Skip to main content

Mji wa Beni watikiswa na maandamano



beni
Wakazi wa mji wa Beni mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamelalamikia mauaji ya watu wengi yaliyotokea hivi karibuni katika mji huo.
Wakazi wa mji huo jana walisitisha kazi zao zote kama ishara ya kulalamikia mauaji hayo ya umati.
Wakazi wa mji wa Beni wanavilaumu vikosi vya serikali ya nchi hiyo kushindwa kuwalinda raia. 
Gilbert Kambale mmoja wa viongozi wa asasi za kiraia amesema kuwa, wakazi wa mji huo wataendelea kusimamisha shughuli zao za kawaida kwa muda usiojulikana na kwamba, wanaitaka serikali imfute kazi kamanda wa vikosi vya serikali vya Operesheni ya Sukola-1 kutokana na kushindwa kulinda roho za watu wa mji huo.

Comments