Skip to main content

GHARAMA MPYA ZA MUHIMBILI ZASITISHWA


SERIKALI imesitisha ongezeko la tozo zilizoanza kutumika hivi karibuni katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), ambayo ndiyo yenye vifaatiba na madaktari wenye uwezo mkubwa kuliko hospitali yoyote nchini.
Hatua hiyo ya Serikali, ipo katika kauli ya Serikali bungeni, iliyotolewa jana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid, ambapo pia Bohari ya Dawa (MSD) iliagizwa kupeleka dawa muhimu zenye thamani ya Sh milioni 200 katika hospitali hiyo.
Hivi karibuni hospitali hiyo ilipandisha gharama za huduma hospitalini hapo, ambapo mgonjwa aliyetakiwa kulazwa baada ya kupatiwa rufaa kutibiwa katika hospitali hiyo, alipaswa kulipa Sh 5,000 kwa siku na Sh 2,000 za chakula, ambazo hazikuwepo hapo awali.
Taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, , ilikaririwa na vyombo vya habari, ikieleza kuwa gharama mpya zilianza kutumika Oktoba 17, mwaka huu.
Kutokana na gharama hizo, baadhi ya wahudumu hospitalini hapo walikaririwa wakisema idadi ya wagonjwa imepungua wodini kutokana na wengi wao kushindwa kumudu gharama.
Wagonjwa kutoka mikoani waliathirika zaidi, kwa kulazimika kutafuta malazi nje ya hospitali hiyo, hata kama hali zao ni mbaya.
Aidha, baadhi ya wananchi waliokuwa wakiuguza ndugu zao, walikaririwa kuchukua uamuzi wa kuwarejesha nyumbani ili kukwepa gharama hizo.
Miundombinu
Mbali na kusitisha ongezeko hilo la tozo, Dk Seif pia ameagiza uongozi wa hospitali hiyo kurekebisha mara moja mazingira na miundombinu ya hospitali hiyo, ambayo yapo ndani ya uwezo wao.
Ingawa tamko hilo halikufafanua, lakini taarifa zinaonesha kuwa hospitali hiyo ilikuwa ikizidiwa na wagonjwa, kiasi cha baadhi kulazimika kulala sakafuni.
Vyombo vya habari viliripoti kuhusu hali ya usafi wa vyoo vya wodi ya Sewa Haji kuwa mbaya, licha ya kuwapo taarifa za kutolewa kwa zabuni kwa kampuni kadhaa kufanya usafi, unaokidhi viwango na kanuni za afya bora.
Baadhi ya vyoo havikuwa na maji na vifaa vya kusukuma maji havikuwa vikifanya kazi, huku baadhi ya mabomba yakiwa na kutu.
Kutokana na ukosefu wa maji, wagonjwa na watu wanaowatembelea, alilazimika kutumia maji yaliyopo kwenye mapipa nje ya vyoo na yalipokosekana, walitafuta mahali kwingine ikiwamo nje ya jengo hilo.
Baadhi ya vyombo vya habari, viliripoti kushuhudia baadhi ya vyoo vikiwa vimejaa uchafu katika majengo ya Sewa Haji, Kibasila na Mwaisela huku vingi vikiwa katika hali mbaya ya uchakavu, kutokana na kutumika muda mrefu bila kufanyiwa ukarabati.
Deni MSD
Kuhusu deni la Bohari Kuu ya Dawa (MSD), Dk Rashid alisema Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha ilifanya uhakiki wa deni la MSD la Sh bilioni 41.5.
Baada ya deni hilo kuhakikiwa, alisema Serikali ilianza kulipa kwa awamu ambapo Sh bilioni 8 zililipwa Juni 14, Sh bilioni 2 Agosti na Sh bilioni 20 zimelipwa mwezi huu. Alisema kiasi kilichobaki cha Sh bilioni 11.5, kitalipwa mwezi ujao.
Kuhusu kutenga fedha za kununua dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi kupitia MSD ili kuhakikisha jamii ya Watanzania inapata dawa na vifaa tiba kwa wakati, alisema katika mwaka wa fedha wa 2014/2015, Bunge liliidhinisha Sh bilioni 70.5 kwa ajili ya kazi hiyo. Ocean Road Akizungumzia huduma za afya katika Hospitali ya Ocean Road, alisema huduma za matibabu ya saratani inaendelea kutolewa,
kutokana na mashine ya E80 kuendelea kufanya kazi na kwa sasa ndiyo inayotibu wagonjwa wote wa saratani katika taasisi hiyo.
"Kutokana na kuwepo kwa mashine moja tu ya mionzi inayofanya kazi, kwa sasa hivi mashine inafanya kazi kwa saa 18 kwa siku ili kupunguza mlundikano wa wagonjwa.
"Mashine ya intra cavitary ambayo ilikuwa imesimama kufanya kazi kutokana na ubovu na kukosekana kwa vifaa muhimu, imetengenezwa na sasa imeanza kufanya kazi hivyo kuwezesha matibabu ya wagonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi kwa ufanisi zaidi," alisema Waziri.
Nafasi ya Njelekela yatangazwa
Wakati hali ikiwa hivyo, nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, ilitangazwa jana kuwa iko wazi. Sifa za mtu anayetakiwa kujaza nafasi hiyo ni pamoja na Shahada ya Uzamili katika Udaktari wa Binadamu; au sifa inayolingana na hiyo katika masuala ya udaktari na upasuaji, pamoja na uzoefu wa zaidi ya miaka kumi katika uongozi wa hospitali.
Tangazo hilo lilitolewa na hospitali hiyo na lilikuwa katika gazeti la Daily News la jana, Ukurasa wa Nne. Waombaji wenye vigezo vinavyotakiwa, wanatakiwa watume maombi ya kazi hiyo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Hospitali.CHANZO:BONGO LEAKS

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...