Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2015

Magufuli atangaza kugombea urais

Na Mwandishi Wetu, Dodoma WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, ametangaza rasmi kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Amesema kwa kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza rasmi kwa wanachama wake wenye sifa kujitokeza kuwania nafasi hiyo kubwa ya uongozi nchini, ameona hana budi kutangaza rasmi azma yake. Dk. Magufuli, mmoja wa mawaziri ambao kwa muda mrefu wamehusishwa kwenye kinyang’anyiro cha nafasi hiyo, alisema anaingia kwenye mchuano huo akiwa na sifa zote stahiki za kupiga na kupigiwa kura. Alitangaza azma yake nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, muda mfupi baada ya kumalizika kipindi cha maswali na majibu bungeni, jana asubuhi. Baada ya kuulizwa kama ana mpango huo, mara moja alisema: “Swali hili nimeulizwa mara nyingi. Mara zote nimekataa kulijibu kwa sababu chama chetu (CCM) kuna utaratibu wake wa namna ya kuomba nafasi ya uongozi. Muda ulikuwa haujawadia. “Lakini utakumbuka wiki hii hapa hapa Do

JamiiForums

JamiiForums Wanamgambo wa ISIS wamemlazimisha mateka kuchimba kaburi lake kisha kumfukia, walimhisi ni jasusi kutoka Nchini Syria. -Hivi karibuni wanamgambo wa ISIS waliukamata Mji wa kihistoria wa Palmyra.168,697 people like this.

Safari Ya Matumaini ya Edward Lowassa Itaanza Rasmi Jumamosi Hii

Inshu Ndiyo Hii Shughuli ya Lowassa Leo Je! Hao Wana CCM Wengine Wanaotarajia Kutangaza nia Wana Nguvu ya Kutosha?

Hii ndiyo shughuli ya Lowassa kesho.. Uwanja wa Sheik Amri Abeid utatapika leo ...Je! Hao wana CCM wengine wanaotarajia kutangaza nia wana nguvu ya kutosha?

Ali Kiba na Jokate pamoja tena kama marafiki !!

. Bado hawajaongea rasmi kuhusu penzi lao ila mpaka sasa wachambuzi wa mambo wamepigia mstari kuwa Ali kiba na Jokate ni wapenzi. Jibu hili wamelipata kupitia picha tofauti wanazotuonyesha wawili hawa kwenye mtandao wa instagram wakiwa wawili. Je picha hizi ni kuwatingisha tuu mashabiki, kuna project wanafanya , ni video, Tutafahamu soon

SOMA RATIBA YA DK SLAA KUANZIA KESHO ANAVYOIZUNGUKA TANZANIA

Kupitia taarifa hii kwa vyombo vya habari Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinapenda kuujulisha umma wa Watanzania kuwa Katibu Mkuu, Dk. Willibroad Slaa atafanya ziara ya kikazi katika maeneo mbalimbali ya mikoa ya Mbeya, Rukwa na Katavi, ambapo atakuwa na shughuli kadhaa, ikiwemo kukagua mwenendo wa uandikishaji wa wapiga kura unaofanyika kwa mfumo wa Biometric Voters Registration (BVR). Katika ziara hiyo ya siku 6 kuanzia Jumamosi ya Mei 30, 2015, Katibu Mkuu Dk. Slaa mbali ya kujionea zoezi hilo la BVR katika vituo vya uandikishaji, atafanya mikutano ya hadhara kwenye maeneo yote atakayozuru ambapo atazungumza na wananchi juu ya masuala yanayowahusu katika maeneo yao pamoja na mengine ya kitaifa. Kupitia shughuli hizo atakazofanya, Katibu Mkuu ataendelea kuwahamasisha Watanzania wenye sifa za kupiga kura, kujiandikisha kwa wingi katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura (DKWK) linalofanyika maeneo mbalimbali nchini kwa kutumia mfumo wa BVR. Aidha, Katibu

Marekani tayari kutuma wanajeshi Nigeria

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, John Kerry Marekani yajiandaa kutuma wakufunzi wa kijeshi nchini Nigeria kumsaidia vikosi vya kijeshi vya rais mpya Muhammadu Buhari kukuza ujuzi wao wa kijasusi. Hali mbaya kati ya washauri wa jeshi la Marekani na jeshi la Nigeria dhidi ya ukiukwaji haiza binadamu na rushwa chini ya rais aliyeshindwa Goodluck Jonathan uliathiri jitihada za kupambana vita ya miaka sita ya Boko Haram Maafisa wa Idara ya mambo ya nje ya Marekani ilisema Buhari na Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani John Kerry watajadili mustakabali wa msaada wa kiusalama na kupanua mshikamano wa kiuchumi katika mkutano baada ya kuapishwa kwa rais huyo Ijumaa. Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari Maafisa wamezungumzia hali ya sintofamu kuhusu ziara ya Kerry mjini Abuja, walisema mazungumzo na Buhari yameonyesha “ushirikiano wa karibu” na Marekani. “Tuna kila dalili kwamba tutakuwa na uwezo wa kuanza mwanzo mpya. Tunaendelea kuwa na washaur

HOTUBA YA MBUNGE SUGU LEO BUNGENI,IKO HAPA

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI MHESHIMIWA JOSEPH O. MBILINYI (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO KWA MWAKA WA FEDHA 2015/2016 (Inatolewa chini ya Kanuni ya 99(9) ya kanuni za Bunge toleo la mwaka 2013) 1.0        UTANGULIZI Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu. Namshukuru Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe. Freeman A. Mbowe kwa kuniamini kwa miaka mitano kwenye nafasi hii ya uwaziri kivuli ili kusimamia mausala ya habari, vijana, utamaduni na michezo. Pia nawapongeza wenyeviti wenza wa UKAWA, Mhe. Prof Ibrahim Lipumba  , Mwenyekiti wa CUF, Mheshimiwa James Mbatia, Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi pamoja na Mwenyekiti wa NLD Mheshimiwa Dr. Emmanuel Makaidi kwa kazi nzuri nzuri wanayoifanya ya kuwaunganisha  watanzania mpaka hivi sasa wako tayari kukiondoa Chama Cha Mapinduzi madarakani kwa ushindi wa kishind

Benteke kwenye rada

Christian Benteke akiwa na kocha wake Tim Sherwood Tim Sherwood amekubali kuwa hana nguvu ya kumzuia Christian Benteke kuondoka Aston Villa msimu huu baada ya mshambuliaji huyo Mbelgiji kuzungumzia mkataba wake. Liverpool wako tayari kumnasa Benteke, ambaye amefunga magoli 12 katika mechi 14 tangu Sherwood atue, Sportsmail inaelewa kuwa pauni milioni 32.5 zitamfanya aondoke. Benteke akishangilia goli na mchezaji mwenzake Fainali ya Kombe la FA Jumamosi dhidi ya Arsenal uwanja wa Wembley utathibitisha mwisho wa Benteke kuvaa fulana ya Vila.

Kundi la Al Shabab lapata pigo

Sheikh Hassan Turki Kundi la Al-Shabaab limetangaza kumpoteza kamanda wake Sheikh Hassan Turki aliyekuwa anasakwa na Marekani. Kwa taarifa iliyotolewa na msemaji wa kundi hilo Ali Mohamud Rage alisema kamanda Sheikh Hassan Turki mwenye umri wa miaka 73 aliaga dunia nyumbani kwake katika kijiji cha Hargeysa Yarey baada ya kuugua kwa muda mrefu. Sheikh Hassan Turki alikuwa kiongozi wa muungano wa Mahakama za Kiislamu nchini Somalia, alijumuishwa kwenye orodha ya watuhumiwa wanaotafutwa na Marekani kwa madai kuwa alikuwa analifadhili kundi hilo.

Mlinda mlango mahiri wa simba katika upendo mwingi kwa dem wake

Huyu ni mlindamlongo wa wekundu wa msimbazi , cheki hapo juu kimwana wake

Upelekaji umeme Magu wakamilika asilimia 53

UTEKELEZAJI wa upelekaji wa umeme katika vijiji kadhaa wilayani Magu umekamilika kwa asilimia 53, Bunge lilielezwa jana. Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage alisema wateja wapatao 1,887 wanatarajiwa kuunganishwa umeme katika mradi huo utakaogharimu Sh bilioni 3.35. Mwijage alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Magu, Dk Festus Limbu (CCM), aliyetaka kufahamu mradi wa kupeleka umeme kwenye vijiji vya Yichobela/ Kinango toka Irungu na Kabila toka Magu Mjini umefikia hatua gani. Naibu Waziri alisema mradi wa kupeleka umeme katika vijiji vya Yichobela na Kinango kutokea Irungu unahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 umbali wa kilometa nane. "Ujenzi wa njia ya umeme ya kilovoti 0.4 umbali wa kilometa saba na ufungaji wa transfoma tano. Mradi huu unatekelezwa na Mkandarasi Chico-CCC (BJ) JV Limited kwa uf

TONY BLAIR AJIUZULU UJUMBE WA UMOJA WA MATAIFA

Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair. Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair ametangaza kujiuzulu nafasi ya Ujumbe wa Umoja wa Kimataifa kwenye kamati inaoshughulikia usuluhishi wa migogoro ya Mashariki ya Kati Quartet. Migogoro hiyo inahusisha nchi ya Israel na Palestina nafasi ambayo ameitumikia kwa kipindi cha miaka nane tangu mwaka 2007 akiwakilisha pande nne yaani Marekani, Russia, Umoja wa Ulaya na Umoja wa Mataifa. Blair alimwandikia barua katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon kuhusu kujiuzulu kwake na kuahidi kusaidia Jumuiya ya Kimataifa katika kazi zinazohusu Israel na Palestina katika siku zijazo. Vyanzo vya habari vilivyokaribu na Blair vinasema, ataendelea kuwepo akijihusisha na baadhi ya shughuli na eneo hilo. Watoa habari hao wanasema kuwa waziri mkuu huyo wa zamani anaamini kuwa mtazamo mpya unahitajika. Lakini wakosoaji wanasema Blair alipambana katika jukumu ambalo l

Mkede sasa Full Kupagawa na Usajili wa Msimbazi

Kiungo mahiri wa Simba, Jonas Mkude amesema kuwa ujio wa kiungo Peter Mwalyanzi katika kikosi chao ni bab’kubwa na kuwatambia wapinzani wao akisema mbona mtatukoma! Mkude alisema ujio wa Mwalyanzi utatengeneza Simba mpya ambayo haitakuwa rahisi kuzuilika sambamba na kuifanya iwe inacheza soka la kuvutia litakalokuwa likitoa matokeo mazuri kwao. Mwalyanzi amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuichezea Simba akitokea Mbeya City na moja kwa moja ameingia kwenye idara ya kiungo ya Simba iliyokuwa inatawaliwa na Jonas Mkude. Mkude ameliambia mwanaspoti akisema: “Huyo jamaa (Peter Mwalyanzi) ni mmoja wa viungo mafundi, ninawakubali sana, si kwa kukimbia bali upigaji wa pasi na umiliki wa mpira. “Nimeshacheza dhidi yake akiwa Mbeya City kama mara tatu, acha kabisa, mziki wake si mchezo. Kwa kweli ninawapongeza viongozi kwa kutuletea bonge la mchezeshaji. “Sasa Simba itakuwa ni mwendo wa kupiga pasi nyingi, kupiga bao na kutwaa ubingwa. Naamini leo hii anakuja kuongeza nguvu k

Chuck Blazer atumiwa kwa kufichua kashfa za rushwa FIFA Chuck Blazer alikuwa mjumbe wa kamati tendaji ya FIFA wakati alikuwa akifanya udukuzuzi kwa niaba ya FBI katika Shirikisho la Soka Dunia Fifa kwa kipindi cha miaka miwili.

Chuck Blazer alikuwa mjumbe wa kamati tendaji ya FIFA wakati alikuwa akifanya udukuzuzi kwa niaba ya FBI katika Shirikisho la Soka Dunia Fifa kwa kipindi cha miaka miwili. Na RFI Kashfa za rushwa zinazoelezwa kwa kiasi kikubwa katika Shirikisho la Kandanda Duniani FIFA, ziliyotolewa Jumatano asubuhi wiki hii baada ya kukamatwa kwa maofisa saba wa Shirikisho hilo, ni za muda mrefu. Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Marekani, yote yalianza mwaka 2011, wakati Idara ya uchunguzi ya Marekani (FBI) ilifaulu kumshawishi Chuck Blazer kuwa afisa wake wa ujasusi. Chuck Blazer alikuwa mwanachama wa kamati tendaji ya FIFA tangu mwaka 1998 hadi mwaka 2013. Chuck Blazer alilitumikia Shirikisho la Concacaf, ambalo ni sawa ni Shirikisho la Soka Duniani FIFA. Chuck Blazer alikuwa akifanya udukuzi kwa niaba ya FBI katika Shirikisho la Soka Dunia FIFA kwa kipindi cha miaka miwili. Alikubali kuwafanyia kazi viongozi wa Marekani baada ya kugunduliwa na ma

Ubunge hautatokana na kiungo cha albino - Silima

WANASIASA wameambiwa kuwa ubunge hautatokana na kiungo cha albino na kuachana na fikra hizo potofu. Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Perreira Ame Silima amekiri bungeni kuwa ni kweli zipo taarifa kuwa baadhi ya wanasiasa wanahusishwa na imani potofu za kutumia viungo vya binadamu ili kupata madaraka. "Ni kweli habari ziko zinazungumzwa kuwa wanasiasa fulani na zinaibuka wakati kama huu ambako kuna joto kali la Uchaguzi Mkuu," alisema Silima na kuongeza: "Ubunge hautatokana na kiungo cha albino." Alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (CCM), aliyesema vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi vinaeleza kuwa wapo wanasiasa wanaotumia viungo vya albino kusaka umaarufu. "Vyombo hivi vya habari vya ndani na nje ya nchi vinaeleza kuwa wapo wanasiasa waokwenda kwa waganga na

Papa Francis aikasirisha Israel

Papa Francis akisalimiana na rais wa Palestina Mahmud Abbas Papa Francis alikutana na rais wa Palestina Mahmud Abbas siku ya Jumamosi, na kumuita “Malaika wa Amani” ikiwa ni siku kadhaa tangu Vatican ijiandae kusaini makubaliano na Palestina na hivyo kuikasirisha Israel. Abbas alikutana na kiongozi huyo wa kidini kwa takribani dakika 20 faragha, makutano yanakuja baada ya Papa kujiandaa kuwatangaza makuhani wawili wa Palestina na kuwa Waarabu wa kwanza Palestina kupewa utakatifu. Rais wa PaIestina Mahmud Abbas Siku ya Jumatano Mtakatifu huyo alitangaza kwamba anajiandaa kusaini mkataba wake na Palestina, miaka miwili baada ya kuitambua nchi hiyo kama taifa.

Kwa wasanii wa ndani Basata bado kazi ipo

Burundi:Nkurunziza ahirisha uchaguzi

Rais wa Burundia Pierre Nkurunziza ameahirisha uchaguzi wa wabunge kwa siku kumi . Msemaji wa rais Willy Nyamitwe ameiambia shirika la habari la AFP kuwa kufuatia jaribio la mapinduzi juma lililopita na vurugu zilizofuatia ni bora kuahirisha uchaguzi huo kwa muda. ''Uchaguzi huo wa ubunge ulikuwa umeratibiwa kufanyika tarehe 26 mwezi Mei lakini sasa inatubidi kuahirisha ili kuwasikiza washirika wetu wa kimataifa pamoja na tume ya uchaguzi ambayo pia inatumia muda huo kutatua maswali yaliyoulizwa na vyama vya upinzani.'' alisema Nyamitwe. Hadi kufikia sasa tarehe rasmi ya uchaguzi wa urais uliopangwa kufanywa Juni tarehe 26 haijabadilika. ''Subiri tu'' Nyamitwe aliwaambia waandishi wa habari. Mwandishi wa BBC aliyeko huko Ruth Nesoba amesema kuwa tayari rais Nkurunziza ametia sahihi amri hiyo ya kuhairishwa kwa uchaguzi. Umoja wa mataifa ya bara Ula

TIZAMA ALICHIKIFANYA PROSESA JAY NA CHADEMA YAKE HUKO MWANZA JANA

 mkutano wa chadema ambao ulifanyika jana  jijini mwanza mkutano ambao ulihutumiwa na viongozi mbalimbali wa CHADEMA akiwemo msanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya PROFESA JAY.chukua muda wako kutizama baadhi ya picha za mkutano huo

Magazeti ya leo

NYALANDU: NASARI MZUSHI

 WAZIRI Nyalandu akikagua gwaride la askari wa wanyamapori wakati akiwa  kwenye moja ya ziara zake.   Na Mwandishi wetu WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, amesema kauli zilizotolewa Bungeni na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari, ni za kutapatapa na zimejaa ukosefu wa busara na uzushi. Amesema mbunge kusimama bungeni na kutoa kashfa badala ya kueleza masuala ya kisera au kiutendaji ni kupungukiwa busara na jamii haina budi kumpuuza. Akichangia hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu bungeni juzi, Nassari alisema Nyalandu kazi yake kubwa ni kuzunguka katika mapori ya akiba na kupiga picha na askari pamoja na kushangaa mbwa wa kizungu na kupokea ndege, helkopta za msaada. Alisema utendaji huo na mawaziri wengine unaweza ukawa ni ishara ya serikali iliyochoka. Hata hivyo, katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Nyalandu alisema Nassari anapaswa kuwakilisha na kutetea wapigakura wake kwa hoja badala ya ku