Skip to main content

Kanda ya Ziwa yang’ara matokeo darasa la saba

 
Esther Mbussi na Adam Mkwepu, Dar es Salaam
SHULE za msingi katika mikoa ya Kanda ya Ziwa zimeongoza matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka 2014 kwa kushika namba moja hadi saba kati ya shule 10 bora kitaifa.
Aidha, watahiniwa wamefaulu zaidi somo la Kiswahili na kufeli zaidi somo la Hisabati.
Katika matokeo hayo yaliyotangazwa jana na Baraza la Mitihani la Taifa (NACTE), wavulana wameongoza somo la Hisabati kwa kupata alama 50/50, ambapo 26 wamefaulu kwa kiwango hicho na wasichana wakiwa wanane.
Akitangaza matokeo hayo, Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde, alizitaja shule 10 bora kuwa ni Twibhoki ya Mara ambayo imeshika nafasi ya kwanza, Mugini iliyoshika nafasi ya pili, Peace land na Alliance zote za Mwanza, Kwema (Shinyanga), St. Severine (Kagera), Rocken Hill (Shinyanga), Tusiime (Dar es Salaam), Imani (Kilimanjaro) na Palikas (Shinyanga).
"Kwa upande wa mikoa iliyofanya vizuri kitaifa na asilimia zake za ufaulu kwenye mabano ni Dar es Salaam (46,434), Kilimanjaro (26,192), Mwanza (37,017), Iringa (14,650), Arusha (23,250), Tanga (26,261), Njombe (11,389), Kagera (24,501), Geita (17,560) na Mtwara (15,608).
"Wilaya zilizoongoza kitaifa ni Mpanda Mji (Katavi), Biharamulo (Kagera), Moshi (Kilimanjaro), Kibaha (Pwani), Arusha (Arusha), Kinondoni (Dar es Salaam), Korogwe Vijijini (Tanga), Ilala (Dar es Salaam), Iringa (Iringa) na Mji Makambako (Njombe)," alisema Dk. Msonde.
Akizungumzia ufaulu wa kimasomo, alisema katika masomo yote umepanda kwa asilimia kati ya 0.64 na 8.94 ikilinganishwa na mwaka jana.
"Watahiniwa wamefaulu zaidi somo la Kiswahili ambapo ufaulu ni asilimia 69.70 tofauti na asilimia 69.06 ya mwaka jana, na somo walilofaulu kwa kiwango cha chini zaidi ni Hisabati lenye ufaulu wa asilimia 37.56 ambapo mwaka jana ilikuwa ni asilimia 28.62.
"Katika somo la Kiingereza watahiniwa waliofaulu kwa mwaka huu ni asilimia 38.84 ikilinganishwa na mwaka jana asilimia 35.52 na Sayansi kwa mwaka huu waliofaulu ni asilimia 54.89 na mwaka jana asilimia 47.49," alisema.
Dk. Msonde alisema jumla ya watahiniwa 451,392 kati ya 792,118 waliofanya mtihani huo wamepata alama 100 au zaidi katika alama 250 ambapo idadi hiyo ni sawa na asilimia 56.99.
Alisema kati ya watahiniwa hao, wasichana ni 226,483 ambao ni sawa na asilimia 53.59 na wavulana ni 224,909 sawa na asilimia 60.87.
Miongoni mwa watahiniwa hao waliofaulu, Dk. Msonde alisema wamo wenye ulemavu 795 wakiwamo wasichana 355 ambao ni sawa na asilimia 44.65 na wavulana 440 ambao ni sawa na asilimia 55.35.
"Katika mtihani huo uliofanyika Septemba 10 na 11, mwaka huu jumla ya watahiniwa 808,085 wa shule za msingi walisajiliwa kufanya mtihani huo wakiwamo wasichana 429,624 sawa na asilimia 53.17 na wavulana 378,461 sawa na asilimia 46.83.
"Kati ya watahiniwa hao waliosajiliwa, watahiniwa 691 walikuwa na uoni hafifu, 87 walikuwa na ulemavu wa macho (wasioona), wenye matatizo ya kusikia 374, wenye mtindio wa ubongo 252 na watahiniwa 27 walikuwa na ulemavu zaidi ya mmoja," alisema Dk. Msonde.
Pamoja na mambo mengine, NECTA imemfutia matokeo mtahiniwa mmoja aliyebainika kufanya udanganyifu katika mtihani huo. Mwaka jana watahiniwa 13 walifutiwa matokeo yao kwa kufanya udanganyifu.
Hata hivyo, Baraza hilo limesita kutoa matokeo ya shule zilizofanya vibaya kwa madai ya kuendelea na uchambuzi wa kuzitambua zaidi.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...