Marouane Fellaini ameeleza kwa kina kwamba kocha Louis van Gaal atadhibiti nidhamu Manchester United.
Fellaini alieleza namna Mholanzi huyo, ambaye aliwasili akiwa na heshima kama kiongozi mwenye msimamo, ameagiza kuwepo na faini endapo wachezaji watakiuka maagizo, ikiwemo kulinda muda.
Akizungumza kuelekea mechi ya United dhidi ya Crystal Palace, Fellaini alisema: “Alifoka siku fulani wakati kikundi cha watu 10 kati yetu kilipochelewa dakika moja kula chakula cha mchana baada ya mazoezi.
“Unafikiri dakika moja si chochote na haikuwa kwa mazoezi, ila kwa ajili ya chakula. Kwake yeye ni jambo muhimu.
“Alitupiga faini. Hivyo ndivyo inavyotokea kwa wachelewaji hata kwa kadi nyekundu. Unatozwa faini, pia hata ukicheza rafu mbaya.”
Fellaini alieleza namna Mholanzi huyo, ambaye aliwasili akiwa na heshima kama kiongozi mwenye msimamo, ameagiza kuwepo na faini endapo wachezaji watakiuka maagizo, ikiwemo kulinda muda.
Akizungumza kuelekea mechi ya United dhidi ya Crystal Palace, Fellaini alisema: “Alifoka siku fulani wakati kikundi cha watu 10 kati yetu kilipochelewa dakika moja kula chakula cha mchana baada ya mazoezi.
“Unafikiri dakika moja si chochote na haikuwa kwa mazoezi, ila kwa ajili ya chakula. Kwake yeye ni jambo muhimu.
“Alitupiga faini. Hivyo ndivyo inavyotokea kwa wachelewaji hata kwa kadi nyekundu. Unatozwa faini, pia hata ukicheza rafu mbaya.”
Comments