Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2018

TIC : Cha jipambanua katika jitihada zake za kutangaza fursa za uwekezaji

MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Geoffrey Mwambe amefanya ziara ya kikazi nchini Ujerumani na Uholanzi kati ya  Mei 14 na 17 mwaka huu katika jitihada zake za kutangaza fursa  za uwekezaji  ili kushawishi na kuvutia wawekezaji kuja kuwekeza nchini. Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji  Tanzania Bw. Geoffrey Mwambe (kulia) alipomtembelea  Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mhe. Dkt. Possi Abdallah ofisini kwake Berlin, Ujeruman    Akiwa nchini Ujerumani Bw. Mwambe alisema lipokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mhe. Dkt. Possi Abdallah ambapo walifanya kikao cha kazi kabla  ya kushiriki kongamano la biashara na uwekezaji kati ya Ujerumani na nchi za Afrika Mashariki lililofanyika Mei 15, 2018 katika mji wa Berlin. Pichani   baada ya kukamilisha zoezi la kusaini MOC . waliokaa kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Bw. Geoffrey Mwambe na kushoto ni Mwenyekiti wa DCIB Bw. Hans Biesheuvel. Pa

Leo siku ya Mazingira Duniani

Elimu zaidi inahitajika kuhifadhi mazingira nchini WAKATI  Mataifa mbalimbali yanaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani yanayofikia kilele chake hapo Juni 5, 2017, takriban hekta 372,000 za misitu hupotea kila mwaka nchini Tanzania kutokana na shughuli mbalimbali.  Kwa miaka mingi siku ya Mazingira duniani imekuwa ikiadhimishwa kwa Wadau katika nchi mbalimbali kuchukua hatua chanya zinazohusu mazingira. Siku hii pia imekuwa ni sehemu ya kampeni ya utoaji elimu juu ya maswala yanayojitokeza kuhusiana na mazingira. Kauli mbiu katika maadhimisho ya mwaka huu inasema “Mahusiano Endelevu Kati ya Binadamu na Mazingira” ikihamasisha jamii kuwa na urafiki endelevu na mazingira asilia ambapo kila mtu anapaswa kutambua, kufurahi, kujivunia na kulinda uzuri wa mazingira asilia na kuhamasishana ili kuyatunza na kuyahifadhi.    Tanzania kama ilivyo kwa nchi nyingi Barani Afrika na duniani kwa ujumla imeendelea kuathirika kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa mazingira unaotokana n

Diwani wa Kata ya Kijiji awapa fursa ya kusoma mafunzo ya kompyuta vijana 200

Diwani wa Kata ya Kijichi Eliyasa Kasim Mtarawanje  Jumla ya vijana wapatao 200 wa kata ya Kijichi iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke jijini Dar es salaam wamepata fursa ya kusoma mafunzo ya kompyuta ili kuendelea kukuza wigo wa kujiendeleza kiuchumi. Mafunzo hayo ambayo yanatolewa bure katika kata hiyo ikiwa ni Moja ya mikakati ya kimaendeleo inayofanywa na Diwani wa Kata ya Kijichi Eliyasa Kasim Mtarawanje katika kuhakikisha vijana wanajipatia ujuzi utakaowasaidia kuweza kujikwamu kiuchumi katika ufanyaji wa kazi. Akizungumza jana Dar es Salaam  Diwani Mtarawanje alisema amewatafuta wafadhili Digital Oportunity Trust (DOT) ili kuweza kuwasaidia vijana kuweza kujifunza mafunzo ya elimu ya kompyuta. "Tunawashukuru sana hawa watu wa DOT kwa kutupatia fursa hii kwani takribani ya vijana 60 tayari wameshahitimu na wamepewa vyeti vyao,ambapo kila mtaa wametoka vijana 12 na ndani ya vijana hao 12 tumewapeleka vijana kufanya kazi na h

Benki ya CRDB yapunguza riba hadi 16% na kuongeza muda wa kulipa mkopo hadi miaka 7 kwa mikopo ya Wafanyakazi

Benki ya CRDB imeanzisha utaratibu wa kununua mikopo kwa wateja ambao wamekopa katika taasisi na benki nyingine kuwapa fursa ya kukopa katika Benki yao pendwa ya CRDB ambapo mikopo hiyo itatolewa ndani ya siku moja kupitia matawi husika. Wafanyakazi wenye mikopo Benki ya CRDB watapewa TemboCard Visa Gold,Wafanyakazi pia wana fursa ya kupata kadi za mkopo za “TemboCard World Reward” na “TemboCard Gold Credit” ambazo huwezesha kupata mkopo bila riba. Akizungumza katika mkutano wake na Waandishi Wahabari Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya hiyo Dokta Charles Kimei alisema Benki ya wametangaza punguzo la riba kwa mikopo ya wafanyakazi kutoka asilimia 22 hadi asilimia 16 na kuifanya mikopo ya wafanyakazi Benki ya CRDB kuwa na riba ndogo zaidi katika soko. Alisema benki hiyo imeamua kupunguza riba ili kutoa unafuu na kurahisisha upatikanaji wa mikopo kwa wateja wake na Watanzania kwa ujumla jambo litakalo saidia kuchochea kukua kwa uchumi wa mtu m

Jafo awaagiza Makatibu Tawala wa Mikoa kutoa Takwimu za Wazee ifikapo 30 Juni, 2018

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Seleman Jafo, akizungumza wakati wa Hafla ya kuwapatia Vitambulisho Wazee wa Jiji la Dodoma. Na. Atley Kuni-OR TAMISEMI Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo (Mb), amewaagiza Makatibu Tawala wa Mikoa Tanzania Bara kuwasilisha taarifa za takwimu za wazee ifikapo 30, Juni 2018. Waziri Jafo, alitoa kauli hiyo mapema leo alipokuwa akizindua zoezi la kuwapatia vitambulisho maalum wazee wapatao 1,118 wa Jiji la Dodoma kutoka kata za Mkonze, Mnadani, Uhuru, Madukani, Makole na Majengo. Vitambulisho hivyo, pamoja na mambo mengine vitawawezesha wazee hao kupata huduma za afya bure na kwa wakati. “Ifikapo tarehe 15 Juni, 2018 kila kata iwe imetambua wazee na ifikapo tarehe 22 Juni, 2018 kila Halmashauri iwe imeunganisha taarifa za wazee kutoka katika kata zake zote” alisema Waziri. Aidha Waziri Jafo aliagiza kuwa, “ifikapo Juni, 26, 2018 kila Mkoa uwe umeunganisha

Kiungo mkongwe wa Kibrazil anatarajiwa kufunga ndoa na vimwana wawili kwa mpigo ndani ya siku moja

Kiungo mkongwe wa Kibrazil – RONALDINHO anatarajiwa kufunga ndoa na vimwana wawili kwa mpigo ndani ya siku moja. Ndoa hiyo itafungwa mwezi Agust ambapo staa huyo atawahalalisha wapenzi wake hao wawili Priscilla Coelho na Beatriz Souza kuwa wake zake halali. Inasemekana wanawake hao wawili wamekuwa wakiishi na Ronaldhino kwenye jumba lake la pauni milioni 5 huko Rio de Janeiro tangu mwezi Disemba mwaka jan a

Askofu Dr.Malasusa azindua jengo la kanisa la ushirika wa kimara

ASKOFU wa dayosisi ya mashariki na pwani Dr.Alex Malasusa jana amezindua jengo  la kanisa la ushirika wa kimara lenye thamani ya shilingi billion 5.1 na kuhimiza  ushirikiano,upendo na amani katika kuleta maendeleo. Mbali na hilo Askofu amezindua shule ya awali na msingi ya Jerusaremu sambamba na kuweka jiwe la msingi katika kituo cha kulelea watoto yatima na hospitali itakayotoa huduma mbali mbali ikiwemo rufaa . Tukio hilo lilitokea jana Dar es Salaam na kuandika historia kubwa ya kipekee katika  ujenzi wa makanisa hapa nchini ambapo wageni kutoka makanisa mengine walihudhuria sambamba na kutoa salamu zao . Askofu alisema makanisa yapo duniani kwaajili ya kusambaza upendo kwa watu wote na uponywaji wa kiroho ambapo mwanadamu haponi kwa sindano na vidonge bali uponywa kwa neno la Mungu. "Kanisa lazima kitovu cha upatanishi hivyo wakazi wa eneo hili dumisheni upendo katika kumtumikia Mungu na kuwa chachu ya maendeleo na kuwa wazazi wapeleke w

Heavy flooding ravages Baltimore-metro city

Simba kuwatema mastaa kibao msimu ujao

Kocha Mfaransa Pierre Lechantre, amepanga kufumua kikosi chake na kukisuka upya kwa mashindano ya Ligi Kuu Tanzania Bara na mashindano ya kimataifa. Katika mkakati huo, Lechantre anatarajia kuwatema wachezaji zaidi ya saba ili kutoa nafasi kwa wapya kusajiliwa. Simba inatarajiwa kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara msimu huu. Hata hivyo, Lechantre atakuwa na uhakika wa kutimiza ndoto yake endapo klabu ya Simba itamuongeza mkataba mpya. Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ alisema mkataba wa Lechantre unatarajiwa kujadiliwa na Kamati ya Utendaji baada ya kumalizika mechi za Ligi Kuu Jumatatu wiki ijayo. Akizungumza jana, Lechantre alisema anataka kuisuka Simba iwe na nguvu ya kushindana na miamba mingine ya soka Afrika katika mashindano ya kimataifa, hivyo atalazimika kuwatema baadhi ya wachezaji maarufu. Panga la wachezaji saba linatarajia kuwapitia Juuko Murshid, Laudit Mavugo, Juma Li

Baby kuanza kutikisa upya anga za filamu

MSANII wa filamu nchini Marry Nicolous a.k.a Baby ambaye amekamilisha ujio wa filamu kama Nguvu ya Neno,Chimvula,Haiba ya Moyo amesema kuwa katika muda mchache kuanzia sasa zitaanza kuoneshwa kupitia Dstv.Moja ya ushawishi mkubwa kuona kazi ya msanii inakuwa katika kiwango bora ni kazi ya msanii kukubalika kuoneshwa katika channel kubwa . Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili Dar es Salaam Baby amesema katika nyakati za sasa wasanii wamekuwa wakifanya biashara na vituo vya  luninga kubwa kama channel ya Dstv ila wanachukua filamu zenye ubora mkubwa. Alisema anafurahishwa na hali ya kupokelewa vyema kwa filamu zake katika luninga hiyo iliyopo Afrika Kusini kwa mkataba na channel hiyo utakuwa wenye maslahi mazuri. "Mania ya kufikia malengo mengine makubwa sana katika anga za filamu , mara  tu filamu hizo zitakapoanza kurushwa katika luninga hiyo kubwa barani Afrika kazi zangu nyingine zitafuata nimepania kuwa mwanamke mwenye muonekano mzuri wa kimafanikio kupitia sana

Idara ya Huduma za Kinga nchini imejipanga kukabiliana na ugonjwa wa Ebola

IDARA ya Huduma za Kinga  ya Wizara ya Afya ,Maendeleo ya    Jamii ,Jinsia ,Wazee na Watoto imesema ugonjwa wa Ebola ni janga hivyo serikali   imejipanga kukabiliana nao. Ugonjwa huo ambao tayari umeripotiwa kuwapo Jamhuri ya Kidemokirasia ya Congo (DRC) tangu mei 8 mwaka huu na hadi kufikia sasa watu 51 wameri potiwa kupata maambukizi na 27 kati yao wamefariki dunia. Hayo yamesemwa Jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita na Kaimu Mkurugenzi  wa Idara hiyo Dkt.Khalid Massa wakati wa kikao cha tathimini  kati ya Kamati  ya Kitaifa ya kukabiliana na magonjwa ya Mlipuko. Alisema Tanzania tumewekwa nafasi ya pili miongoni mwa nchi zenye uwezekano  wa kupata maambukizi ya ugonjwa huo kwa haraka kwa kuwa tupo jirani  na DRC . "Ugonjwa huo ulishawahi kutokea miaka ya nyuma katika baadhi ya nchi zilizopo Barani Afrika na katika kipindi hicho waliweza kuwapa mafunzo wataalamu wao na wapo walio kwenda kusaidia katika baadhi ya nchi ,"alisema  Dkt. Massa.

Kesi ya AG Kilangi na wananchi wa Vicheji mgogoro wa ardhi kusikilizwa Julai 26

Hussein Ndubikile,Pwani Baraza  la Ardhi na Nyumba la Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani  limesema Julai 26 mwaka huu litaanza kuisikiliza kesi ya msingi ya mgogoro wa ardhi kati ya  Mwanasheria Mkuu wa Serikali(AG), Adelardus Kilangi ambaye ni mdai dhidi ya wadaiwa zaidi ya 70 ambao ni wananchi wa Kijiji cha Vicheji kilichopo wilayani humo. Hatua hiyo imdikiwa jana wakati Mwenyekiti wa baraza hilo Mwakibuja alipokuwa akisoma uamuzi wa mapingamizi yaliyowasilishwa na pande mbili katika shauri hilo. Akisoma uamuzi huo leo wialyani humo, Mwenyekiti Mwakibuja aliitupilia mbali hoja ya mdai Kilangi ambayo iliwasilishwa kwa maandishi barazani hapo kupitia wakili wake Daudi Maginge Kuwa wadaiwa hawana nguvu ya kumshtaki.. " Baraza linatupilia mbali hoja hiyo kwa kuwa kila raia ana haki ya kushtaki na kushtakiwa,' Anadai Mwenyekiti Mwakibuja. Pande mbili zilwasilisha mapingamizi mbalimbali kwa maandishi huku wadaiwa wakiliomba baraza limuongeze mwe

Kikao cha Chama cha Mapinduzi

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akata utepe kufungua Kituo cha Polisi cha Kiluvya wilayani Ubungo

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe kufungua Kituo cha Polisi cha Kiluvya wilayani Ubungo Mei 24, 2018. Wapili kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhadisi, Hamad masauni na wanne kukhoto ni Inspekta Jenerali wa Polisi, Simon Siro, Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa a Dar es salaam na Mkuu wa wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva. (Picha na Ofiosi ya Waziri Mkuu)  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Inspekta Jenerali wa Polisi, Simon Siro baada ya kufungua Kituo cha Polisi cha Mbweni Wilayani Kawe, Mei 24, 2018. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisoma hotuba ya bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2018/2019 bungeni jijini Dodoma.  Mapema leo Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepisha kiasi cha Shilingi Bilioni Mia Moja Sabini na Saba, Milioni Sita na Mia Mbili Thelathini na Mbili Elfu. Kati ya fedha hizo Shilingi Bilioni Mia Moja Sitini na Sita, Milioni Mia Sita na Sita, na Mia Mbili Thelathini na Mbili Elfu ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida, na Shilingi Bilioni Kumi na Milioni Mia Nne ni kwa ajili ya bajeti ya maendeleo.  Prof. Adolf F. Mkenda Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,(wa kwanza kushoto) akifuatilia uwasilishwaji wa hotuba ya bajeti ya Wizara. Wa pili kutoka kushoto, ni Naibu Katibu Mkuu Balozi Ramadhani Mwinyi akifuatilia hotuba Sehemu ya Watendaji wa Wizara wakifuatilia hotuba ya bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2018/201