Skip to main content

UN waunga mkono kazi ya Kikwete


Rais Jakaya Kikwete
Rais Jakaya Kikwete 
JUMUIYA ya Kimataifa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa (UN) jijini hapa, imeelezea msimamo wake thabiti wa kuunga mkono kwa dhati na kwa kila hali kazi na jukumu ya Jopo la Watu Mashuhuri Duniani la Kukabiliana na Majanga Duniani linaloongozwa na Rais Jakaya Kikwete.
Jumuiya hiyo imeeleza msimamo wake wa kuunga mkono Jopo hilo wakati Rais Kikwete na wana-Jopo wenzake walipopata nafasi ya kuwaelezea Wawakilishi wa Kudumu wa nchi mbali mbali duniani katika Umoja wa Mataifa kuhusu kazi iliyofanywa na Jopo hilo katika siku za mwanzo kabisa.
Jopo hilo lililotangazwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon Aprili 2, mwaka huu, limepewa jukumu ya kupendekeza jinsi gani dunia inavyoweza kukabiliana na majanga ya kiafya duniani, na hasa magonjwa ya milipuko, kama ilivyokuwa ebola katika nchi za Afrika Magharibi za Guinea, Liberia bna Sierra Leone.
Baada ya wiki moja ya kazi kubwa mjini New York, Rais Kikwete na wajumbe wa Jopo hilo kutoka Brazil, Botswana, Indonesia, Uswisi na Marekani, walikutana na Wawakilishi wa Kudumu wa mataifa mbali mbali katika UN kuwaelezea nini kimefanyika na nini kinatarajia kufanyika.
Baada ya maelezo ya wajumbe wa Jopo, mwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani katika UN alisema kuwa Ujerumani inaunga mkono moja kwa moja kazi ya Jopo hilo akisisitiza kuwa Kiongozi wa Ujerumani, Kansela Merkel amekubali kutoa kiasi cha dola za Marekani milioni moja (sh bilioni 1.9) kuunga mkono shughuli za Jopo hilo.
Mwakilishi wa Senegal alisema kuwa nchi yake inaunga mkono moja kwa moja kazi ya Jopo hilo lililoteuliwa na Katibu Mkuu wa UN, akisisitiza kuwa Senegal, kama Mwenyekiti wa Kamati ya Oslo ya Afya katika Umoja wa Mataifa itashirikiana na Jopo hilo moja kwa moja.
Mwakilishi wa Ufaransa alisema kuwa nchi yake inaunga mkono kazi ya Jopo moja kwa moja na kuwa ni uamuzi wa busara wa Katibu Mkuu wa UN kuunda Jopo hilo.
Mwakilishi wa Uingereza alipokea kwa mikono miwili uundwaji wa Jopo hilo, akisisitiza kuwa nchi hiyo itaendelea kuunga mkono jitihada za Jopo hilo kama ilivyoiunga mkono Sierra Leone wakati wa kukabiliana na ebola.
Mwakilishi wa Luxembourg alisema kuwa dunia inalitarajia Jopo hilo kuelekeza nguvu yake katika mapendekezo ya uongozi kuliko changamoto za kiufundi.
Aidha, ameongeza kuwa nchi hiyo baada ya kushika Uenyekiti wa Umoja wa Ulaya (EU) itaongeza kazi yake katika kuchunguza athari za ebola na kiini chake.CHANZO: HABARI LEO (Muro)

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.