karanga. Jipya alilolifanya siku ya jana ni pale alipoamua kutumia usafiri wa Matatu au kwetu tunaita Daladala kwenda mjini. Inasemekana Rais Kenyata ndio rais wa kwanza ktumia usafiri huo akiwa madarakani, marais wote waliopita hawajawahi kuutumia wakiwa madarakani. Kikubwa kingine alichosema na kimeungwa mkono na vijana wengi ni kuruhusu Daladala kuchorwa Graffit jambo ambalo limekua likizuiliwa na uongozi nchini humo kwa mda sasa. Rais Kenyata alisema ” To be frank why are we interfering with graffiti on Matatu? Let us promote our young people – Uhuru Kenyatta ”

Kanda ya Ziwa yang’ara matokeo darasa la saba

  Esther Mbussi na Adam Mkwepu, Dar es Salaam SHULE za msingi katika mikoa ya Kanda ya Ziwa zimeongoza matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka 2014 kwa kushika namba moja hadi saba kati ya shule 10 bora kitaifa. Aidha, watahiniwa wamefaulu zaidi somo la Kiswahili na kufeli zaidi somo la Hisabati. Katika matokeo hayo yaliyotangazwa jana na Baraza la Mitihani la Taifa (NACTE), wavulana wameongoza somo la Hisabati kwa kupata alama 50/50, ambapo 26 wamefaulu kwa kiwango hicho na wasichana wakiwa wanane. Akitangaza matokeo hayo, Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde, alizitaja shule 10 bora kuwa ni Twibhoki ya Mara ambayo imeshika nafasi ya kwanza, Mugini iliyoshika nafasi ya pili, Peace land na Alliance zote za Mwanza, Kwema (Shinyanga), St. Severine (Kagera), Rocken Hill (Shinyanga), Tusiime (Dar es Salaam), Imani (Kilimanjaro) na Palikas (Shinyanga). "Kwa upande wa m

Marekani kubadili sera dhidi ya Iran?

Marekani imepinga madai ya taifa hilo kwamba imebadili sera zake dhidi ya Iran kutokana na ripoti za magazeti na kuwa Rais Obama amekuwa na mawasiliano ya siri na viongozi wa juu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei. Jarida la The Wall Street Journal lilitoa taarifa kwamba mwezi uliopita kuwa Rais Obama alituma barua kwa Khamenei iliyobeba malengo ya pamoja katika kupigana na kundi la wapiganaji wa kiislam la IS. Rais Obama Msemaji wa Ikulu ya Marekani White House Josh Earnest amepuuzakukanusha ama kukubali madai ya ripoti hiyo dhidi ya Marekani kwamba sasa mlengo wake kwa Iran unalegezwa na muungano wa kuungana pamoja kuwapiga kundi la IS. Iran na mataifa mengine yenye nguvu Duniani ikiwemo Marekani yamekuwa yakijadiliana dhidi ya mpango wa Iran na Nyuklia.

Utawala wa raia kurejea Burkina Faso?

Kiongozi wa Burkina Faso Isaac Zida Rais wa Ghana,Nigeria na Senegal wanatarajiwa kuwasili nchini Burkina Faso hii leo kwa ajili ya kutoa msukumo kwa Jeshi la nchi hiyo lirudishe utawala wa kiraia. Kiongozi wa mpito Luteni Kanali Isaac Zida amesema jeshi litaachia madaraka ndani ya majuma mawili,muda uliopangwa na Umoja wa Afrika. Zida ameahidi kuanzisha serikali ya Umoja ili kuepuka vikwazo ambavyo vinaweza kutolewa dhidi yao. Jeshi lilichukua madaraka baada ya kutokea machafuko na maandamano yaliyoshinikiza kujiuzulu kwa Rais Blaise Compaore.BBC

Sudani Kusini kukumbwa na vikwazo

Marekani imesema itapeleka rasimu ya maazimio ndani ya Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuweka vikwazo dhidi ya Watu wanaozorotesha hali ya kisiasa nchini Sudani Kusini. Rais wa Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa ambaye ni Rais wa Australia amesema baadhi ya wanachama wa baraza hilo wanaunga mkono hatua ya kuwekewa vikwazo na kuzuia biashara ya silaha. Haijajulikana ni lini hatua hiyo itatekelezwa. Mapigano yameendelea nchini Sudani Kusini ,ingawa kumekuwa na jitihada za kimataifa kuhakikisha makubaliano ya amani yanatekelezeka. Mzozo wa kuwania madaraka uliokuwepo kwa miezi kumi kati ya Rais Salva Kiir na aliyekuwa Makamu wake Riek Machar umegharimu maisha ya maelfu ya Watu na takriban watu milioni mbili kuyakimbia makazi yao. Makubaliano ya amani yaliyotiwa saini yalishindwa, kwa kuwa pande zinazokinzana zilishindwa kuunda Serikali ya umoja.BBC