Skip to main content

Ubunge hautatokana na kiungo cha albino - Silima



bunge1
WANASIASA wameambiwa kuwa ubunge hautatokana na kiungo cha albino na kuachana na fikra hizo potofu.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Perreira Ame Silima amekiri bungeni kuwa ni kweli zipo taarifa kuwa baadhi ya wanasiasa wanahusishwa na imani potofu za kutumia viungo vya binadamu ili kupata madaraka.
"Ni kweli habari ziko zinazungumzwa kuwa wanasiasa fulani na zinaibuka wakati kama huu ambako kuna joto kali la Uchaguzi Mkuu," alisema Silima na kuongeza: "Ubunge hautatokana na kiungo cha albino."
Alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (CCM), aliyesema vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi vinaeleza kuwa wapo wanasiasa wanaotumia viungo vya albino kusaka umaarufu.
"Vyombo hivi vya habari vya ndani na nje ya nchi vinaeleza kuwa wapo wanasiasa waokwenda kwa waganga na kutumia viungo vya albino kujitafutia umaarufu. Kwa nini serikali isiwabane waandishi hawa ili iwataje wanasiasa hao ili wasiohusika wasitiwe doa," alihoji mbunge huyo wa Rombo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani alisema serikali imekuwa ikifanya jitihada kubwa katika kukabiliana na tatizo la mauaji ya watu wenye ulemavu, na kuwa lazima jamii kuanzia ngazi ya familia ibadili fikra zao.
Alisema haiwezekani albino wauawe katika baadhi ya mikoa au eneo fulani tu la nchi, hivyo elimu inahitajika kwa watu husika na kuwa serikali itaendelea kuchukua hatua zikiwamo za kuielimisha jamii.
Aidha, alisema kifaa maalumu kitakachofungwa kwa albino ili kufuatilia mienendo yao, kinaendelea kufanyiwa kazi na serikali ili kufahamu kama teknolojia kinafanya kazi na pia kufahamu kama ni salama.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Jenista Mhagama, alisema serikali haijalidanganya Bunge kuhusu kifaa hicho, na kuwataka wabunge kuungana pamoja na serikali katika kukomesha mauaji hayo yanayolitia aibu Taifa.
Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Philipa Mturano (Chadema), Silima alisema mpaka sasa watu 15 wa mauaji ya albino, wamekamatwa, kufikishwa mahakamani na kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa.(HABARI LEO)
(KILONGE)

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.