Skip to main content

Upelekaji umeme Magu wakamilika asilimia 53



UTEKELEZAJI wa upelekaji wa umeme katika vijiji kadhaa wilayani Magu umekamilika kwa asilimia 53, Bunge lilielezwa jana.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage alisema wateja wapatao 1,887 wanatarajiwa kuunganishwa umeme katika mradi huo utakaogharimu Sh bilioni 3.35.
Mwijage alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Magu, Dk Festus Limbu (CCM), aliyetaka kufahamu mradi wa kupeleka umeme kwenye vijiji vya Yichobela/ Kinango toka Irungu na Kabila toka Magu Mjini umefikia hatua gani.
Naibu Waziri alisema mradi wa kupeleka umeme katika vijiji vya Yichobela na Kinango kutokea Irungu unahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 umbali wa kilometa nane.
"Ujenzi wa njia ya umeme ya kilovoti 0.4 umbali wa kilometa saba na ufungaji wa transfoma tano. Mradi huu unatekelezwa na Mkandarasi Chico-CCC (BJ) JV Limited kwa ufadhili wa Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Awamu ya Pili," alieleza Naibu Waziri.
Alisema mpaka sasa ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 umekamilika kwa asilimia 100; kazi ya upimaji na michoro ya njia ya msongo wa kilovoti 0.4 imekamilika kwa asilimia 100 na mkandarasi ameshaleta nguzo zote na transfoma tano kumalizia kazi zilizosalia.
"Mradi wa umeme kutokea Magu Mjini kuelekea Kabila kupitia Itumbili, Kitongo, Sukuma Sekondari, Lumeji, Busalanga, Nhaya Sekondari, Nhaya Senta na Mwashepi unahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 umbali wa kilometa 28; ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 0.4 umbali wa kilometa 10 na ufungaji wa transfoma 18," alieleza Mwijage.(HABARI LEO)

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...