Skip to main content

SOMA RATIBA YA DK SLAA KUANZIA KESHO ANAVYOIZUNGUKA TANZANIA


Kupitia taarifa hii kwa vyombo vya habari Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinapenda kuujulisha umma wa Watanzania kuwa Katibu Mkuu, Dk. Willibroad Slaa atafanya ziara ya kikazi katika maeneo mbalimbali ya mikoa ya Mbeya, Rukwa na Katavi, ambapo atakuwa na shughuli kadhaa, ikiwemo kukagua mwenendo wa uandikishaji wa wapiga kura unaofanyika kwa mfumo wa Biometric Voters Registration (BVR).


Katika ziara hiyo ya siku 6 kuanzia Jumamosi ya Mei 30, 2015, Katibu Mkuu Dk. Slaa mbali ya kujionea zoezi hilo la BVR katika vituo vya uandikishaji, atafanya mikutano ya hadhara kwenye maeneo yote atakayozuru ambapo atazungumza na wananchi juu ya masuala yanayowahusu katika maeneo yao pamoja na mengine ya kitaifa.

Kupitia shughuli hizo atakazofanya, Katibu Mkuu ataendelea kuwahamasisha Watanzania wenye sifa za kupiga kura, kujiandikisha kwa wingi katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura (DKWK) linalofanyika maeneo mbalimbali nchini kwa kutumia mfumo wa BVR.

Aidha, Katibu Mkuu Dk. Slaa atatumia fursa hiyo kukagua shughuli mbalimbali za chama zinazofanywa na viongozi na watendaji wa CHADEMA katika kanda za chama; Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ambayo inajumuisha mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe, Ruvuma Rukwa pia Kanda ya Magharibi yenye mikoa ya Kigoma, Tabora na Katavi.

Katibu Mkuu pia atapata fursa ya kukutana na viongozi na watendaji wa chama wa ngazi za chini katika kanda hizo na kusikia kutoka kwao namna wanavyoendelea kutekeleza programu na mikakati waliyojipangia katika maeneo yao au kuelekezwa na vikao vya chama, ikiwa ni sehemu ya kuzidi kukiandaa chama na UKAWA yaani vyama vinne (NLD, NCCR-Mageuzi, CUF na CHADEMA), kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Ratiba ya ziara ya Katibu Mkuu Dk. Slaa itakuwa kama ifuatavyo;
1.      Jumamosi Mei 30, 2015 - Mbozi (Vwawa) atafanya mkutano wa hadhara Uwanja wa Ichenjezya.
2.      Jumapili Mei 31, 2015 – Tunduma- Mbeya, atafanya mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Shule ya Msingi Tunduma.
3.      Jumatatu Juni 1, 2015 – Sumbawanga- Rukwa, atafanya mkutano wa hadhara Uwanja wa Stendi ya Chanji, mjini Sumbawanga.
4.      Jumanne Juni 2, 2015 – Mpanda Mjini- Katavi, atafanya mkutano katika Uwanja wa Kashaulili.

Itakumbukwa kuwa Katibu Mkuu Dk. Slaa alifanya ziara ya siku 3 hivi karibuni katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Kagera ambako alishuhudia udhaifu na mapungufu makubwa katika uandikishaji wa BVR, ikiwemo wananchi kutishwa, kupigwa, kuzuiwa kujiandikisha na viongozi wa CCM wakiwa vituoni, mashine kutofanya kazi, siku za kuandikishwa kutojulikana na uandikishaji kufanyika ‘electronically na manually’ bila maelezo yoyote kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Imetolewa leo Ijumaa, Mei 29, 2015 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano

CHADEMA

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...